Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
Nionavyo mimi badala ya kumzonga Sitta, ilipaswa tu mumtake awataje hao mafisadi. Kumtaka akae kimya ili mijizi iendelee kutuibia sidhani kama ndio sera ya CCM. Siamini pia kama ni sifa ya kiongozi bora kufumbia macho uoza wa serikali yake ili kulinda nafasi yake katika chama au serikali.Wassira amemwambia Sitta "kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."
Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".
Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"
My take;
Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu hayo.
Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania, kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
Inawezekana akawa haridhishwi na mwenendo wa serikali yake ingawa naye ni part ya serikali, hii sio ajabu. Nionavyo mimi Wassira ndo anaropoka, haiwezekani kiongozi wa serikali inayoiita tufuku, akiri hadharani kuwa serikali yake ina uongozi uliooza afu ategemea wananchi wawe na imani na serikali ya CCM.
Anachokisema Wassira ni kuwa serikali ya CCM haina viongozi wazalendo au waadilifui, kusema samaki mmoja akioza ni wote hii ni kauli ya kipuuzi kabisa. Kama Wassira yeye ana busara, atutajie basi ni samaki gani huyo aliyeoza na anayeozesha wengine ili tumtoe mapema asiozeshe wengine. Kuendelea kukaa kamya ilhali anajua samaki flan kaoza ni utapeli wa kisiasa pia.
Kwako Mtoa mada, unasema nyinyi CCM hamna tabia ya kuropoka, hivi kusema ukweli juu ya mwenendo wa serikali yako ni kuropoka??? Mnakaa kimya na kuunyamazia uoza huu unaoendelezwa na serikali yenu kwa manufaa ya nani??? Nina wasiwasi kuwa siasa ya Tanzania imeanza kutumia wanasiasa wendawazimu.
Hii nchi ni ya Watanzania, maslahi yaelekezwe kwa Tanzania kwanza na sio chama kiwekwe mbele kuliko maslah ya Tanzania. Kama hali ndo hii ya kuweka chama mbele kuliko Tanzania, basi nchi yetu inatawaliwa na genge la wahuni.