Mimi sifahamu Kiingereza lakini kwa kutumia kamusi sioni chochote cha maana alichoandika!!!
Kwamba, eti wakati wa Mwinyi Ulimwengu aliachana na mawazo ya kimapinduzi huku akisukumwa sana na masuala ya udini ni hoja inayoweza kutolewa na mtu aliyeishiwa na maarifa tu!
Ni mpuuzi tu ndie anaweza kuamini kwamba Jenerali Ulimwengu anafanya mambo kwa kusukumwa na udini!!!
Na sijui kwanini mwanzoni amemuita Ulimwengu lakini alipohusisha na utawala wa Mwinyi aka-highlight jina la Twaha Khalfani! Yaani anachotaka kutuaminisha ni kwamba, wakati wa Mwinyi ndo alipenda sana kutumika kwa jina la Twaha Khalfani ili tu ajitambulishe serikalini kwamba nae ni "mmoja wao!"
Na ni kuishiwa maarifa kuhusisha u-DC ambao alipewa na dini yake kwa sababu, hiyo haikuwa mara ya kwanza Ulimwengu kuhudumu serikalini!!!!
Lakini cha ajabu, mwisho wa hiyo post anaonesha kumbe povu lote alilomwaga ni kwa sababu tu anam-criticize JPM!!
Nimepekua pekua JF na kukutana na hii... sina shaka nawe ushapata kuiona:
View attachment 477017
Kwa mujibu wa alieambatanisha hiyo screenshot, hiyo ni habari ya 1993 na inaonekana kweli ni ya 1993 manake inazungumzia kujiuzuru kwake u-DC!!
Inawezekana 1993 ilionekana ni jambo lisilo la kweli lakini hivi sasa hata mtoto wa darasa la sita anafahamu CCM imejaa manyang'au!!!
Kauli kama hizo ndizo zinawafanya serikali, CCM na mawakala wao kumchukia Jenerali Ulimwengu!! Hata alipovuliwa uraia wake ilikuwa ni baada ya kuandika maovu ya serikali ya Mkapa! Ili kumnyamazisha; ndipo wakaja na hoja ya uraia lakini kwa bahati mzuri hajanyamaza wala haielekei kwamba atanyamaza!!!
Na kwamba Ulimwengu ni Mnyarwanda kwangu ni hoja isiyo na maana yoyote manake hata kama kweli angekuwa ni Mnyarandwa; basi ni bora niishi na Wanyarwanda 1000 wasio wezi kuliko kuishi na Mtanzania mmoja aliyejaa ulafi; wizi, fisadi na asiyetosheka!!!