Watanganyika wanaoitetea DP World wana matatizo ya akili?

Watanganyika wanaoitetea DP World wana matatizo ya akili?

Ukiona mtu hajadili hoja akaanza kumzodoa mtoa hoja, akaanza tafuta makandokando ya hoja, basi jua hoja hiyo ina mashiko na mjibu hoja ameshindwa.

Mtu anaanza tafuta vyuo vilivyopo malaysia, maana yake hoja kuu imemshinda kujibu.

Mtu akianza tafuta dini ya mleta hoja, basi hoja kuu imemshinda.

Uzuri Samia ameshasikia hoja, na hili tamko la TEC ndio msumali wa mwisho, watayazingatia tu matakwa ya Watu.

Sisi waislam tuache kujitoa akili. Hakuna anayepinga hili suala sababu ya dini. Waturuki wanajenga reli hakuna aliyewapinga. Wairan wanamashirikiano na jeshi letu, toka enzi za Jakaya na haijawahi kuwa shida.

Mkataba wa Richmond tuliupinga si kwa sababu wazungu ni wakristo.

Juzi nasikia wale waimba mapambio wa wasafi, wanasema kama kuna mapungufu yarekebishwe maana muwekezaji hawezi fanya kazi ikiwa wananchi hawataki-wameanza legea.

Samia ameshasikia, atatii tu, hawa court jesters wa mitandaoni ni vifuata upepo tu.
Samia ameshasikia, atatii tu, hawa court jesters wa mitandaoni ni vifuata upepo tu.[emoji419][emoji375]
 
Wewe tunajua umo kwenye wale wataopunguzwa pale bandarini tanua dawa iingie
 
Kuna kiongozi mkubwa hata mimi nilimsikia alisema watanzania milioni 60 wameshindwa kusimamia bandari ina pata hasara.nikasikia ikitoa suluhu kwamba eti Wapewe DP World milele. Nilijiuza mbona mimi mtanzania ila sijawai pewa nafsi nitashindwa nilishangaa sana
 
Aliyekwambia nina uchu wa uongozi ni nani?
Fanya hivi
ee1d182305a30d7b43bd2911de0a77fc.jpg
 
Kuna kiongozi mkubwa hata mimi nilimsikia alisema watanzania milioni 60 wameshindwa kusimamia bandari ina pata hasara.nikasikia ikitoa suluhu kwamba eti Wapewe DP World milele. Nilijiuza mbona mimi mtanzania ila sijawai pewa nafsi nitashindwa nilishangaa sana
Hata mimi sijashindwa!
 
Unamkuta mtu mmoja ana kichwa kikubwa kabisa, anasema DPW wapewe bandari kwakuwa bandari imekuwa ikiendeshwa bila ufanisi.

Mtu mjinga kama huyo ameshindwa kabisa kufikiri na kuona aibu kwamba nchi yenye watu zaidi ya million 60 inakosa watu wa kusimamia bandari ifanye kazi kwa ufanisi na anashangilia ibinafsishe kwa Nchi ya ugenini.

Nchi hii ina watu wajinga sana, pengine kwa ujinga Duniani sisi tunashika nafasi ya kwanza, pili na ya tatu.
Hao wenye vichwa vikubwa kama simtank ni Viongozi walioamua kukaza shingo na kufikiri kwa kutumia makalio huku wakivimbiwa na khalua za tende

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Sikumbuki Gazeti, ila nililisoma miaka ya 2000 kipindi cha utawala wa Dr. Mkapa. Kwenye hilo Gazeti, kulikuwa na makala yaliyodadavua kile kilichosemekana mahojiano ya BBC na mfanyabiashara mwenye asili ya India.

Huyo mfanyabishara alitaka kuwekeza kwenye ufugaji wa Kamba, nafikiri, kwenye bonde la Mto Rufiji, lakini mpango wake ulikwama baada ya Serikali kumnyima kibali.

Alipoulizwa juu ya fursa zilizopo Tanzania, alisema, " Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo unaweza ukaenda ukiwa maskini ukarudi ukiwa tajiri".
Ni sahihi..
 
Back
Top Bottom