Wasichana /Wanawake wenzangu

hahaahahahaha

mm mwenyewe natafuta mwenye tabia hzo tuyajenge lakin wap mpaka nasemaga i will marry when I want because beautiful once is not yet born
Kuoa skuizi imekuwa ni bahati nasibu, ukibugi umeumia, yani ni tofauti na zamani
 
Mbona ivo jamani.. Kuweni na imani nasisi basi hio dhana mlojijengea kichwani si nzuri kwa afya na ustawi wa mahusiano
Kwani uongo jamani? Kuwa tu mkweli usiidanganye nafsi yako. Kufuatia ongezeko la watu wasiojielewa basi probability ya kumpata mtu anayejielewa inapungua japo wapo.

Mfano wewe leo hii katika marafiki zako hao wa kike ulionao ungeambiwa uoneshe wanaofaa ili kaka yako aoe mmoja wao. Je ni wangapi ungewapendekeza ili kaka yako aishi naye kama mke ili afurahie maisha yake ya ndoa na nyie kama ndugu mfurahie jinsi kaka yenu anavyoishi na mke anayejielewa na mwenye upendo wa kweli?

Unaweza kumwona mtu anajielewa sana lakini ukimwambia samahani shida yangu natafuta rafiki wa kike/kiume anayejielewa kama wewe. Mtu huyo anaweza kukwambia subiri nifanye kwanza uchunguzi au akakwambia naweza kukuonesha halafu ukaja kunilaumu maana yake pamoja na kuwa yeye anajielewa lakini bado hata rafiki zake anaona bado hawajielewi kiasi cha kumwezesha yeye kutoa majibu ya moja kwa moja.

Ukitaka kuamini hili mtafute mtu mzima mwenye busara zake. Kaa naye mdadisi kuhusu maisha, mwombe akushauri namna maisha yanavyoendeshwa katika kipengele ambacho utaona kinafaa. Halafu mwisho mwambie yeye kama mzazi unajua amekua zamani na anazijua tabia za watu na pengine anaweza kumsoma mtu tabia zake na akaweza kuproject maisha yake atakavyokuja kuishi na familia yake na jamii nzima. Mwambie ninakakuomba unioneshe msichana au mvulana ambaye akiolewa/kuoa atakuwa ni mke/Mme mwenye kujua majukumu na wajibu wake kwa Mme/mke wake na familia kwa ujumla. Mzazi huyo atakwambia nipe mda niwachunguze kwanza maana yake hana jibu la moja kwa moja na pengine hata kama familia za rafiki zake kuna wavulana/wasichana wakubwa hatawataja hao moja kwa moja.

Kwa kifupi watu wasiojielewa wameongezeka sana kiasi cha kuwafanya watu wanaojielewa wapatikane kwa kupekua sana.

Kadiri unavyokuwa na sample nyingi na katika sample hizo kuna nzuri na mbovu na Kibaya zaidi sample mbovu zikawa nyingi kuzidi nzuri basi probability ya kupick sample nzuri hupungua.
 
Wanawake wenzangu!
Natamani sana sote humu tuwe wake wema kwa wame zetu au mahusiano yetu kiujumla. Hivo naomba kushea kitu hapa. Hii nimeona mahali nikabarikiwa nayo kuleta kwenu wapendwa.

BUSARA KWA WANAWAKE.

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubutu wako.

2. Mwanamke anaemuheshimu mumewe ni mwanamke bora ambae kila mwanaume angetamani kuwa nae.

3. Tabia yako na misimamo yako ndio itakayomfanya mumeo ajute au afurahie kukuoa wewe.

4. Kuwa mke bora inakubidi uwe vizuri katika maarifa ya kutawala hasira zako na sio kuwa mtu wa kulipiza visasi.

5. Kuwa kiongozi huko kazini kwako lakini kuwa mtu wa kunyenyekea nyumbani kwako kwa mumeo. Hiyo ni busara.

6. Usiweke mashindano na mumeo, mpe hongea na mtie moyo kwa kila hatua anayopiga katika maisha.

7. Kuwa na ubinadamu, sio kosa dogo tu mumeo amefanya ukatamani kulipiza kisasi. It won't help u!

8. Kuwa mkarimu, kila mwanaume anamuheshimu mwanamke mkarimu na mwenye msimamo.

9. Usijaribu kumpa adhabu mumeo ya kumnyima chakula cha usiku kitandani, hii itamlazimu kutafuta chakula nje ya ndoa.

10. Hakuna kitu kibaya kama utakubali kuwa ulikosea kama kweli ulikosea. Kuwa mrahisi kukubali kama kweli ulikosea. Na omba radhi pale inapobidi.

11. Jiandae kumsamehe mumeo pale anapokosea kwa maana mke atoae msamaha kwa mumewe ni mke mwema tofauti na yule aliejaa visasi.

12. Tengeneza maamuzi ya kuwa mke mwema, pasina kuwa na hofu yoyote na Mungu atakubariki.

13. La mwisho na la muhimu tambua kwamba mwanamke aliejaliwa umbo zuri na sura nzuri pasina maarifa kichwani anafaa kwa usiku mmoja, lakin yule mwenye maarifa na ufahamu yeya afaa kwa maisha yote!

Akhsanteni na weekend njema
Inawezekana umejificha kwenye story kumbe ww ni single mother's.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom