Wassira: CHADEMA kufa ni Ngumu

Wassira: CHADEMA kufa ni Ngumu

Hatimaye waziri wa Jk bwana Stephen Wasira kakili kuwa CHADEMA haiwezi kufa kirahisi na CCM wasibweteke na kudhani kitakufa kama walivyopanga huko nyuma na kuwaomba waangalie njia mbadala ikiwemo kumshawishi msajili wa vyama vya siasa kukifuta.

Source Gazeti Jamuhuri
Huu ni uzushi mkubwa, Taarifa yenye uhakika WASIRA yuko jimboni mwake Bunda ziara ya kutembelea wapiga kura wake.
Unaweza kuthibitisha hayo kayasemea wapi mbona Jamhuri halina Taarifa hiyo?
 
Chama gani hiki cha msimu.Si upepo tu utapita hakina uwezo wa kukitikisa CCM.Watanzania msihangaike na photocopy wakati original ipo.Maneno ya mnyampala tarehe 10.10.2010 Uwanja wa CCM wa majimaji Songea.
 
We wasira NCCR ilikulea, unaweza ukajikuta CDM siku moja.

Kwani hamjui kwamba Wasira alienda NCCR Mageuzi baada ya kutoka Chadema? Yeye ni mmoja wa waanzilishi wa Chadema, na hizi kelele zake zote ni wivu wa kuona wenzake wanapata mafanikio wakati yeye anafakamia matapishi yake. Ni mtu wa ajabu sana! Haiwezekani mtu aliyeshindwa kuwa baba bora wa familia yake(mke na watoto) akawa kiongozi bora kwa nchi! Watoto wake na ndugu zake ni wanachadema, hili pekee linamtesa sana! Na bado ataweweseka sana.
 
nitajitolea kuizika itakapokufa rasmi juni 20.2014

Mlianza kusema itakufa 2013,tehe tehe.Imeshindikana sasa ni 20 juni 2014,tehe tehe.UTANGOJA MILELE NA UTAKUFA BILA KELELE,KAMA WALIVYO KUFA WAFUASI WA KIBWETELE,tehe tehe,peopleeeeeesssss,................
 
Hivi huyu mzee kwa umri wake kwa nini hatulii na kutumia busara kama wazee wengine?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Bora angekuwa na Busara za Marehemu Phares Kabuye....

Wabunge kumbukeni, fuateni nyayo za marehemu Kabuye
BY MASHAKA MGETA
29th June 2011
…….
Akasema mkoani Kagera kuna hadithi inayomzungumzia nyani aliyeketi juu ya mwamba mkubwa. Akiwa kwenye mwamba huo, nyani huyo alitoa ushuzi.
Baada ya kitendo hicho, mwamba ule, kutokana na ukubwa wake, ulimwambia nyani ‘ushuzi wako hauwezi kunitikisa’ na kweli mwamba haukutikisika.
Lakini nyani akitambua ukweli huo akajibu; ‘japokuwa siwezi kukutikisa, lakini harufu yake umeipata.’
Wabunge walicheka sana. Hata waandishi wa habari na watu wengine waliohudhuria kikao kile walishindwa kujizuia, wakacheka sana.
Wengine hawakujua kusudio la Kabuye. Ingawa watafsiri wa misemo ya asili waliweka bayana kwamba ukubwa na nguvu za mtoa hoja haviwezi kuukwepa ukweli. Kwa maana ukweli unabaki kuwa ukweli daima, hata kama utatofautiana na matakwa ya baadhi ya watu.
……...
Itakumbukumbwa kwamba hata lilipoibuka suala la kufutwa posho zisizokuwa na tija kwa watumishi wa umma wakiwemo wabunge, watawala na wenye nguvu mithili ya mwamba waliwabeza, waliwadharau na kuwakejeli watoa hoja.
…….
Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ni miongoni mwa waliokaririwa wakisema posho ni sehemu ya vyanzo vinavyowapa wanasiasa fedha nyingi kuliko hata wanataaluma na wataalamu wa fani tofauti nchini!
………...
Kwa ambao hawakuwa bungeni wakati wa Kabuye, wanaweza kupitia kitengo cha taarifa za Bunge, wazisome na kuzisikiliza hoja zake, ili wajiepushe na kujiweka kando kabisa mwa kasumba ya ‘ninaunga mkono hoja kwa asilimia 100 pasipo tija’.


[h=2]Asiyekuwa na dhambi na awe wa kwanza…31/07/2007[/h][TABLE="width: 499"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
MBUNGE wa Biharamulo Magharibi, Phares Kabuye (TLP), jana aliwashtua wabunge na kuamsha hisia zao pale alipoinuka na kudai kuwa wabunge wote walipata ushindi baada ya kutumia rushwa. Akichangia katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria, Kabuye alisema kuwa hakuna mbunge safi ndani ya Bunge hilo isipokuwa yeye na Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

akini baada ya kauli hiyo, Kabuye alianza kuzungumzia rushwa na kusema: “Rushwa katika siasa. Zamani kuku walikuwa hawajisaidii sehemu wanayolala, lakini akatokea jogoo akajisaidia mahali wanapolala, na kuku wengine wakiwamo vifaranga wakaona kumbe tulikuwa tunahangaika… tunaweza kujisaidia hapa hapa. Wakaanza kujisaidia.”
“Sasa wewe jogoo mwanasiasa unapotoa rushwa unakuwa umejisaidia sehemu tunayolala… humu ndani kama tunachunguza na kuwaondoa wabunge… sidhani kama angebaki mbunge… wabunge walioingia humu wameingia kwa rushwa… hatabaki mtu kasoro mimi… pengine na waziri mkuu na rais,” alisema, hali iliyodhihirika kuwaudhi wabunge wenzake.
“Mnasema mnamuenzi (Mwalimu Julius) Nyerere, halafu mnatumia rushwa… nasema akifufuka humu ndani mtamkimbia wote,” alisisitiza.
Mara baada ya kauli hiyo, Mbunge wa Karagwe, Gosbert Blandes (CCM) alisimama na kutaka mwongozo wa Spika, kuhusu alichotamka Kabuye.
Baada ya hapo, Kabuye alisema: “Hilo nililitegemea. Ninao ushahidi wa watu wa Biharamulo, ninaweza kuwaleta wakathibitisha kuwa sijatoa hata pipi.” Hata hivyo, wakati mbunge huyo akizungumza, wabunge wenzake walisikika wakitamka bila kutumia vipaza sauti wakimtaka afute usemi na aombe radhi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Uratibu), Dk. Batilda Burian naye alilazimika kusimama, kumdhibiti mbunge huyo kwa kutumia kanuni.
Dk. Burian alisema alikuwa amemvumilia kwa muda mrefu Kabuye wakati akizungumza kwa sababu amekuwa akitumia lugha ya kuudhi. Baada ya hapo, Kabuye alisimama na kusema: “Kwa kulazimishwa, naomba kufuta usemi.” Hali hiyo haikuishia hapo, Job Ndugai, Mwenyekiti wa kikao cha jana, alisimama na kumtaka mbunge huyo kuzungumza lugha inayowiana na mazingira ya Bunge, akisisitiza kwa kusema huenda Kabuye aliamka vibaya.
“Mheshimiwa mwenyekiti, si kwamba leo nimeamka vibaya, bali nina uchungu… hata mtu anapofiwa hajui machozi yanatoka wapi… kuna wakati tutafukuzana humu bungeni kwa kusema kwa uchungu,” alisema.
 
Ama kweli nimekubali kuwa huyu mzee kazeeka.Lakini kumbukeni kuwa Wasira alikuwa mpinzani wa ccm sana ghafla akajipenyeza hadi akaingia tena ccm hivyo ni mtu anaejua kusoma upepo. Hivyo wana CHADEMA tuweni macho na watu wa aina hii.
 
CDM haitakufa milele na milele yote, ndilo tumaini pekee la wanyonge lililobakia!! Mtakufa nyie wazee wenye sura zilizofanana na roho zenu!! Hata mkiuwa viongozi wake wote,,,,bado sera za CDM zipo palepale!!!
 
Umeona eeh?
Yaani mzee mwanzilishi wa Chadema anataka Chadema ife (mwaka jana), baada ya mbinu za kuiua kufeli (mwaka huu)then ana suggest Tendwa aifute (mwakani?), then anasema haitakufa! Haeleweki. Wassira ni janga

Mkuu ni jambo la ajabu, sijui ukomavu wa siasa uko wap ukizingatia umri wake kwenye siasa, pia uanzishwaji wa vyama vingi ni miaka 20 sasa ila bado tu hajaweza ku change na mabadiliko ya kisiasa!

unaweza kudhani kawekewa maneno mdomon! Atoke akanushe mapema hii maneno, hebu fikiria msajil akaifuta CDM si itaonekana dhahiri ni njama za serikal? Watazuia vip reaction za wananchi?

kuropoka ovyo bila tafakari pana ni kubaya sana..au mwandish alimkurupusha usingizin ndio akatoa hayo maneno? Au labda kwenye vikao vya bar! Still ni ngumu kuamin alichosema!
 
Ama kweli nimekubali kuwa huyu mzee kazeeka.Lakini kumbukeni kuwa Wasira alikuwa mpinzani wa ccm sana ghafla akajipenyeza hadi akaingia tena ccm hivyo ni mtu anaejua kusoma upepo. Hivyo wana CHADEMA tuweni macho na watu wa aina hii.
Kalewa Madaraka huyu, hana lolote, na anaogopa CDM Kikiingia Ikulu atakosa ujasiriatumbo kama alivyozoea!
 
Hatimaye waziri wa Jk bwana Stephen Wasira kakili kuwa CHADEMA haiwezi kufa kirahisi na CCM wasibweteke na kudhani kitakufa kama walivyopanga huko nyuma na kuwaomba waangalie njia mbadala ikiwemo kumshawishi msajili wa vyama vya siasa kukifuta.

Source Gazeti Jamuhuri

If you can't fight then you join...
 
Hivi wasira kaamshwa? mi namkumbuka akiwa bungeni amelala usingizi!
wasira%2Bchapa%2Busingizi.jpg
 
Huyu mzee ndio chanzo cha wazungu kusema waafrica wametokana na sokwe.
 
Sema hujamuelewa Wasira Mkuu, amemaanisha kuwa chadema kina wenyewe na hao hata wapewe utajiri nusu ya nchi na Ccm au mito ya asali na maziwa iwekwe nchi nzima hawatokubali kukiacha cdm. Mi nawashangaa watu kama nyinyi wa kanda ya kati mnajihangaisha na cdm, hiki chama kimewamezesha watu sumu mbaya sana na kuitema ni ngumu.

Naona mnaanza kukiri kwa vinywa vyenu kwamba hata Kanda ya Kati, Chadema inakubalika. Ni bado wewe pekee maana huenda mkeo ni Chadema kwa siri. Wanao ndo usiseme kabisa!!
 
Wameanza kukana kauli zao,bado Jk kauli yake ya kwamba vyama vya upinzani ni vya msimu,sijui ana haha nini!?

JK alikuwa sahihi wakati akitoa statement hiyo kwani alidhani CDM ni wale Maliberali, wanaoolewa hovyo hovyo na sisi magamba. JK aliona toka mapema kuwa CDM sio mashoga, hivyo kila plan yake inatibuka tu. Mwisho misimu yote inaisha sasa na CDM ndo inazidi kuwa imara...
 
Back
Top Bottom