Wassira: Dk Slaa Si Msafi!

Hebu tuangalie tena hoja za Wassira.
1. Dr. Slaa alifukuzwa upadre kwa sababu aliiba hela za kugharamia mapokezi ya baba mtakatifu
2. Dr. Slaa anaishi na mchumba wake huku akiwa na umri wa miaka sitini na ushee
3. Joshua Nassari (mgombea wa CHADEMA) ni mkorofi
4. Joshua Nassari hajaoa
5. Joshua Nassari ameonekana na bibi wa kuzungu mwenye umri wa zaidi ya miaka 60

Haya Mzee Wassira pengine ungetupa majibu kwa haya:

1. Wananchi wa Arumeru Mashariki wanaporwa ardhi kwa sababu gani? kwa sababu Dr Slaa alifukuzwa upadre? au kwa sababu Dr Slaa anaishi na mchumba wake? au kwa sababu Joshua hajaoa? Kwa nini wewe Wassira na ccm wenzako mmeuza ardhi wa watu wa Arumeru kwa 'wawekezaji' huku wananchi wakikosa sehemu ya kulima?

2. Barabara za Arumeru ni mbovu mbovu mno, kwa nini?

3. Vijana wamekosa ajira kwa nini? au ni kwa sababu Joshua ni mkorofi?
4. Kwa ujumla maisha ya wana-Arumeru yamekuwa ya shida siku hadi siku, ni kwa sababu Dr Slaa anaishi na mchumba wake?

5. Joshua ni mkorofi, je, mgombea wa ccm - Sioi Summari yeye vipi? wasifu wake ukoje? Kwa nini usiwape watu wa Arumeru wasifu wa wagombea wote wawili (Joshua na Sioi). Au pengine haumfahamu mgombea wa chama chako maana ni Mkenya?

6. Mwisho, nani msafi CCM? Mwigulu? Malima? au wewe mwenyewe Wassira- baba-mama Ndege?
 
nafahamu wengi hamtapenda lakini ndivyo dunia ilivyo ukimwaga ugali watu wanamwaga mboga lakini katika viongozi wa sasa wa vyama vyote vikuu hakuna aliyekuwa msafi tofauti ni kwamba kundi fulani liko jikoni la kundi lingine liko sebuleni waliko jikoni wananafasi kubwa ya kula msosi wanavyotaka lakini ikitokea nafasi ya kundi lililoko sebuleni kuingia jikoni tatizo litakuwa lile lile kwani nao si wasafi ebu soma hii stori ya katibu mkuu wa magwanda akiwa na umri wa miaka sitini na tisa akini bado ana mchumba:....

Kashfa ya katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema),Dk Willibrod Slaa imewekwa hadharani kwamba kiongozi huyo alifukuzwa upadri baada ya kutafuna mamilioni ya fedha zilizochangwa kwa ajili ya ujio wa hapa nchini wa Kiongozi wa Kanisa katoliki nchi duniani papa katika miaka ya tisini

Tuhuma hizo zimemwagwa na Waziri Steven Wassira katika mikutano ya kampeni za ccm kumnadi mgombea wa chama hicho sioi Solomon sumari katika Jimbo la Arumeru mashariuki

tuhuma hizo zinakuja wakati vyama hivyo viwili vikubwa nchini vikirusiana vijembe na makombora mazito mazito

kashfa hiyo imetolewa katika vijiji vya kata Kikwe katika Jimbo hilo la Arumeru Mshariki Mkoani Arusha.

Wassira alisema kwamba Dk Slaa ambaye pia aliwahi kuwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu nchini(TEC) kabla ya kukumbwa na kashfa hizo za kutafuna mamilioni hayo ya fedha zilizochangwa na waumini wa katoliki kutoka vigango na parokia mbalimbali nchini ili kufaniisha ujio wa Papa miaka ya tisini kitendo kilichopelekea kufukuzwa kazi ya upadri.

amesisitizas kwamba kiongozi huyo hana kifua cha kupambana na ufisadi kwa kuwa hata yeye alitafuna fedha za kanisa.

Aliwataka wakazi wa kata ya Kikwe kumuuliza Dk Slaa chanzo cha kufukuzwa upadri pindi atakapotia mguu ndani ya kata yao na kuwataka wakazi hao kutosikiliza sera za kiongozi huyo kwa kuwa si msafi wa kujipambanua kwamba anapambana na ufisadi nchini.

Alimtuhumu Dk Slaa Pia katika hatua nyingine anatuhumiwa kumfukuza kazi mhasibu wa chama hicho ngazi ya taifa kwa kosa la kukataa kutekeleza maagizo yake amlipe shilingi milioni 10 mchumba wake,Josephine Mushumbushi kitendo kinachotia mashaka ya uadilifu wa kiongozi huyo.

Hata hivyo,alishangaa kitendo cha Dk Slaa kuishi maisha ya uchumba wakati akiwa na umri wa miaka zaidi ya 60 na kudai kitendo hicho kinashangaza umma wa watanzania pamoja na wafuasi wa vyama vya siasa nchini.

Wakati huo huo,Wassira ambaye pia ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM alisema kwamba mgombea ubunge wa Chadema,Joshua Nassari hafai kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa kuwa ni kijana mkorofi na mara kwa mara baba yake mzazi amekuwa akimsihi kuachana na ukorofi tangu wakati akiwa chuo kikuu cha Dar es salaam.

Alisema kwamba baba wa mgombea huyo ambaye ni kiongozi wa dini amekuwa akimsihi kuachana na ukorofi ikiwa ni pamoja na kuoa ili aweze kutulia lakini cha ajabu Nassari amekuwa akionekana na bibi wa kizungu mwenye umri wa zaidi ya miaka 60 akizunguka naye mitaani.

Wassira amewataka wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanatunza shada zao ili kuepuka kuporwa na wafuasi wa chadema

Amesema tayari chama cha chadema kimeanza mchezo mchafu kwa kusambaza waraka pamoja na vijana kwa ajili ya kununua shahada


Wao Ndiyo wana serikali na Tuhuma za Wizi haijalishi mtu kaiba wapi anatakiwa kupelekwa mahakamani.... Mbona Kimya na wanaongea hadharani..

Kwa nini wasimpeleke Mahakamani.. Hivi ndiyo ile kauli kwamba CCM Nchi imewashinda nini au Dr Slaa wanamwogopa sana kwa 2015 na hata hizi chaguzi ndogo.

Nasikia alikuwa anasinzia kwenye mkutano wa Kampeni, Hivi Huyu naya anatumia yale mambo ya vijana vijiweni nini?
 
A failure! Slaa isn't a candiate in Meru ndugu Wasira. Slaa didn't grab Land there. Slaa didn't bring joblessness.
CCM is damned tired! Kajilalie tu mzee
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hakuna ukomo wa umri ktk uchumba!!
Kuhusu kumfukuza mhasibu wa chama, nadhani kila mtu anajua kwamba CDM ni chama hivo kina viongozi (si dr. Slaa pekee) ambao wanaongoza chama, hivo si suala la Dr. Slaa kukurupuka tu(dr. Slaa hamiliki cdm)!! Tusisahau mhasibu (kwa anaejua maana) wa chama ni mtu mzito sana ktk chama si wa Dr. Slaa kuamka na kumfukuza kazi lazima kuna taratibu za kufuatwa (kama kweli amefukuzwa)!!
Suala la dini si jepesi kama wanasiasa wanavotuaminisha, kanisa katoriki lina taratibu zake, kama lingekuwa lilimfukuza kila mmoja asingesubiri kuambiwa na wanasiasa!!
Jamani ma-GT wa Jf mnatakiwa kutumia zaidi ubongo ktk kutafakari mambo, tuache ushabiki, uzandiki, majungu na chuki binafsi badala yake tujikite ktk taifa letu linalozama, tutumie mda wetu na taaluma zetu kwa manufaa ya taifa!!

I 'LL BE BACK.
 
A failure! Slaa isn't a candiate in Meru ndugu Wasira. Slaa didn't grab Land there. Slaa didn't bring joblessness.
CCM is damned tired! Kajilalie tu mzee

Bosi wake aliyestaafu anasema HANA ADABU NA NIMPUMBAVU.

Ndo sera zao izo
 
Hebu tuangalie tena hoja za Wassira.
1. Dr. Slaa alifukuzwa upadre kwa sababu aliiba hela za kugharamia mapokezi ya baba mtakatifu
2. Dr. Slaa anaishi na mchumba wake huku akiwa na umri wa miaka sitini na ushee
3. Joshua Nassari (mgombea wa CHADEMA) ni mkorofi
4. Joshua Nassari hajaoa
5. Joshua Nassari ameonekana na bibi wa kuzungu mwenye umri wa zaidi ya miaka 60

Haya Mzee Wassira pengine ungetupa majibu kwa haya:

1. Wananchi wa Arumeru Mashariki wanaporwa ardhi kwa sababu gani? kwa sababu Dr Slaa alifukuzwa upadre? au kwa sababu Dr Slaa anaishi na mchumba wake? au kwa sababu Joshua hajaoa? Kwa nini wewe Wassira na ccm wenzako mmeuza ardhi wa watu wa Arumeru kwa 'wawekezaji' huku wananchi wakikosa sehemu ya kulima?

2. Barabara za Arumeru ni mbovu mbovu mno, kwa nini?

3. Vijana wamekosa ajira kwa nini? au ni kwa sababu Joshua ni mkorofi?
4. Kwa ujumla maisha ya wana-Arumeru yamekuwa ya shida siku hadi siku, ni kwa sababu Dr Slaa anaishi na mchumba wake?

5. Joshua ni mkorofi, je, mgombea wa ccm - Sioi Summari yeye vipi? wasifu wake ukoje? Kwa nini usiwape watu wa Arumeru wasifu wa wagombea wote wawili (Joshua na Sioi). Au pengine haumfahamu mgombea wa chama chako maana ni Mkenya?

6. Mwisho, nani msafi CCM? Mwigulu? Malima? au wewe mwenyewe Wassira- baba-mama Ndege?

Kaka naona umeamua kuanzisha tamthilia yako unaandika mwenyewe halafu unajijibu mwenyewe!
 
Mkapa amekiri kuwa alipofungua kampeni za uchaguzi huko Arumeru alisema uwongo kwa kuongelea masuala ya familia ya Nyerere ambayo hayakuwa na ukweli.
CCM ni mabingwa wa kutunga kashfa za uongo ili kufanikisha malengo na wakishafanikiwa wanawatelekeza watumiwa kufanikisha malengo yao. Akina Masumbuko Lamwai, Walid Kaburu na wengine wamebaki kwenye kumbukumbu ya historia tu kwa kufanikisha malengo ya CCM kusambaratisha nguvu za upinzani kisha kusahaulika, wao wanazidi kujaza matumbo kama akina Wasira, Komba, Mkapa nk wakiwa ni vitufe maumbile yao kutokana na ulaji usio na kiwango cha kiafya.

Kanisa siku nyingi lilisha kanusha kuhusiana na uongo wa mzee mzima Wasira asiye na haya kutamka yasiyo kwali, na kesho sijui ataonekana vipi kanisani kutokana na wongo anaopaka matope kanisa.
Taasisi ya Kanisa katoliki lina taratibu na sheria ambazo mwenye wito wa upadre au utawa siku akijiona hajisikii wito wa huduma hiyo kwa kanisa anaomba ridhaa ya Kiti cha Kitume Rome kimfungue kuacha utumishi huo ili kuishi maisha ya kawaida ya kilei. Wapo wengi walifanya hivyo. Na wapo watumishi wengi ambao wamesoma seminari lakini walipomaliza waliomba kutoendelea na masomo ya upadre ili waishi maisha ya kawaida. Je hao wote waliiba pesa kanisani au walichukua wake au walifukuzwa?

Slaa amekuwa na huyo mama kwa uwazi bila kificho na kutangaza hadharani, huu ndio ustaarabu na usomi, lakini hawa viongozi wa CCM wamajaza vimada kila kona na kuwatelekeza wake zao. Slaa hajaoa, na liyekuwa naye kwanza alikuwa gf wake, alikuwa mpenzi wake ambaye wamezaa, na katika kampeni mwakajuzi ndipo alipotangaza kwamba ana mchumba, na hatujasikia malalamiko toka kwa mpenzi wake wa zamani, maana yake walikubaliana na tofauti zao na wakayamaliza, sasa CCM kinawauma nini? na hawa CCM wanaowatelekeza wake zao kuishi na vimada hasa wawapo Dodoma. Hakuna kiongozi wa CCM aliyewahi kutangza hadharani vimada wao, na wengi wanaotafuta kazi maofisini wasichana inabidi wajirahizishe ili kupata ajira ndio rushwa ilivyokithiri ndani ya CCM.

Kanisa Katoliki lina utaratibu wa utunzaji wa fedha, padre jukumu lake ni usimamizi na kuna walei ndio watunza fedha, wanachojaribu hapa CCM ni kutafuta kila njia kumchafua Slaa anayewanyima usingizi kila kukicha.

CCM kadiri ya kumbukumbu zangu wasingeweza kumweka Kinana kuwa kiongozi wa kusimamia uchaguzi last time kutokana na kashfa kubwa ambayo aliipata na kufukuzwa uwazili katika awamu kama sijakosea ya Mwinyi, Kashfa kutoka Wizara ya Ujenzi ambayo alikuwa waziri alivyoiba pesa nyingi za kujengea barabara nchini, waliishia kumfukuza uwaziri tu, na leo anatanua na kubakia kula fedha za chama kwa vile hawezi kurudi serikalini kutokana na kashfa zilizomtokea.

Kanisa lilishatoa ufafanuzi na kukanusha uwongo huo wa CCM ni sawa na uwongo wa kuwapambikiza tuhuma maaskofu katoliki kule kwenye sherehe za kumsimika Askofu wa Mbinga kwamba wanauza madawa ya kulevya, hiyo ndiyo sera ya CCM siku zote.

Wasira ni popo, amehangaika mara ahamie NCCR Mageuzi, na mambo yalipomshinda huyo karudi tena CCM, alikuwa anatafuta nini kama si ubinafsi wa kutaka madaraka? Kazeeka vibaya na uzee ule wa kulala bungeni kila kukicha bora tu apumzike awaachie vijana vinginevyo tutamwumbua vingi tunavyojua hadi kwama kwenye thread moja walivyomjadili alivyoiba mke wa mtu kama alivyofanya Pius Msekwa na kuishia kumlundikia tuhuma hayati Askofuwa wa Mwanza Butibubage.
 
Hizi ni dalili za kuishiwa sera, aongee hoja na sio kufanya personal attacks zisijo na tija!
 
Haya si maneno yangu( Wasila kushindwa kulala usiku kwa kukoseshwa usingizi na Dr Slaa au kupigwa Rigwaride na vibinti vichanga huku mkewe wa ndoa kampa makalio) yaliandikwa siku nyingi enzi za kikombe chaa babu




PICHA ZOTE HIZI ZIMEPIGWA KATIKA KIKAO CHA BUNGE KINACHOENDELEA HUKO DODOMA.HIVI WAZIRI MZEMBE KAMA HUYU ANAYEDIRIKI KULALA OVYO OVYO HADHARANI (BUNGENI) AKIWA OFISINI KWAKE SI NDIO ANAJIFUNIKA NA SHUKA KABISA.JE CHANZO CHA KULALA LALA OVYO KAMA TEJA NI UCHOVU NYAKATI ZA USIKU (ATUELEZE ANAKESHA AKIFANYA NINI),MARADHI KAMA SLEEPING SICKNESS AU "TEJA"?
 
nafahamu wengi hamtapenda lakini ndivyo dunia ilivyo ukimwaga ugali watu wanamwaga mboga lakini katika viongozi wa sasa wa vyama vyote vikuu hakuna aliyekuwa msafi tofauti ni kwamba kundi fulani liko jikoni la kundi lingine liko sebuleni waliko jikoni wananafasi kubwa ya kula msosi wanavyotaka lakini ikitokea nafasi ya kundi lililoko sebuleni kuingia jikoni tatizo litakuwa lile lile kwani nao si wasafi ebu soma hii stori ya katibu mkuu wa magwanda akiwa na umri wa miaka sitini na tisa akini bado ana mchumba:....

Kashfa ya katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema),Dk Willibrod Slaa imewekwa hadharani kwamba kiongozi huyo alifukuzwa upadri baada ya kutafuna mamilioni ya fedha zilizochangwa kwa ajili ya ujio wa hapa nchini wa Kiongozi wa Kanisa katoliki nchi duniani papa katika miaka ya tisini

Tuhuma hizo zimemwagwa na Waziri Steven Wassira katika mikutano ya kampeni za ccm kumnadi mgombea wa chama hicho sioi Solomon sumari katika Jimbo la Arumeru mashariuki

tuhuma hizo zinakuja wakati vyama hivyo viwili vikubwa nchini vikirusiana vijembe na makombora mazito mazito

kashfa hiyo imetolewa katika vijiji vya kata Kikwe katika Jimbo hilo la Arumeru Mshariki Mkoani Arusha.

Wassira alisema kwamba Dk Slaa ambaye pia aliwahi kuwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu nchini(TEC) kabla ya kukumbwa na kashfa hizo za kutafuna mamilioni hayo ya fedha zilizochangwa na waumini wa katoliki kutoka vigango na parokia mbalimbali nchini ili kufaniisha ujio wa Papa miaka ya tisini kitendo kilichopelekea kufukuzwa kazi ya upadri.

amesisitizas kwamba kiongozi huyo hana kifua cha kupambana na ufisadi kwa kuwa hata yeye alitafuna fedha za kanisa.

Aliwataka wakazi wa kata ya Kikwe kumuuliza Dk Slaa chanzo cha kufukuzwa upadri pindi atakapotia mguu ndani ya kata yao na kuwataka wakazi hao kutosikiliza sera za kiongozi huyo kwa kuwa si msafi wa kujipambanua kwamba anapambana na ufisadi nchini.

Alimtuhumu Dk Slaa Pia katika hatua nyingine anatuhumiwa kumfukuza kazi mhasibu wa chama hicho ngazi ya taifa kwa kosa la kukataa kutekeleza maagizo yake amlipe shilingi milioni 10 mchumba wake,Josephine Mushumbushi kitendo kinachotia mashaka ya uadilifu wa kiongozi huyo.

Hata hivyo,alishangaa kitendo cha Dk Slaa kuishi maisha ya uchumba wakati akiwa na umri wa miaka zaidi ya 60 na kudai kitendo hicho kinashangaza umma wa watanzania pamoja na wafuasi wa vyama vya siasa nchini.

Wakati huo huo,Wassira ambaye pia ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM alisema kwamba mgombea ubunge wa Chadema,Joshua Nassari hafai kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa kuwa ni kijana mkorofi na mara kwa mara baba yake mzazi amekuwa akimsihi kuachana na ukorofi tangu wakati akiwa chuo kikuu cha Dar es salaam.

Alisema kwamba baba wa mgombea huyo ambaye ni kiongozi wa dini amekuwa akimsihi kuachana na ukorofi ikiwa ni pamoja na kuoa ili aweze kutulia lakini cha ajabu Nassari amekuwa akionekana na bibi wa kizungu mwenye umri wa zaidi ya miaka 60 akizunguka naye mitaani.

Wassira amewataka wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanatunza shada zao ili kuepuka kuporwa na wafuasi wa chadema

Amesema tayari chama cha chadema kimeanza mchezo mchafu kwa kusambaza waraka pamoja na vijana kwa ajili ya kununua shahada

Slaa sio msafi compared to who?

 
Jamaa hoi haijwezi bungeni.

hdJWK65WRzPeQAAAABJRU5ErkJggg==
 
if this was his statement for sure, now i see why Mr kikwete government and his CCM is collapsing. Mtu kama wasira kwa position yake ndo ana kampeni hivi,
 
Huyu Jamaa alitumwa na wabunge wenzie wa CCM kwenda katika NEC yao ili apinge kuondolewa kwa wabunge katika kugombea nafasi za uongozi katika chama, cha-ajabu agenda (agendum) hiyo ilipitishwa huko yeye akiwa amesinzia. Anastuka na kuuliza kinana, mkuu ili hoja yakuwaondoa wabunge katika uongozi wa chama mbona sijaiskia....? haha imeshapitishwa mkuu....pole..alisema Kinana huku akicheka....Huyo ndo wasira bwana.
 
kwani ufisadi wa CCM unawanyima usingizi CHADEMA? cha msingi jibu hoja ili kama Dr. ambaye nami nampenda na kumkubali kama kiongozi mwadilifu tujue madhaifu yake na kama vipi ashauriwe vizuri ili asichafue tulipofikia

wasira ameenda kumnadi mgombea wa ccm sioi, lakini hakuna sehemu alipo mtaja sioi. je anamchafua slaa ndo anayegombea? mbona hakufanya hivyo 2010? watanzania wa sasa hawadanganyiki. ccm imekula kwao.
 
Kwasababu Wassira ni nyani mwenye umbile la sokwe kamwe hawezi kuona kundure lake. Mbona yeye kapora mke wa mtu? Kwa mila na desturi za wakurya mama Ndege bado ni mke wa mtu.
 
Back
Top Bottom