Wasifu(CV) ya Jenerali Ulimwengu

Wasifu(CV) ya Jenerali Ulimwengu

[QUOTE="
Kenge (Eng) said:
Huyu mnayemuongelea ni mhaya wa Kamachumu, wilaya ya Muleba mkoa wa Kagera. Ni mzaliwa wa pale ambapo kuna hata kaburi la Babu wa Babu yake.

Kwa kifupi history ya migration wahaya wote ni wakuja pale lkn ni kabla ya mwaka 1850 hivi. Sasa huyu atakuwa raia wa nchi gani. Histori ya ukoo inaonyesha walitokea RWANDA.

Amesoma shule ya msingi Rwanga, Kamachumu
Secondary Ihungo ambapo kulingana na vipaji vyake kwenye michezo ndo kapewa nick name(s) Jenerali Ulimwengu, yeye ni TWAHA Byeshurilo Ismail.

Amesoma darasa moja na FREEMAN MBOWE pale Ihungo Secondary.
.[/QUOTE]
Huyu naye katuwekea uongo wake hapa. Ni ushabiki tu. Twaha hakuwahi kusoma sekondari ya Ihungo bali Nyakato. Mbowe alisoma Ihungo high school kati ya 1981/82-82/83 wakati Twaha alisoma Nyakato miaka ya 1960. Tusiemuke!
 
Siyo Mzalendo yule. Ni mnafiki kama Zitto. Ana hasira na visasi sababu nchi yake ya asili karibu raia wake wote ni watu wa visasi vya kudumu tena wengine wanarithishwa.
Kama ni hivyo basi anafanana na Bwana huyu. Kwahiyo hata Bwana huyu inawezekana hii siyo nchi yake ya asili.
 
Nadhani sasa unaleta Siasa bila sababu. Twaha Khalifani alizaliwa Rwanda na alikuja Tanganyika kama migrant akiwa na baba yake wakati huo akiwa na umri wa miaka 5. Tusipende kupotosha, Serikali ya Mkapa ilim-pin down kwa kuwa kisheria Twaha Khalifani ni munyarwanda, ila ku-quaify uraia wa Tanzania alitakiwa kuwa amekana uraia wa Rwanda, jambo ambalo hadi 2001 wakati wa kunyang'anywa uraia hakuwa ametimiza takwa hilo la kisheria. Stories nyingine ni blah blah tu. Baba yake Twaha alizikwa Kamachumu. Dadake pekee wa Twaha anayeitwa Zainabu ni mjane wa Peter Claver Bakilana (1939-2012) [rip] aliyewahi kuwa CEO wa THA (sasa TPA), TRC (sasa TRL) na NTC. Twaha huwa haendi kwao kamachumu kwa sababu shamba la babake aliliuza.
Kwa facts zako hizi ambazo naweza kupata proof, ndo maana nimekuwa nikigomba na wana JF ambao kila wakati ni kumeza tu wanachosikia au kuambiwa. Hawana muda wa kujiuliza na wakati mwingine unaweza kutukana kwamba hawawazi. Ulipomtaja Shemejiye, nimelitafuta jina hilo na kukuta tanzia iliyoandikwa na yeye Ulimwengu akimtaja ni shemejiye ndani ya Rai 2012.

Iko hapa; Kwaheri Bakilana, daima utakuwa mioyoni mwetu – Raia Mwema

Nisichoelewa ni kwa status kama hii ambayo imekuwa siioni ktk sheria ya uraia. Juu ya watu ambao wakati wa kupata uhuru walikuwa ndani ya Tanganyika.
 
Siyo Mzalendo yule. Ni mnafiki kama Zitto. Ana hasira na visasi sababu nchi yake ya asili karibu raia wake wote ni watu wa visasi vya kudumu tena wengine wanarithishwa.
Tunaomba mfano mmoja wa mtu aliemlipizia Kisasi
 
Mkuu acha kutoa mapovu. Mimi sijasema kuhusu ushiriki wake ama mabaya yake ila nasema kwa kinywa kipana kwamba si Mtanzania. Naweza kuwa nina reservations lakini sijasema. Kitu ninachoweza kusema ni kwamba wakati wa mauaji ya 1994 kule Rwanda, Wanyarwanda wengi waliokuwa Tanzania walishiriki kwa njia moja ama nyingine.

Ila nafahamu kwamba Kabila aliponyakua madaraka kule Zaïre akishirikiana ana akina Bizima Karaha (Banyamulenge), Generali na Prof. Wamba dia Wamba walikuwa watu wa kwanza kwanza kufika kule.
Hata Nyerere alienda pia
 
Ulimwengu ni boya. Hana kitu. Roho mbaya kama Kagame. Huyu alishiriki mauaji ya Rwanda 1994. Kwakuwa yupo upande wa kagame ndiyo maana hawezi kamatwa.
Msitumie kichaka hiki cha kufichwa na jamiiforums na kutoa maneno ya kashfa kwa wengine mkjiua hamtawajibika kwa sababu mmefichwa na jamiiforums.
Wewe ndugu nikweli unauhakika kuwa generali ulimwengu alwahi kuhusika na mauaji ya kimbari ya Rwanda?
Tuwe great thinkers wa kweli si kutengenza majungu kwa chuki zisizo nz msingi kivile.
Generali ulimwengu amekuwepo Tanzania tangia mimi naanza kupata ufahamu hadi leo nikiwa na umri huu wa miaka 58, nakushangaa ni lini aliwahi kuwa Rwanda.
Jukwaa hili limekimbiwa na watu makini wengi sana kwa sababu ya watu kulifanya la hovyo kwa kupost mambo yasiyofanyiwa utafiti wo wote.
 
Acha roho mbaya. Jenerali Ulimwengu ni Mtanzania. Hajawahi shiriki udharimu unaotaka kutuaminisha hapa. Unamsingizia mabaya kwa sababu ya misimamo yake ya kutopindisha lugha, akisimama kutoa hoja wenye akili huwa tunatulia kupata madini ghafi. Ana fikra huru, haishi kwenye kibuyu, haelekezwi cha kuandika. Ni msomi mwenye mawazo huru sio mtumwa wa mtu
Kwa sentence 1 tu: Jenerali hawazi kwa kutumia tumbo!
 
Walijipenyeza humu wengi tu. Balozi Timothy Bandora naye alijipenyeza hadi akawa balaozi wetu nchi kadhaa kumbe hakuwa raia. Wakamshitukia wakampokonya uraia. Nadhani yupo Rwanda
Ni mtanzania. Watu wa mipakani huwa wana ndugu nchi jirani, ni kawaida.
 
Kabila alikuwa mzalendo na hakuwahi kuongoza Zaire bali Drc na msimamo wake ukiungwa mkono Nyerere na Ulimwengu lkn siyo hivyo tu Ulimwengu alienda kupigana Msumbiji kabla mbona huulizi kwanini ="Kimbunga, post: 19989829, member: 6294"]Mkuu nikuweke tu sawa kwamba mimi simchukii Jenerali Twaha Ulimwengu. Mimi binafsi namheshimu sana. Najua ni mpambanaji asiyechoka na naifahamu misimamo yake tangia zamani. Nafuatilia makala zake nyingi tangia wanaanzisha Dimba na Rai hadi Raia mwema. Nafuatilia makala zake kwenye gazeti la The East African pia. Kusema kwamba alishawahi kupokonywa uraia si chuki bali ukweli.
Hilo la akina Kabila najua kwamba Mzee Kabila alitoka hapa na alikuwa anaishi hapa tangia wakati wa Nyerere na alikuwa akiungwa mkono. Najua pia unafahamu kilichomkumba Mzee Kabila baada ya kufarakana na akina Bizima Karaha.
Hapo kwenye kwenda Zaire kwa Twaha nilikuwa nataka uone jinsi alivyokuwa na nasaba na akina Bizima ambao walikuwa ni de facto leaders wa Zaire ya Mzee Kabila.[/QUOTE]
 
Siyo Mzalendo yule. Ni mnafiki kama Zitto. Ana hasira na visasi sababu nchi yake ya asili karibu raia wake wote ni watu wa visasi vya kudumu tena wengine wanarithishwa.
Hahah aisee kweli naamini kumbe mambo mengi humu wengi huwa wanaropoka ropoka tu
 
Povu mnatoa nyie wenye roho mbaya, mmekalia kuwavua uraia Watz wenzenu. Tena bila haya, miongoni waliomuunga mkono Kabila ni Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere, mbona yeye hujamtaja. Moja ya tatizo letu kubwa, tukitofautiana na mwenzetu kimawazo, na hasa ukikuzidi uwezo wa kiakili. Badala ya kujifunza kutoka kwake, unavua uraia. Dunia ilitusuta kwa kumvua uraia Jenerali Ulimwengu na kumfanya stateless, wakaona aibu wakamrejeshea uraia wake. Leo nawe unakuja na ujinga ule ule wa kumvua uraia. Kazaliwa Tanzania, kakulia Tanzania, kazeekea Tanzania. Acheni roho mbaya
Mkuu wasamehe.
 
Mkuu hapo sasa unaposema aliomba na kupewa ndipo nawe unachanganya mambo. Uraia wa kuzaliwa ni haki yako na wala huuombi. Kama aliomba basi uraia wa kuzaliwa unakuwa umefutwa.
Nimesema alinyang'anywa uraia na sina kumbukumbu kama aliomba na kupewa ila kuna wakati alikuwa akifanya kazi kwa vibali.
Msijitoe ufahamu, yote ilikuwa siasa. Na wengi mnafahamu hilo.
 
Babaake anaitwa "ulimwengu" jiulize amepata uraia wa tz lini alisota mapaka kaomba poo ndo kapewa sasa anaota mapembe
 
Hahah aisee kweli naamini kumbe mambo mengi humu wengi huwa wanaropoka ropoka tu
Wengi hawana maisha nje ya vyama vya siasa. Inabidi waelewe kwamba kuna wakati it's about the country sio vyama, kwa sababu Leo utakuwa huku na kesho kule. Lazima katiba itulinde wote Kama watanzania
 
Ulimwengu ni boya. Hana kitu. Roho mbaya kama Kagame. Huyu alishiriki mauaji ya Rwanda 1994. Kwakuwa yupo upande wa kagame ndiyo maana hawezi kamatwa.
wewe una roho nzuri kama mama huruma.
 
Anapodharirishwa=Anapodhalilishwa

Stahili=Stahiki

Kuchikua=Kuchukua
Unasahihisha "typo errors" badala ya mahudhui, hakika hiyo ni dalili tosha ya madhara ya utumiaji unga au viroba. Jisalimishe mapema upate tiba na kwa vile vita imekolea!
 
Mods naomba tuepuke mada/hoja za kuzalilisha watu. Michango ya hayo niliowanukuu kwenye mada kuu haina faida yoyote katika kuelimishana zaidi ya kuwachafua watu, wengine wakiwa kioo katika jamii.

JF isiwe kijiwe cha udaku na majungu.

Wazo muhimu hili.

Hao uliowanakili ni watu wasiompenda kabisa mtu anayeonyesha misimamo tofauti na serikali. Hawataki au hawawezi kuwa objective katika hilo. Ni dhahiri kabisa kuwa harakati za kumnyang'anya Jenerali Ulimwengu uraia na kumnasibisha na Rwanda na Burundi zilianza mara baada ya yeye kupishana na utawala uliokuwepo kimsimamo, period. Kama si hivyo angekuwa anamiminiwa kila sifa ya uzalendo.

Leo hii Kinana akileta jeuri dhidi ya serikali na chama anarudishwa "kwao Somalia" fasta. Hata Mkapa angepishana na serikali kabla hajawa rais angepelekwa home "Msumbiji".

Tujadili watu kwa merit zao. Kuna mahali unaweza kumkosoa Jenerali hata katika kuitetea serikali lakini si kwa uraia, uzalendo, visirani, ujinga, n.k. Let's be objective.
 
Back
Top Bottom