Wassira amtaka Sitta "kujiuzuru".

KYAMTUNDU, hayo uyasemayo ni kweli na nukuu yako ni sahihi, lakini tatizo linakuja kwenye kuipenda CHADEMA, kama kweli kingekuwa mbadala wa ccm, basi muda mrefu tu ningekuwa mkereketwa wake. Tatizo lilipo ni kwamba Chadema wameonyesha mapungufu mengi wakiwa nje ya dola, sasa tukiwapa dola itakuwaje?

Sasa tumeelewana ndugu yangu!Sasa tuwape dola tuone kama watafanya usanii,tuwapige chini!Kitu ambacho watanzania wanapaswa kufahamu ni kutokuwa na urafiki na watawala!Hata kama ni CHADEMA, wakiingia madaraka wanaweza kuwepo watu waliokosa fursa wakataka kujinufaisha mapema..
Tutawapima CHADEMA kwa jinsi watakavyokuwa tayari kuwashughulikia watu wa jinsi hiyo!
Tatizo la CCM ni kulindana! Mimi siseme CHADEMA ina malaika, ILA naamini wakiwekewa presha watakuwa tayari kutii!CCM hawaofii kupoteza madaraka ndo maana kwao liwalo na liwe,maana wamejenga urafiki wa kinafiki na watawaliwa kwa kutumia elimu hafifu na umaskini wetu! Mwisho, huwa sielewi nnaposikia mtu anasema CHADEMA si mbadala wa CCM na wakati huo huo hasemi mbadala ni chama kipi! Kutosema maanake tuendelee na CCM! Chama Kimoja kushika madaraka kwa muda mrefu ni sawa na nchi kuwa na chama kimoja! Tuwape likizo CCM ili wajifunze kwamba wananchi ndo msingi wa utawala...Hata wakirudi madarakani (jambo ambalo ni afya ya demokrasia), watakuwa wamejifunza mambo mengi!
Kuanzia leo utakuwa rafiki yangu! Tehe!
 
Mkuu Kite Munganga, umeleta hoja nzuri sana, nadhani hii itadhihirisha ukigeu geu wa huyu mzee Sitta. Kila siku, mimi ni miongoni mwa wana CCM tunao pinga maslahi ya wabunge kuwa yalivyo sasa.

Ni mzigo mzito kwa taifa, ndio maana huwa namkubali Zitto kwenye hili la kukataa posho za viti, ni ufujaji mkubwa sana wa fedha za umma.

Lakini pia sababu za wabunge kung'ang'ania kuongezwa posho sio reasonable kabisa, mara watakwambia gharama za maisha Dodoma ni kubwa, mara wamegeuzwa ATM na wapiga kura wao, sasa kweli hizi nazo sababu?

Sitta kwenye hili aliniudhi kwa kweli.

Huko Kenya mawakili wameenda mahakamani kupinga kula walizojipigia wabunge wao wanaopendakula kama Nguruwe,

Sijui sisi tufanyeje na huyo Mr Six ambaye sasa anajifanya ana huruma na watanzania wakati kumbe anatoa machozi ya mamba?
 
SIASA ZA Mh 6 SIJUIKAMA ATALAMBA DUME! Mara CCJ! Mara atajejiunga Chadema! Mara anaikosoa Serikali aliomo! Mara atangaza Marafiki zake ambapo mda ukifika watajadiliana nani agombe Urais! Daah! "NAMSHAURI ASTAAFU SIASA"

Hajielewielewi. Huku anataka na kule anataka. Aibu kwa mtu mzima
 
Wassira amemwambia Sitta "kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."

Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".

Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"

My take;

Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu hayo.

Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania, kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
Hapa ninamuunga mkona WAHASIRA!! Six ni mnafiki mkubwa!! Mpashe huyo anayezeeka vibaya!!
 
Wassira amemwambia Sitta "kama unaona serikali inaendeshwa kwa rushwa jiuzuru", akaendelea kusisitiza, "huwezi kuwa kwenye serikali hiyo hiyo bado unaisema ni serikali ya kifisadi wakati na wewe ni sehemu ya serikali."

Wassira pia aliongeza yafuatayo, "huwezi kuisema serikali vibaya wakati na wewe ni sehemu ya serikali hiyo, vinginevyo ndugu Sitta aachie ngazi la sivyo huu utakuwa utapeli wa kisiasa".

Aidha, katika kuimalizia hoja yake hii aliuliza swali, "samaki mmoja akioza, wote wanaoza, sasa yeye (akimaanisha Sitta) atasalimika vipi?"

My take;

Mhe. Sitta nadhani ana hitaji kukopeshwa busara kidogo, katika hatua hii huwezi kujifanya una chukizwa na madudu ya serikali ambayo kwa kipindi chote hiki amekuwa akiitumikia, amekuwa sehemu ya serikali hiyo na kama akisema kuna madudu, na yeye tuseme ni miongoni mwa wazalisha madudu hayo.

Mhe. Sitta, kiu ya urais isikufanye uonekane kituko mbele ya watanzania, kuwa mpole na usubiri wakati muafaka, kwani tabia hizi za kuropoka ropoka ndani ya CCM hatunazo, tuwaachie hii tabia wasaka dola bila mbinu (CHADEMA).
Nimeipenda hii: CHADEMA NI WASAKA DOLA BILA MBINU. IMEKAA VIZURI NA IMEPENDEZA.
 
Nyie mnaangaika na wassira na sitta, ya kwenu yamewashinda mmekosa hoja sas ni umbea tu! na membe nae ni RAIS?:hatari:
 
Back
Top Bottom