Tumia hiyo link kupata CV yake!
Hiyo link yenye half baked biography ya Ulimwengu inajaribu kumtetea kwa kutumia hoja za Nyerere dhidi ya Iddi Amini wakati alipowafukuza wahindi Uganda. Mahasimu wake walitaka Ulimwengu aende wapi, mwezini?
Well, labda wangeaza kwa kutuambia kwa nini Ulimwengu alikuwa kama Mhindi wa Uganda. Mhindi wa Uganda hakuwa mzawa. Whether unakubaliana au hukubaliani na sera za ukuu wa wazawa mbele ya wakuja, jambo moja wote tunakubaliana ni kwamba Wahindi hawakuwa wazawa! Huwezi kulikwepa hilo.
Sasa Jenerali Ulimwengu ana background gani kiuraia kiasi kwamba hata wanaomtetea wanamfananisha na wahindi wa Uganda?
Wanakiri watetezi wake kwamba Ulimwengu aliomba uraia akanyimwa. Well, kwa nini alitakiwa kuomba? Mbona sisi wengine hatujawahi kutakiwa kuomba uraia? Mbona hamsemi ana nini Ulimwengu kwenye uzawa wake?
Jibu moja la haraka haraka kwa nini Ulimwengu amekuwa akibanwa-banwa na sheria ni kwa vile hakuzaliwa Mtanzania. He is not a natural born citizen of Tanzania. Hilo tusilikwepe.
Inawezekana kabisa, na mimi naamini ndivyo ilivyo, sheria ilitumika dhidi yake binafsi kwa sababu za kisiasa, lakini mwisho wa siku aliyetenda kitendo cha kumtangaza kama sio raia alitumia sheria. Na hilo nalo huwezi kulikwepa!
Sasa kibaya kilichopo ni kwamba Waafrika huwa hatuandiki historia, hatuandiki biography zetu. Tunamsifuje mtu kwamba ni mwanazuoni anaeheshimika, mwandishi mahiri, mwanafikra pevu, halafu mtu mwenyewe hajawahi kuandika chochote kuhusu maisha yake? Background yake giza tupu! Ndio maana wanampa vyeo wanamnyang'anya, wanamtishia-tishia kumkamata, wanamrusha-rusha kama M-mexico aliyeruka ukuta kuingia Marekani ya Donald Trump.
Inawezekana kuna fomu alishawahi kujaza kuomba uraia wa Rwanda akajifuta wa kwetu. Au wa Algeria, huko alikokuwa, halafu Tanzania ikainasa fomu. Na ndo maana tunaambiwa Serikali haijawahi kumwambia sababu ya kumkatalia wala sisi hatujaambiwa. Well, yeye anajua! Ulimwengu sio unschooled peasant anyimwe kitu asiulize kwa nini, anajua!
Na hapo bado hatujauliza ilikua-kuaje akaitwa Generali Ulimwengu ilhali alizaliwaTwaha Khalfani?