Wasifu(CV) ya Jenerali Ulimwengu

Wasifu(CV) ya Jenerali Ulimwengu

Nadhani sasa unaleta Siasa bila sababu. Twaha Khalifani alizaliwa Rwanda na alikuja Tanganyika kama migrant akiwa na baba yake wakati huo akiwa na umri wa miaka 5. Tusipende kupotosha, Serikali ya Mkapa ilim-pin down kwa kuwa kisheria Twaha Khalifani ni munyarwanda, ila ku-quaify uraia wa Tanzania alitakiwa kuwa amekana uraia wa Rwanda, jambo ambalo hadi 2001 wakati wa kunyang'anywa uraia hakuwa ametimiza takwa hilo la kisheria. Stories nyingine ni blah blah tu. Baba yake Twaha alizikwa Kamachumu. Dadake pekee wa Twaha anayeitwa Zainabu ni mjane wa Peter Claver Bakilana (1939-2012) [rip] aliyewahi kuwa CEO wa THA (sasa TPA), TRC (sasa TRL) na NTC. Twaha huwa haendi kwao kamachumu kwa sababu shamba la babake aliliuza.
Kwahiyo ile tu kusema "...alikuja Tanzania as a migrant wakati akiwa na miaka 5...!" ndo tayari unaona ulichoongea ni sahihi na kwamba sio wewe ndie uliepotosha?! Akija mwingine akisema alikuja akiwa na miaka 10 utambishia?! Na utambishia kwa kutumia vigezo gani na vigezo gani utamtaka mtu akukubalie wewe uliyesema alikuja akiwa na miaka 5?!

Maandiko mbalimbali yanaonesha Jenerali Ulimwengu alizaliwa Ngara mwaka 1948. Pambazuka, hawa hapa:
JENERALI ULIMWENGU was born on 4th April 1948 in Ngara, Kagera Region of Tanzania. He went to school in Kamachumu, Katoke and Nyakato in Kagera and high school in Tabora from 1955 to 1968 and was a student of the then University of East Africa from 1969 to 1972.
Mtandao wa Suffrage-Universel unaripoti:
According to the lecturers' memorandum, distributed to different organisations and media houses, Mr Ulimwengu was born in Ngara district on April 4, 1948, and went to school in Kamachumu, Katoke and Nyakato in Kagera region.
Mimi nimetoa reference 2; nakuomba wewe utoe reference MOJA TU hata kama credibility yake inatia shaka... source inayosema Ulimwengu aliingia Tanzania akiwa na miaka 5!!!!

Remember, kwenye post za siku za nyuma ulisema ulimfahamu Ulimwengu Nyakato wakati akiwa sekondari!
For those of us who know him well right from Nyakato Secondary School to the University of Dar es Salaam, Ulimwengu is nothing but an accomplished exhibitionist opportunist whom no normal-minded person can trust - so his opium-orchestrated opinion.
Kwa maana hiyo, ni kwamba hufahamu utoto wa Jenerali Ulimwengu na kwahiyo; kama unasema alikuja akiwa na miaka 5 ni lazima itakuwa ni habari ya kusikia!

Weka source yako hapa!!!!

Kwamba, serikali ya Mkapa ilim-pin down kwa sababu alikuwa Mnyarwanda.... unataka kuniambia kwa zaidi ya miaka 6 ya mwanzo ya uongozi wa Mkapa haikufahamu kwamba Jenerali ni Mnyarwanda lakini ikaja kufahamu pale alipoanza kuandika makala za kuikosoa serikali yake?! Au angeendelea kuishi kama "mhamiaji haramu" endapo tu asingeiandika vibaya serikali?!

By 2001, Ulimwengu alikuwa na umri wa +50 years. Na hata tuki-assume maelezo yako kwamba ni kweli aliingia akiwa na 5 years; ina maana aliishi 45 years akiwa "Mhamiaji Haramu" na wakati huo alikuwa tayari kahudumu serikalini na bado hawakujua kwamba si raia?!

Ni nini kiliupumbaza serikali isichunguze uraia wake kwa miaka yote hiyo lakini ikaja kuchunguza uraia wake wakati ameshakuwa mzee?!

Kwamba mengine yote ni blah blah.... ukweli ni kwamba blah blah ndo hizo unazoleta wewe!!!
 
Mkuu, suala ni je ni kweli Ulimwengu hakuwa raia wa Tanzania, kama serikali ilivyotaka kutuaminisha huko nyuma? Nikirudi kwenye hoja yako, unaposema kuwa Ulimwengu ni "Mnyawaranda" unaweza kutusaidia kujua kwanini mpaka leo yupo nchini na anafahamika kama Mtanzania mwenzetu? Wazungu wanasema ... "support your claim". Hebu na wewe tuweke sawa Mkuu.
Sahau kupata majibu
 
Naomba usipinge sana suala la dini kumfanya awe kinyonga wa majina. Ktk tawala za nchi hii watu wamekuwa wakiiga udhaifu au muonekanao wa kiongozi mkuu wa nchi ili waendelee kuonekana.
Wakati wa Nyerere tulivaa Chou en-lai (Zhou enlai) kama yeye alivyofanya. Hata Kawawa akavaa lubega ya Ghana kama Nyerere alivyomuiga Nkuruma. Kipindi cha Mwinyi kuna watu walihama msikiti mmoja hadi mwingine ili tu wawe swala moja na Rais. Uliza misululu ya kuelekea Tandika ilivyokuwa ijumaa kadhaa. Wengine wakaandikwa kwa kuweka vyumba (au misikiti) ofisini.

Siyo ajabu kwa Ulimwengu kuinua majina ya Twaha .. ili kuonekana udhaifu ulishaonekana kwa mtawala.
Ukinyonga wa majina kivipi?! Umeshawahi kusikia historia yake ya kuitwa Ulimwengu na Twaha?!!

Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, ni kwamba Baba ake mzazi, yaani Mzee Khalfani Ulimwengu alikuwa na ukaribu na Mzungu mmoja aliekuwa anamiliki gari aina ya Ford. Sikumbuki vizuri lakini nadhani kulikuwa na uhusiano fulani na General Motors... maybe aliinua GM!!

Sasa Mzee Khalfani akawa amelipenda hilo jina la General/Jenerali na hivyo akajiwekea nadhiri kwamba akipata mtoto wa kiume atampa jina Jenerali!!!

Kwa bahati mbaya au mzuri mtoto wa kwanza wa Mzee Khalfani alizaliwa mwanamke kwahiyo akashindwa kumpa hilo jina na badala yale akampa jina la Nyangasa (am not sure manake sitoki pande hizo lakini linafanana na hilo).

Mtoto wa pili kuzaliwa akawa mwanaume ndipo akampa hilo jina la Jenerali! Walipokuwa wakubwa kidogo akawapeleka madrasa... sasa mambo ya wakati ule walimu wa pale madrasa wataka wapatiwe majina ya Kiarabu! Kutokana na hilo, yule Nyangasa akajiita Zainabu na Jenerali akajiita Twaha!

Na kwavile hata alipoenda shule aliingia kwenye shule ya Kiislamu; sina shaka huko nako alitumia Twaha! Kwa maana nyingine, Twaha ndio jina lake official lakini Ulimwengu pia ni jina lake!!!

Sasa tangu lini mtu kutumia jina lake ionekane ni ukinyonga?!

Bernie Fikiri
 
Kwenye siasa huwa kuna degree of tolerance, kiasi chake huwa kinatofautiana ikiwa mna itikadi sawa au tofauti!!
Huyo mzee siyo raia, na ndiyo amechana mbeleko sasa...
Sikufahamu hili, ok thanks mkuu nimekusoma
 
Chokochoko zimeanza kujaribu kumnyamazisha Ulimwengu kama yule mjinga Wa awamu ya tatu alivyomnyan'ganya uraia.
 
Kalne=Karne.

Ni muhalifu ndio maana kakimbilia chadema, ambako ndio kuna genge la wahalifu, ukiwa jambazi, muuza unga, teja,mwizi, mmbakaji, muuza viwanja vya watu n.k we kimbilia chadema utawekewa wakili.
Wewe kweli choco-late. Hivyo viwanda ndio vitapatikana kwa ndio mzee zenu!? Endeleeni kumtukuza mungu wenu Juma maharagwe.
 
Kizazi cha 'voda fasta', kama Jenerali anavyopenda kuwaita, hakiwezi na wala hakitaki kujua nchi hii imetoka wapi. Wengi wao ni waathirika wa 'collective imbecilisation' kama anavyoandika Jenerali. Baadhi ni 'mamluki'; watu waliopewa kazi ya propaganda chafu dhidi ya raia wema wanaojaribu kutumia elimu yao, maarifa na uzoefu wao kwa faida ya nchi yao. Mamluki hawashughulishwi na mustakabali wa taifa, bali na matumbo yao. Watu wazima wanaomjua Jenerali wako kimya; hawana baya kumhusu. Kwanza, wanamjua ni mwana-ccm mpaka leo. Lakini vijana wanaodhani wanaipigania ccm wanamwita kila jina baya! Je, ni yale yale ya Warioba? Jenerali yeye ameamua kuwa uanachama wake siyo wa kushangilia kama zuzu; wala siyo wa kunyamazia mambo yakiharibika. Sivyo alivyolelewa na Nyerere. Alilelewa kupigania maslahi ya taifa na kukosoa kwa maslahi mapana ya nchi. Alifanya hivyo kupitia The Daily News, ile safu ya "The Way I see it", aliyorithi kutoka kwa Phillip Ochieng, nadhani 1972. Nyerere hakuona shida; badala yake alimwandaa kwa madaraka makubwa zaidi. Hatimaye akawa Mbunge wa viti vya vijana na wakati huo huo DC miaka ya 1990. Akajiuzulu u-DC kwani ulikuwa unambania uhuru wa kutekeleza wajibu wa ubunge. Ndipo akapata nafasi ya kushiriki kikamilifu kwenye harakati za G55. Kushiriki kwake leo katika jopo la mawakili kwenye shauri la kikatiba lililofunguliwa na Mbowe hakumfanyi kuwa Chadema; bila shaka yeye anaamini ni jukumu la kitaaluma na kiraia. Jenerali ni mfuasi wa falsafa ya Nyerere. Makala zake zinaonyesha anakerwa sana na viongozi wanaojinasibu na Nyerere huku matendo yao yakiwa kama mbingu na ardhi kwa kile Mwalimu alichopigania; yaani taifa la watu huru, lenye umoja na usawa na lisilo na ubaguzi wa aina yoyote. Makala hizo ndizo zinazowasumbua hata vijana wa kizazi cha 'voda fasta' ambao wameaminishwa na kupandikizwa chuki dhidi ya raia wenzao wenye mtazamo tofauti.
You made my day! Elimu ya siasa tuliyoisoma sasa hivi inafundishwa kwa kimombo na ni kama history distorted jovyo hawa voda fasta hawawezi jua tulitoka wapi tupo wapi na tunakwenda wapi.
 
Watz tunachukiana sana, umaskini umedhoofisha kufikiri kwetu. Hata maofisini hizi roho mbaya zipo. Mtu amesoma lakini kuona kwake ni mufilisi kabisa
Mkuu wewe mbona unaleta porojo tu, Usicheze kabisa na Usalama Kuna watu wanaitwa striper Agents ni Hatari sana kwa Long term security hawa utakaa nae utaishi nae na ata behave Full kama mko wote kumbe anatafuta njia ya kupenya tu ikulu, Jiulize huyo jamaa alifikaje Ikulu mana amewah fanya kazi apo.
 
"Jenerali Ulimwengu" is a revolutionary credo he self-assumed during revolutionary heydays, especially while taking part in the students political debates or as byline when he wrote articles in the Daily News. But from Kamachumu Primary School, Kaigara Middle School, Nyakato Secondary School, Tabora (High) School and the UDSM, his true official names were Twaha Khalifan, not Jenerali Ulimwengu.
Kwa waliosoma Tabora School kuna majina waliowahi kuwa viongozi wa wanafunzi yameandikwa kwenye mbao ukutani dinning hall. Jina la Jenerali Ulimwengu lipo sikumbuki alikuwa kiongozi wa nini
 
ukiona mtu yupo chadema hujue huko nyuma alisha alibu, anatafuta tu huruma za wananchi
 
Naona vijana wasiofahamu chochote juu huyu mmoja ya wanahalisi wa Africa wanabwabwaja tu.
 
Mkuu wewe mbona unaleta porojo tu, Usicheze kabisa na Usalama Kuna watu wanaitwa striper Agents ni Hatari sana kwa Long term security hawa utakaa nae utaishi nae na ata behave Full kama mko wote kumbe anatafuta njia ya kupenya tu ikulu, Jiulize huyo jamaa alifikaje Ikulu mana amewah fanya kazi apo.
Hakuna cha porojo, Watz hii tabia tunayo sana. Nawe unaonesha umo kwenye hilo kundi. Mtu akikuzidi akili mnamwinukia oooohh mara agent, ooohh mara mchochezi, ooohh mara what!!! Very sad, picha hii ipo kila mahali, mitaani mpaka maofisini.

Unaweza kukataa lakini ukweli unabaki ukweli. Acheni kujenga chuki, jifunzeni kwa wenye akili sio kwa vilaza. Ndiyo maana tunachekwa na Noran. Akija mweupe utamuona ni mzalendo, mzawa nyang'au na kumvua uraia. Siipendi hii tabia ya ubaguzi ila basi!!!
 
20170305_143846.jpg


20170305_143747_001.jpg


20170305_143730_005.jpg


Mwanamapinduzi,Mwana wa Afrika.
 
Hakuna cha porojo, Watz hii tabia tunayo sana. Nawe unaonesha umo kwenye hilo kundi. Mtu akikuzidi akili mnamwinukia oooohh mara agent, ooohh mara mchochezi, ooohh mara what!!! Very sad, picha hii ipo kila mahali, mitaani mpaka maofisini.

Unaweza kukataa lakini ukweli unabaki ukweli. Acheni kujenga chuki, jifunzeni kwa wenye akili sio kwa vilaza. Ndiyo maana tunachekwa na Noran. Akija mweupe utamuona ni mzalendo, mzawa nyang'au na kumvua uraia. Siipendi hii tabia ya ubaguzi ila basi!!!
Wasi wasi ni Akili Boss, Harafu haya mambo ya kusema katuzidi Elimu wewe una uhakika gani nayo Au unatakwimu za Member wote humu juu ya Level yao ya Elimu? Huyo jamaa ni Tsu lazima tuwe care nae tu mana tabia zao tunazijua Visasi visivyo na Ukomo, Hatumbagui ila hatuwezi kusema Tumpe Uhuru Full no
 
Nadhani sasa unaleta Siasa bila sababu. Twaha Khalifani alizaliwa Rwanda na alikuja Tanganyika kama migrant akiwa na baba yake wakati huo akiwa na umri wa miaka 5. Tusipende kupotosha, Serikali ya Mkapa ilim-pin down kwa kuwa kisheria Twaha Khalifani ni munyarwanda, ila ku-quaify uraia wa Tanzania alitakiwa kuwa amekana uraia wa Rwanda, jambo ambalo hadi 2001 wakati wa kunyang'anywa uraia hakuwa ametimiza takwa hilo la kisheria. Stories nyingine ni blah blah tu. Baba yake Twaha alizikwa Kamachumu. Dadake pekee wa Twaha anayeitwa Zainabu ni mjane wa Peter Claver Bakilana (1939-2012) [rip] aliyewahi kuwa CEO wa THA (sasa TPA), TRC (sasa TRL) na NTC. Twaha huwa haendi kwao Kamachumu kwa sababu shamba la babake aliliuza.
Uongo first grade. Ulimwengu amezaliwa 1948. Kama aliingia Tanzania akiwa na miaka mitano hapo ni 1952. Hakukuwa na Taifa LA Rwanda wala Tanganyika!! Na kwa maana hiyo hakuwa RAIA wa Rwanda.

Yeyote aliyekuwapo Tanganyika wakati inapata Uhuru ni Mtanganyika na kwa maana hiyo Mtanzania.

Ukiwa muongo usiwe msahaulifu
 
Kwa facts zako hizi ambazo naweza kupata proof, ndo maana nimekuwa nikigomba na wana JF ambao kila wakati ni kumeza tu wanachosikia au kuambiwa. Hawana muda wa kujiuliza na wakati mwingine unaweza kutukana kwamba hawawazi. Ulipomtaja Shemejiye, nimelitafuta jina hilo na kukuta tanzia iliyoandikwa na yeye Ulimwengu akimtaja ni shemejiye ndani ya Rai 2012.

Iko hapa; Kwaheri Bakilana, daima utakuwa mioyoni mwetu – Raia Mwema

Nisichoelewa ni kwa status kama hii ambayo imekuwa siioni ktk sheria ya uraia. Juu ya watu ambao wakati wa kupata uhuru walikuwa ndani ya Tanganyika.
Fact!! Mkuu tafakari kidogo. Hivi mwaka 1952 kulikuwa na Uraia au Taifa la Rwanda?
 
Wasi wasi ni Akili Boss, Harafu haya mambo ya kusema katuzidi Elimu wewe una uhakika gani nayo Au unatakwimu za Member wote humu juu ya Level yao ya Elimu? Huyo jamaa ni Tsu lazima tuwe care nae tu mana tabia zao tunazijua Visasi visivyo na Ukomo, Hatumbagui ila hatuwezi kusema Tumpe Uhuru Full no
Sijui kama kweli umeisoma post vizuri, hakuna niliposema elimu, nimesema akili, akili na elimu ni vitu viwili tofauti. Hii tabia iko wazi ktk jamii yetu, of which you're part of. Ipo mitaani kwetu na kwenu pia na imeenda mpaka maofisini, tunachukiana sana kwa sababu za kisiasa, kidini, kiuchumi, kiuwezo kichwani. Ukiwa public figure, omba upendwe kwa ukweli wako, ukichukiwa tu, unavuliwa uraia. We have to change our mind set. Kuna watu ambao ni maprof. wanawekea wenzao kuta wasifanikiwe, shida sio elimu shida ni akili ya kupambanua mambo.
 
Unasahihisha "typo errors" badala ya mahudhui, hakika hiyo ni dalili tosha ya madhara ya utumiaji unga au viroba. Jisalimishe mapema upate tiba na kwa vile vita imekolea!
"Kudharirirshwa" hii nayo ni typing error?
 
Back
Top Bottom