Wasichana /Wanawake wenzangu

Wasichana /Wanawake wenzangu

Nishaanza kupaniki,

Kuna mjinga karopoka hilo neno

""Eti kutafuta huyo mke zama hizi, ni sawa na kutafuta bikra kwenye wodi ya wazazi""

Yeye alichoshauri ni kwamba bora uoe tuu ukiwa hutarajii hayo mambo, kama ni silka yake hujikuta muhusika huyafanya yeye hata bila kujua.


Akasema yeyote anayeyafanya hayo kwa kujitambua hua tabia hiyo haidumu.

Na kibaya zaidi watakao muona ni majirani zako na hata wewe kwa kulewa na upendo utakaopewa, utajikuta ukihisi kuwa ni wajobu wake kukufanyia hivyo, hapa wanaune wanaobahatika kuwapata hawa hufikiri kuwa wanawake wooooote wako hivo na hujivunia uanaume zaidi kuliko kutimiza majukumu kama baba.
 
vipi kungwi ushaolewa au bado?! na kama bado je? upo tayari kuolewa na mimi? naomba jibu tafadhali
 
Ushauri mzuri kweli kweli,ila wewe mwenyewe unaufuatilia kweli?
Huu ushauri umewasaidia watu kwa asilimia ngapi?
Je wewe mwenyewe huu ushauri umekusaidia?

Nimeuliza hayo kwa sababu every action imposed to people has different responce.....
mkuu mi nadhan kushika neno n busara zaid no matter hyo mtu anae toa hilo neno n mzur/mchaf kias gan
 
Mleta maada kaitoa kwa ujumla wake bila ubaguzi wa kdini


1 wakorintho 7:14
"Kwa maana Yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe,na Yule mke asiye amini hutakaswa ktk mumewe,kama isingekuwa hivyo,watoto wenu wangekuwa si safi,Bali sasa ni watakatifu"
 
Wanawake wenzangu!
Natamani sana sote humu tuwe wake wema kwa wame zetu au mahusiano yetu kiujumla. Hivo naomba kushea kitu hapa. Hii nimeona mahali nikabarikiwa nayo kuleta kwenu wapendwa.

BUSARA KWA WANAWAKE.

1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubutu wako.

2. Mwanamke anaemuheshimu mumewe ni mwanamke bora ambae kila mwanaume angetamani kuwa nae.

3. Tabia yako na misimamo yako ndio itakayomfanya mumeo ajute au afurahie kukuoa wewe.

4. Kuwa mke bora inakubidi uwe vizuri katika maarifa ya kutawala hasira zako na sio kuwa mtu wa kulipiza visasi.

5. Kuwa kiongozi huko kazini kwako lakini kuwa mtu wa kunyenyekea nyumbani kwako kwa mumeo. Hiyo ni busara.

6. Usiweke mashindano na mumeo, mpe hongea na mtie moyo kwa kila hatua anayopiga katika maisha.

7. Kuwa na ubinadamu, sio kosa dogo tu mumeo amefanya ukatamani kulipiza kisasi. It won't help u!

8. Kuwa mkarimu, kila mwanaume anamuheshimu mwanamke mkarimu na mwenye msimamo.

9. Usijaribu kumpa adhabu mumeo ya kumnyima chakula cha usiku kitandani, hii itamlazimu kutafuta chakula nje ya ndoa.

10. Hakuna kitu kibaya kama utakubali kuwa ulikosea kama kweli ulikosea. Kuwa mrahisi kukubali kama kweli ulikosea. Na omba radhi pale inapobidi.

11. Jiandae kumsamehe mumeo pale anapokosea kwa maana mke atoae msamaha kwa mumewe ni mke mwema tofauti na yule aliejaa visasi.

12. Tengeneza maamuzi ya kuwa mke mwema, pasina kuwa na hofu yoyote na Mungu atakubariki.

13. La mwisho na la muhimu tambua kwamba mwanamke aliejaliwa umbo zuri na sura nzuri pasina maarifa kichwani anafaa kwa usiku mmoja, lakin yule mwenye maarifa na ufahamu yeya afaa kwa maisha yote!

Akhsanteni na weekend njema
NATAFUTAGA WA AINA HII . UMEOLEWA WEWE.......? NI- PM
 
Kwanza ni kile, nilikosea , ilipaswa iwe hivi,...
"""""' mwanaume huishi kulingana na matakwa ya mwanamke"""
Hii nadhani yenyewe utata wake umeisha.

Yaa wanaume tunachaguliwa namna ya kuishi na wanawake,
Mwanamke ndio hutoa malezi kwa mwanaume hasa katika kila nyanja.
Mathalani:-
Kuelewana/kutoelewana sana na majirani hutengenezwa na mwanamke, usafi au uchafu kwa ujumla hutegemea mwanamke, kipato kwa asilimia kubwa hutegemea mwanamke., nguvu na molari za kufanya kazi hutegemea mwanamke, furaha au huzuni nyumbani humtegemea sana mwanamke
N.k nyingi

Ukitaka mafanikio huwezi mkimbia mwanamke.
Mkuu naunga mkono hoja hasa kwa mifano uliyotolea!
Kwa upande mwingine mke ni kama mama maana anamchango mkubwa sana katika kuleta amani na furaha ya familia pamoja na ustawi kwa ujumla.

Mi kuna Senior mmoja kazini kwangu he is about 50 yeas old huwa nafurahia sana hata tu ile namna anavyomwita mke wake hata akiwa anaelezea incidence inayomhusu huwa hasemi sijui mama fulani au mke wangu badala yake huwa anasema mama. Mfano anaweza kusema " kuna siku nilikuwa naenda safari fulani nikiwa na mama ........" Hii inaonesha anampenda na anamkubali na kiukweli hata kimaendeleo yuko successful.

Huwa namwomba sana Mungu anioneshe yule ambaye tutaendana naye!
 
Aisee wapo, mfano mzuri ni mke wangu. Hivyo vigezo vyote anavyo na sifa zingine nzuri ambazo hakutaja. Maisha swafi kabisa.
Hongera sana mkuu!
Ni kweli bado wapo ila wamepungua sana na pengine wako hatarini kupotea kama mnyama faru japo wenyewe hawawindwi na majangiri!
 
Kwani wote wanaamini katika Mungu??
Na siku hizi dini zimejawa na wanafiki sana! Mtu kutwa kucha yuko kwa kusali lakini moyoni hana upendo kabisa! Dini ya kweli matendo ya mtu!
Na huwezi kujua imani ya mtu kwa Mungu ila wengi tunapima imani kwa frequency ya kuattend sehemu za ibada et ndio tunasema mtu yule mshika dini!
Kuna watu wengine akiona anatafuta kitu fulani anajifanya anashika sana dini hata miaka mitano inaweza kupita anajifanya mshika dini kumbe ana moja kichwani na wengi hapo watajidanya kuwa huyu mtu amemrudia Mungu kumbe anatumika kwa kutaka kuwapoteza walio na macho ya kibinadamu! Na akishapata kile alichokuwa anakitafuta utaanza kuona frequency ya kuattend na kushiriki shughuli za kiibada zinaanza kupungu.

Mwenyezi Mungu kwa kweli atusamehe maana watu wengi sana wanajivisha ngozi ya kondoo kumbe ndani mbwa mwitu!
 
Wapo wengi tu, sema wanaume wanaolalamika sana huwa wanakutana na wa kufanana nao, hapo ndipo tatizo linapoanzia.
Wanasahau kuwa unapewa wa kufanana nawe.
Sio kweli mkuu kuna watu wapole mpaka unamwonea huruma anavyohangaishwa na mke wake tena mke anajidai kabisa kwa kusema kuwa ameshamteka hawezi kufurukuta kumbe ni mtu kuwa mwelewa na uvumilivu tu.

Lakini pia ikumbukwe kuna watu wanajua kupretend pale anapokuwa anatafuta kuolewa anaweza kufanya pretending hata kwa miaka sita ila akishaingia kwenye himaya ndio anaonesha makucha! Kuna wengine wapole kwa sababu wako weak either economically au kitu fulani hana ila kadiri mnavyoendelea kuishi na kupata mafanikio ndio wanaanza kuonesha jeuri! Hujawahi kuwaona/kuwasikia hao?
 
Sio kweli mkuu kuna watu wapole mpaka unamwonea huruma anavyohangaishwa na mke wake tena mke anajidai kabisa kwa kusema kuwa ameshamteka hawezi kufurukuta kumbe ni mtu kuwa mwelewa na uvumilivu tu.

Lakini pia ikumbukwe kuna watu wanajua kupretend pale anapokuwa anatafuta kuolewa anaweza kufanya pretending hata kwa miaka sita ila akishaingia kwenye himaya ndio anaonesha makucha! Kuna wengine wapole kwa sababu wako weak either economically au kitu fulani hana ila kadiri mnavyoendelea kuishi na kupata mafanikio ndio wanaanza kuonesha jeuri! Hujawahi kuwaona/kuwasikia hao?
Bado tu huoni udhaifu wa huyo mwanaume ulomdescribe katika maelezo yako!!!
 
Back
Top Bottom