Wasifu(CV) ya Jenerali Ulimwengu

Wasifu(CV) ya Jenerali Ulimwengu

Unamanisha haya:Twaha or Jenerali Khalfani Ulimwengu aliyezaliwa Ngara 1948 na kusoma elimu ya msingi Kamachumu, middle school Katoke, sekondari Nyakato na baadae Tabora Boys kabla hajaenda JKT na hatimae UDSM leo unasema Sophist kamuelezea vizuri kwa sababu amesema ni Mnyarwanda!!! Seriously?!!!

Jenerali huyu huyu ambae inasemekana hata baba ake mzazi Mzee Khalfani Ulimwengu na Babu yake Mzee Ulimwengu walikuwa ni watu walioheshimika sana Mkoa wa Ziwa Magharibi enzi hizo Tanzania ikiitwa Tanganyika lakini leo hii mnamuona Mnyarwanda kwa sababu tu amekuwa akiandika yale ambayo Mkapa hakupenda kuyasikia?!!!

Mungu anawaona mjue....
Kulikuwa na majadiliano marefu kuhusu ubora wa Ulimwengu. weka cursor yako click hapa;

Ulimwengu: Heaven knows where we are going, but Magufuli knows he can walk on water


Nenda post #7
 
Umeacha mambo ya msingi sana kuhusu Jenerali; ama kwa makusudi au kwa kutofahamu historia yake vizuri!!!

Kwamba, pamoja na Unyarwanda wa Jenerali/Twaha Ulimwengu (Twaha Ulimwengu or Jenerali Uimwengu) ambao ulioneshwa na serikali ya Mkapa lakini Mzee Khalfani Ulimwengu; Baba mzazi wa Jenerali/Twaha Khalfani Ulimwengu alikuwa ni mmoja wa watu walioheshimika sana miaka ya 1940's huko Mkoa wa Ziwa Magharibi; nchini Tanganyika!!!!!

Likewise, huyu Jenerali/Twaha Khalfani Ulimwengu, nae alizaliwa Tanganyika hii hii huko Ngara na kusoma Tanganyika hii hii ambapo, eilimu yake ya awali aliipatia Kamachumu na middle school Katoke tangu miaka hiyoooo... hata kabla ya uhuru!!!

Hata elimu ya sekondari, aliipatia Tanzania hii hii huko Nyakato na Tabora Boys kabla hajaenda JKT na hatimae UDSM!!

Lakini pamoja na yote hayo, miaka 54 baadae ndipo serikali ya Mkapa ikamuona eti sio Mtanzania!!!!!

Bado nina kumbukumbu ya Makala ya mwisho kabla Ulimwengu hajapigwa ban!!! Heading ya makala ile ilisomeka: Akina Jefferson na Magazeti!!

Kwamba, hapo kabla Rais Jefferson wa Marekani alijifanya ni mpenzi kweli kweli wa magazeti kwa sababu tu walikuwa wanamwandika vizuri! Lakini magazeti yale yale yalipoanza kuandika mabaya ya serikali ya Jefferson, Rais Jefferson akageuka kuwa mbogo na mkali kweli kweli dhidi ya magazeti!!!

Hivi ndivyo Mkapa alikuwa!! Mwanzoni alijifanya ni rafiki wa media jambo ambalo watu halikuwashangaza kwa sababu nae alipata kupitia huko hapo kabla! Lakini media zilipoanza kuandika maovu ya serikali ya Mkapa; Ben akageuka kuwa mbogo.... AKINA JEFFERSON NA MAGAZETI!!
Mkuu nashukuru kwa kuliweka vizuri. Pia nakumbuka kwamba Jenerali Ulimwengu alikuwa member kwenye timu ya kampeni ya Rais Mstaafu Mkapa.
 
Kuna kipindi nilisikia huyu jamaa ni mrundi ila bado sina uhakika maana ccm nawajua kwa fix

Siyo Mzalendo yule. Ni mnafiki kama Zitto. Ana hasira na visasi sababu nchi yake ya asili karibu raia wake wote ni watu wa visasi vya kudumu tena wengine wanarithishwa.

Chadema akili zenu fupi sana yaani mtu hata akiwa zuzu mtamwagia sifa zote ilimradi akija upande wenu,tatizo hata hamjiulizi kwa nini kaja kwetu mlivyo mazuzu

Mrundi , mrundi rundi

Ulimwengu ni boya. Hana kitu. Roho mbaya kama Kagame. Huyu alishiriki mauaji ya Rwanda 1994. Kwakuwa yupo upande wa kagame ndiyo maana hawezi kamatwa.

Generali Twaha Ulimwengu si Mtanzania, ni Mnyarwanda na siamini kama aliomba uraia baada ya kupokonywa.

Mods naomba tuepuke mada/hoja za kuzalilisha watu. Michango ya hayo niliowanukuu kwenye mada kuu haina faida yoyote katika kuelimishana zaidi ya kuwachafua watu, wengine wakiwa kioo katika jamii.

JF isiwe kijiwe cha udaku na majungu.
 
Mods naomba tuepuke mada/hoja za kuzalilisha watu. Michango ya hayo niliowanukuu kwenye mada kuu haina faida yoyote katika kuelimishana zaidi ya kuwachafua watu, wengine wakiwa kioo katika jamii.

JF isiwe kijiwe cha udaku na majungu.
Ila wengine wakidhalilishwa uje tena uandike hivi hivi sio kwa kuwa huyo ni mchadema.
 
Ni Mnyarwanda na alinyang'anywa uraia wa Tanzania yeye na akina Balozi Bandora, Castico, nk. Nadhani hakurudishiwa na kwa sasa anafanya kazi kama mgeni.
Ni mwandishi wa Habari na pia miaka kama mitatu nyuma alitunukiwa u advocate. Amewahi kuwa TYL na akawa mwakilishi wa Tanzania kule Algiers. Amewahi kuwa Mbunge wa kuteuliwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala wakati ule wa kuanzishwa kwa vyama vingi vya siasa. Wakati vyama vingi vinaanzishwa kulikuwa na sheria kwamba ukitaka kufanya maandamano ama mikutano unaomba kibali kwa mkuu wa wilaya. Basi huyu bwana alikuwa hana hiyana ya kutoa vibali kwa vyama. Akahamishwa kupelekwa Singida kama mkuu wa Wilaya. Kama sijasahu hakwenda Singida badala yake akajiuzulu ukuu wa Wilaya.

Huyo ndiye Generali Twaha Ulimwengu.
Na kupewa ukuu wa wilaya kumbe hakua raia? Kuna mambo nchi utadhani hao watawala ni vichaa
 
Siyo Mzalendo yule. Ni mnafiki kama Zitto. Ana hasira na visasi sababu nchi yake ya asili karibu raia wake wote ni watu wa visasi vya kudumu tena wengine wanarithishwa.
Kama ifanyikavyo kwa serikali ya sasa.
 
Je, una uhakika gani kama aliyeandika hii comment ni chadema? Generali ulimwengu hawezi kufahamika kwa kizazi cha sasa cha mwendo kasi. Watu tuliokuwa vijana wa TYL miaka ya sitini na sabini tunamjua saana. Muulize mzee Kikwete, waulize wana Tanu wote na jinsi vijana kama Ulimwengu walivyoiletea sifa nchi hii? Mtu zuzu asingeteuliwa kuwa Mwakilishi wa nchi nje hasa enzi hizo ambazo hazikuangalia umetoka familia gani na una nini. Tufanye research sisi tuliokuwa vijana wa TYL from sixtees na nyinyi mnajifanya wana CCM sasa nani ana uchungu wa nchi?

Kizazi cha 'voda fasta', kama Jenerali anavyopenda kuwaita, hakiwezi na wala hakitaki kujua nchi hii imetoka wapi. Wengi wao ni waathirika wa 'collective imbecilisation' kama anavyoandika Jenerali. Baadhi ni 'mamluki'; watu waliopewa kazi ya propaganda chafu dhidi ya raia wema wanaojaribu kutumia elimu yao, maarifa na uzoefu wao kwa faida ya nchi yao. Mamluki hawashughulishwi na mustakabali wa taifa, bali na matumbo yao. Watu wazima wanaomjua Jenerali wako kimya; hawana baya kumhusu. Kwanza, wanamjua ni mwana-ccm mpaka leo. Lakini vijana wanaodhani wanaipigania ccm wanamwita kila jina baya! Je, ni yale yale ya Warioba? Jenerali yeye ameamua kuwa uanachama wake siyo wa kushangilia kama zuzu; wala siyo wa kunyamazia mambo yakiharibika. Sivyo alivyolelewa na Nyerere. Alilelewa kupigania maslahi ya taifa na kukosoa kwa maslahi mapana ya nchi. Alifanya hivyo kupitia The Daily News, ile safu ya "The Way I see it", aliyorithi kutoka kwa Phillip Ochieng, nadhani 1972. Nyerere hakuona shida; badala yake alimwandaa kwa madaraka makubwa zaidi. Hatimaye akawa Mbunge wa viti vya vijana na wakati huo huo DC miaka ya 1990. Akajiuzulu u-DC kwani ulikuwa unambania uhuru wa kutekeleza wajibu wa ubunge. Ndipo akapata nafasi ya kushiriki kikamilifu kwenye harakati za G55. Kushiriki kwake leo katika jopo la mawakili kwenye shauri la kikatiba lililofunguliwa na Mbowe hakumfanyi kuwa Chadema; bila shaka yeye anaamini ni jukumu la kitaaluma na kiraia. Jenerali ni mfuasi wa falsafa ya Nyerere. Makala zake zinaonyesha anakerwa sana na viongozi wanaojinasibu na Nyerere huku matendo yao yakiwa kama mbingu na ardhi kwa kile Mwalimu alichopigania; yaani taifa la watu huru, lenye umoja na usawa na lisilo na ubaguzi wa aina yoyote. Makala hizo ndizo zinazowasumbua hata vijana wa kizazi cha 'voda fasta' ambao wameaminishwa na kupandikizwa chuki dhidi ya raia wenzao wenye mtazamo tofauti.
 
Ila wengine wakidhalilishwa uje tena uandike hivi hivi sio kwa kuwa huyo ni mchadema.

Kama una uhakika unachotaka kusema kuwa muwazi kwa kutumia mitandao yenye kutumia ID zilizo kweli ili mtu aweze kuchukua hatua pale anapodharirishwa.

Waheshimiwa waliodharirishwa wamachikua hatua stahili
 
Kulikuwa na majadiliano marefu kuhusu ubora wa Ulimwengu. weka cursor yako click hapa;

Ulimwengu: Heaven knows where we are going, but Magufuli knows he can walk on water


Nenda post #7
Mimi sifahamu Kiingereza lakini kwa kutumia kamusi sioni chochote cha maana alichoandika!!!

Kwamba, eti wakati wa Mwinyi Ulimwengu aliachana na mawazo ya kimapinduzi huku akisukumwa sana na masuala ya udini ni hoja inayoweza kutolewa na mtu aliyeishiwa na maarifa tu!

Ni mpuuzi tu ndie anaweza kuamini kwamba Jenerali Ulimwengu anafanya mambo kwa kusukumwa na udini!!!

Na sijui kwanini mwanzoni amemuita Ulimwengu lakini alipohusisha na utawala wa Mwinyi aka-highlight jina la Twaha Khalfani! Yaani anachotaka kutuaminisha ni kwamba, wakati wa Mwinyi ndo alipenda sana kutumika kwa jina la Twaha Khalfani ili tu ajitambulishe serikalini kwamba nae ni "mmoja wao!"

Na ni kuishiwa maarifa kuhusisha u-DC ambao alipewa na dini yake kwa sababu, hiyo haikuwa mara ya kwanza Ulimwengu kuhudumu serikalini!!!!

Lakini cha ajabu, mwisho wa hiyo post anaonesha kumbe povu lote alilomwaga ni kwa sababu tu anam-criticize JPM!!

Nimepekua pekua JF na kukutana na hii... sina shaka nawe ushapata kuiona:

Ulimwengu.png

Kwa mujibu wa alieambatanisha hiyo screenshot, hiyo ni habari ya 1993 na inaonekana kweli ni ya 1993 manake inazungumzia kujiuzuru kwake u-DC!!

Inawezekana 1993 ilionekana ni jambo lisilo la kweli lakini hivi sasa hata mtoto wa darasa la sita anafahamu CCM imejaa manyang'au!!!

Kauli kama hizo ndizo zinawafanya serikali, CCM na mawakala wao kumchukia Jenerali Ulimwengu!! Hata alipovuliwa uraia wake ilikuwa ni baada ya kuandika maovu ya serikali ya Mkapa! Ili kumnyamazisha; ndipo wakaja na hoja ya uraia lakini kwa bahati mzuri hajanyamaza wala haielekei kwamba atanyamaza!!!

Na kwamba Ulimwengu ni Mnyarwanda kwangu ni hoja isiyo na maana yoyote manake hata kama kweli angekuwa ni Mnyarandwa; basi ni bora niishi na Wanyarwanda 1000 wasio wezi kuliko kuishi na Mtanzania mmoja aliyejaa ulafi; wizi, fisadi na asiyetosheka!!!
 
Unamanisha haya:Twaha or Jenerali Khalfani Ulimwengu aliyezaliwa Ngara 1948 na kusoma elimu ya msingi Kamachumu, middle school Katoke, sekondari Nyakato na baadae Tabora Boys kabla hajaenda JKT na hatimae UDSM leo unasema Sophist kamuelezea vizuri kwa sababu amesema ni Mnyarwanda!!! Seriously?!!!

Jenerali huyu huyu ambae inasemekana hata baba ake mzazi Mzee Khalfani Ulimwengu na Babu yake Mzee Ulimwengu walikuwa ni watu walioheshimika sana Mkoa wa Ziwa Magharibi enzi hizo Tanzania ikiitwa Tanganyika lakini leo hii mnamuona Mnyarwanda kwa sababu tu amekuwa akiandika yale ambayo Mkapa hakupenda kuyasikia?!!!

Mungu anawaona mjue....
Nadhani sasa unaleta Siasa bila sababu. Twaha Khalifani alizaliwa Rwanda na alikuja Tanganyika kama migrant akiwa na baba yake wakati huo akiwa na umri wa miaka 5. Tusipende kupotosha, Serikali ya Mkapa ilim-pin down kwa kuwa kisheria Twaha Khalifani ni munyarwanda, ila ku-quaify uraia wa Tanzania alitakiwa kuwa amekana uraia wa Rwanda, jambo ambalo hadi 2001 wakati wa kunyang'anywa uraia hakuwa ametimiza takwa hilo la kisheria. Stories nyingine ni blah blah tu. Baba yake Twaha alizikwa Kamachumu. Dadake pekee wa Twaha anayeitwa Zainabu ni mjane wa Peter Claver Bakilana (1939-2012) [rip] aliyewahi kuwa CEO wa THA (sasa TPA), TRC (sasa TRL) na NTC. Twaha huwa haendi kwao Kamachumu kwa sababu shamba la babake aliliuza.
 
Ni Mnyarwanda na alinyang'anywa uraia wa Tanzania yeye na akina Balozi Bandora, Castico, nk. Nadhani hakurudishiwa na kwa sasa anafanya kazi kama mgeni.
Ni mwandishi wa Habari na pia miaka kama mitatu nyuma alitunukiwa u advocate. Amewahi kuwa TYL na akawa mwakilishi wa Tanzania kule Algiers. Amewahi kuwa Mbunge wa kuteuliwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala wakati ule wa kuanzishwa kwa vyama vingi vya siasa. Wakati vyama vingi vinaanzishwa kulikuwa na sheria kwamba ukitaka kufanya maandamano ama mikutano unaomba kibali kwa mkuu wa wilaya. Basi huyu bwana alikuwa hana hiyana ya kutoa vibali kwa vyama. Akahamishwa kupelekwa Singida kama mkuu wa Wilaya. Kama sijasahu hakwenda Singida badala yake akajiuzulu ukuu wa Wilaya.

Huyo ndiye Generali Twaha Ulimwengu.
Kisa Cha kupigwa transfer kwenda singida ambako hakwenda ilikuwa ni kutofautiana Na mkuu wamkoa Wakati huo Mary Chips kuhusu mihadhara ya waislamu Mkuu wa wilaya aliyapiga marufuku , mkuu wa mkoa alikuwa muoga kuyapiga marufuku Na Raisi Wakati huo alikuwa Alhaji Ali Hassan Mwinyi
 
Kama una uhakika unachotaka kusema kuwa muwazi kwa kutumia mitandao yenye kutumia ID zilizo kweli ili mtu aweze kuchukua hatua pale anapodharirishwa.

Waheshimiwa waliodharirishwa wamachikua hatua stahili
Anapodharirishwa=Anapodhalilishwa

Stahili=Stahiki

Kuchikua=Kuchukua
 
Chadema akili zenu fupi sana yaani mtu hata akiwa zuzu mtamwagia sifa zote ilimradi akija upande wenu,tatizo hata hamjiulizi kwa nini kaja kwetu mlivyo mazuzu
Umewaona aisee...angalau kwetu tuna PhD holder asitejue kizungu
 
Mimi sifahamu Kiingereza lakini kwa kutumia kamusi sioni chochote cha maana alichoandika!!!

Kwamba, eti wakati wa Mwinyi Ulimwengu aliachana na mawazo ya kimapinduzi huku akisukumwa sana na masuala ya udini ni hoja inayoweza kutolewa na mtu aliyeishiwa na maarifa tu!

Ni mpuuzi tu ndie anaweza kuamini kwamba Jenerali Ulimwengu anafanya mambo kwa kusukumwa na udini!!!

Na sijui kwanini mwanzoni amemuita Ulimwengu lakini alipohusisha na utawala wa Mwinyi aka-highlight jina la Twaha Khalfani! Yaani anachotaka kutuaminisha ni kwamba, wakati wa Mwinyi ndo alipenda sana kutumika kwa jina la Twaha Khalfani ili tu ajitambulishe serikalini kwamba nae ni "mmoja wao!"

Na ni kuishiwa maarifa kuhusisha u-DC ambao alipewa na dini yake kwa sababu, hiyo haikuwa mara ya kwanza Ulimwengu kuhudumu serikalini!!!!

Lakini cha ajabu, mwisho wa hiyo post anaonesha kumbe povu lote alilomwaga ni kwa sababu tu anam-criticize JPM!!

Nimepekua pekua JF na kukutana na hii... sina shaka nawe ushapata kuiona:

View attachment 477017
Kwa mujibu wa alieambatanisha hiyo screenshot, hiyo ni habari ya 1993 na inaonekana kweli ni ya 1993 manake inazungumzia kujiuzuru kwake u-DC!!

Inawezekana 1993 ilionekana ni jambo lisilo la kweli lakini hivi sasa hata mtoto wa darasa la sita anafahamu CCM imejaa manyang'au!!!

Kauli kama hizo ndizo zinawafanya serikali, CCM na mawakala wao kumchukia Jenerali Ulimwengu!! Hata alipovuliwa uraia wake ilikuwa ni baada ya kuandika maovu ya serikali ya Mkapa! Ili kumnyamazisha; ndipo wakaja na hoja ya uraia lakini kwa bahati mzuri hajanyamaza wala haielekei kwamba atanyamaza!!!

Na kwamba Ulimwengu ni Mnyarwanda kwangu ni hoja isiyo na maana yoyote manake hata kama kweli angekuwa ni Mnyarandwa; basi ni bora niishi na Wanyarwanda 1000 wasio wezi kuliko kuishi na Mtanzania mmoja aliyejaa ulafi; wizi, fisadi na asiyetosheka!!!
Naomba usipinge sana suala la dini kumfanya awe kinyonga wa majina. Ktk tawala za nchi hii watu wamekuwa wakiiga udhaifu au muonekanao wa kiongozi mkuu wa nchi ili waendelee kuonekana.
Wakati wa Nyerere tulivaa Chou en-lai (Zhou enlai) kama yeye alivyofanya. Hata Kawawa akavaa lubega ya Ghana kama Nyerere alivyomuiga Nkuruma. Kipindi cha Mwinyi kuna watu walihama msikiti mmoja hadi mwingine ili tu wawe swala moja na Rais. Uliza misululu ya kuelekea Tandika ilivyokuwa ijumaa kadhaa. Wengine wakaandikwa kwa kuweka vyumba (au misikiti) ofisini.

Siyo ajabu kwa Ulimwengu kuinua majina ya Twaha .. ili kuonekana udhaifu ulishaonekana kwa mtawala.
 
Inawezekana kabisa ilikua ni visa vya kisiasa
Kwenye siasa huwa kuna degree of tolerance, kiasi chake huwa kinatofautiana ikiwa mna itikadi sawa au tofauti!!
Huyo mzee siyo raia, na ndiyo amechana mbeleko sasa...
 
Back
Top Bottom