Wana jamvi
Kutokana na matamko ya Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako haswa katika sekta ya elimu kama vile "moja la sifa za kujiunga chuo kikuu lazima uwe na form six pass" na sio equivalent, kwa maana umesoma foundation course ya Open university, certificate ukachukua Diploma halafu unaenda chuo kikuu, hili lina lengo baya sana katika kuthibiti idadi ya wanafunzi kwenda vyuo vikuu, aidha kupandisha GPA sasa mi naomba kama kweli alikuwa na sifa zote hizo mpaka akafika hapo mwenye cv yake aiweke tuijadili kwa manufaa ya elimu yetu, ina maana sasa ukiishia form form maana yake ndoto ya degree futa , au ukiwa na diploma futa ndoto za degree sasa sijui tunatengeneza kitu gani hakyamungu, na hivi ni kweli watu wote hawakupitia hatua hizo? kwa maana wote walipita form six wakapata degree?? masikini Tanzania yetu daaaah