kutumia matusi kujibu hoja za wassira hapa JF kumbe nayo ni maendeleo. hakika demokrasia inashamiri.
Haitasaidia, wasipoteze muda maana wanamajukumu mengi ya kutenda ili kujibu hoja za CDM. Kama ni kweli wanampango huo, basi ni dhahiri tusitegemee Ufisadi kwisha, DOWANS na mikataba mingine feki kushughulikiwa kiadilifu nk. Yani pamoja na ushauri mwingi niliousoma hapa JF na kwingineko bado hawajifunzi. Kweli nimeamini ule usemi wa wenzetu usemao mbwa mzee huwezi kumfundisha mbinu mpya.
eti mpaka leo hii anategemea kilimo cha mvua kiondoe njaa!
Si wawashitaki viongozi hao wa CDM wanaotuhumiwa kwa uhaini, uchochezi, majungu na fitna mbaya kwa JK. Mbona kila siku kulalamika sasa tutashindwa kuelewa kama serikali inaiogopa CDM au?Bado anasema Chadema wanataka kuiondoa serikali kwa mabavu.
Ni kama mimi ninavyofikiria kuchoma nyumba kwa maji ya moto (100% C).eti mpaka leo hii anategemea kilimo cha mvua kiondoe njaa!
.
Kuna jamaa juzi alinivunja mbavu. Eti dereva wa wasira aliwahikamatwa na askari wa mbuga ya serengeti. Siku hiyo walikuwa wametoka mara wakiwawanacross mbuga ghafla wakakuta geti la askari wa Tanapa, wakati huo mh. Alikuwa ameuchapa usingizi kwenye kiti cha nyuma baada ya hao askari kulikagua gari wakamwambia dereva uko chini ya ulinzi, alipohoji sababu akajibiwa kwamba amebeba nyara za serikali kwa nia ya kuzitorosha. Ndipo dereva alipojitetea kuwa "jamani hizi siyo nyara za serikali bali ni mh, waziri wa serikali"
.