King Zenji
Senior Member
- Feb 18, 2008
- 178
- 18
Jamani kwanza wanajamii kama ni great thinker hatupaswi kutoa mitusi, hakuna mshindi kwenye Mitusi na haisaidii, maana sisi ndo wakuwaongoza kina wasira, sasa mnamuita sura mbaya nani mwanaume mzuri? Kama mzuri ujue unauza na wewe, pia hatuwezi hata kuumba kidole chake kwanini tunadharau umbile la mtu. Na kama uzuri ungekua uongozi basi Richard wa big brohter angekua raisi, Tuongeleeni hoja zake zaidi.
Nimemsikiliza Wasira, Pia nilimsikiliza na Tendwa TBC taifa siku mbili za nyuma wote wanaongea vitu vinafanana, Kama wanaCDM lisemwalo lipo tuwe waungwana zaidi tusifanye mambo ya ujanja ujanja, Arusha mabomu yamepigwa juzi kesi ilipoahirishwa watu wanataka waandamane wawapeleke viongozi ofisin kwa ruhusa ya nani? Matendo ya Chadema yanonyesha wazi hawajakubaliana na Matokeo ya uchaguzi ambao ndio chaguo la wengi.
Hatukubali kuwa RAIS amepata kura 5M, wakati CDM 2M, wabunge 178 majimbo, CMD 25 sasa CDM inataka nchi hawa waliowachagua hawa wabunge 178 mtawapeleka wapi? Mtawashawishi wawaunge mkono? Au mtawaua? Nchi sio Arusha, Mwanza na MBEYA. ni pamoja na lindi, singida na TABORA, nani atasema kua MKONO ameiba kura Musoma vijijini? Nani atasema NYARANDU ameiba kura Singida? nani atasema RAGE ameiba kura TABORA? Hawa wamepewa kura na wananchi ambao na hakika ni wengi kuliko wa Mikoa ya chadema tusidharau hili
Muhimu chadema tukubali kuwa ni suprise kuangakuka lakini ndo imetokea tayari, tuwe wapole tusubiri 2015
Chadema wanasema Kikwete kashindwa kuendesha nchi wakati BAJETI YA KWANZA ndo inapelekwa mwezi Juni ameshindwa vipi kabla ya mipango. hata chadema ingekua madarakani ingetumia bajeti na mipango iliyopo mpaka hapo juni ndo wangeweza kurekebisha. Siku mia mnataka rais amalize matatizo ya watanzania tuwe kama libya maji bure, umeme bure, ukioa nyumba unapewa.
Mbona majomboni mimi sijaona walkichofanya wabunge zaidi ya kuita wapiga picha kupiga picha matrekta, trekta la milion saba litatatua matatizo ya wannchi wa jimbo kwani hiyo ni SACCOS?
Awangalie wabunge wenzake wa MUSOMA ameweka Grader na engineer, angalia Mo singida anafanya nini
TUACHE MANENO TUCHAPE KAZI
KUCHAMBA KWINGI MWISHO...., CDM tuache kuchamba maana.........
,,,,,,Yote kwa yote,MASWALI haya ni lazima yapate majibu yake sasa na sio kila siku tunasubiri,tusubiri mpaka lini,tushachoka bana,we kila siku UMEME ni tatizo,mambo ya MGAO wa umeme yalianza tangu enzi za mzee RUKSA mpaka leo tunazungumzia MGAO????hivi kweli viongozi woooote hao waliopita na waliopo sasa hawajaweza KUJIBU matatizo haya jamani????,Pamoja na wafanyakazi kulipishwa kodi mara mbilimbili,lakini bado serikali hii haijaweza kutatua matatizo haya,,,Angalia bei ya mafuta ya MALAWI,nchi ambayo inaingiza mafuta kwa kupitia bandari yetu ya hapo Dar,inauza mafuta kwa bei rahisi sana kuliko sisi,pamoja na mafuta hayo kusafirishwa masafa marefu tu toka hapo bandarini mpaka kwa mlaji wa huko malawi,tena yakisafirishwa kwa gharama kuubwa kuliko sisi tunaoyamwaga tu hapo moja kwa moja toka melini,ukweli ni kwamba nyie akina WASSIRA and ur co. MMESHINDWA na hata mpewe miaka mingine 100 hamna jipya.:angry::angry::angry: