Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Status
Not open for further replies.
Unachozungumza ni kweli, kwani si vyema kuikashfu imani ya mwingine lakini kuna swala linalonitatiza kwa walokole.
Ni kwamba kuingiwa na roho wakati wa maombi ni kitu ambacho kimezungumziwa katika Biblia takatifu, na nachojua Mimi katika nyakati zile mtu alieingiwa na roho na kuanza kunena, alinena maneno yenye kueleweka hata kama lugha alioizungumza hakuwa akiifahamu kabla, wanaoijua walimwelewa.
Hili lilifanyika sana wakati watumishi walipokuwa wakihubiri katika jamii ngeni na walihubiri kwa lugha za wenyeji bila wakalimani wala kujifunza, sasa tatizo linalonisumbua mimi ni kuwa wengi wa walokole niliowaona huwa maneno yanayowatoka huwa siyaelewi na hakuna anaelewa wanazungumza lugha ipi.
Mimi si Mlokole ama msabato, naomba tu msaada wa ufafanuzi juu ya hili.
 
Ha ha ha ha ha ha ha ha.....

Bwana tido,
nakushauri ufuate sabato ya muumba wako kwa kuwa anakupenda na kukujali ndo maana upo mpaka mida hii na ndio agano lake na ni la milele na sabato itaadhimishwa hadi huko mbinguni..isaya 66:22-23.
Balikiwa sabato ijayo tukutane church..
 
Unachozungumza ni kweli, kwani si vyema kuikashfu imani ya mwingine lakini kuna swala linalonitatiza kwa walokole.
Ni kwamba kuingiwa na roho wakati wa maombi ni kitu ambacho kimezungumziwa katika Biblia takatifu, na nachojua Mimi katika nyakati zile mtu alieingiwa na roho na kuanza kunena, alinena maneno yenye kueleweka hata kama lugha alioizungumza hakuwa akiifahamu kabla, wanaoijua walimwelewa.
Hili lilifanyika sana wakati watumishi walipokuwa wakihubiri katika jamii ngeni na walihubiri kwa lugha za wenyeji bila wakalimani wala kujifunza, sasa tatizo linalonisumbua mimi ni kuwa wengi wa walokole niliowaona huwa maneno yanayowatoka huwa siyaelewi na hakuna anaelewa wanazungumza lugha ipi.
Mimi si Mlokole ama msabato, naomba tu msaada wa ufafanuzi juu ya hili.


Mimi ntakujibu swala moja! Hilo la kunena kwa lugha ningeomba walokole waje hapa walitetee kimaandiko!

Nataka nikujibu swala la Wewe unayoiita kashfa! Kwanza kashfa ni nini? Au ni pale ninapokufunulia KWELI then Wewe ndio useme kashfa? Au kashfa ni lugha mbaya za matusi dhihaka juu ya Imani ya mwenzako? Na Je wasabato wanafanya dhihaka na kutukana Imani za wengine? Au wanasema KWELI YA MUNGU?
 
Wasabato wanawachukia wote ambao sio wasabato, na wanaamini kuwa wakristo wengine hawataweza kwenda mbinguni isipokuwa wasabato.

oooh! Renegade na Kaunga, wasabato hawachukii watu wa imani nyingine ila wanasoma na kuelekeza kwa mujibu wa biblia. Hebu angalia ujumbe huu katika biblia, si hata romani wanatumia biblia jamani na walokole? sasa fungu hili mnalisemaje wapendwa?hivi hii ni chuki kweli?? tusome pamoja hapa.....

Isaya 56:1....... "Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatende haki;kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikae sana; azishikaye sabato asizivunje,......" soma na tafakari hiyo Isaya 56 yote utaelewa! Karibuni kumtukuza Mungu wa kweli wala hapana chuki hapa, tunaeleweshana tu!
 
oooh! Renegade na Kaunga, wasabato hawachukii watu wa imani nyingine ila wanasoma na kuelekeza kwa mujibu wa biblia. Hebu angalia ujumbe huu katika biblia, si hata romani wanatumia biblia jamani na walokole? sasa fungu hili mnalisemaje wapendwa?hivi hii ni chuki kweli?? tusome pamoja hapa.....

Isaya 56:1....... "Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatende haki;kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikae sana; azishikaye sabato asizivunje,......" soma na tafakari hiyo Isaya 56 yote utaelewa! Karibuni kumtukuza Mungu wa kweli wala hapana chuki hapa, tunaeleweshana tu!


Mkuu Blueband au Siagi

Ebu niongezee hapo Kidogo tu andiko jingine ambalo makanisa mengine wanataka Kua wakristo au waitwe wakristo kwa jina lake Lkn wasifate mafundisho ya Mungu!

Isaiah 4:1

And in that day seven women shall take hold of one man, saying, We will eat our own food and wear our own apparel; only let us be called by your name, to take away our reproach
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Blueband au Siagi

Ebu niongezee hapo Kidogo tu andiko jingine ambalo makanisa mengine wanataka Kua wakristo au waitwe wakristo kwa jina lake Lkn wasifate mafundisho ya Mungu!

Isaiah 4:1

And in that day seven women shall take hold of one man, saying, We will eat our own food and wear our own apparel; only let us be called by your name, to take away our reproach

super!! asomaye na aelewe!
 
Hii mada kuna jukwaa lake ingependeza sana kama ingewekwa kule
 
Wasabato wanawachukia wote ambao sio wasabato, na wanaamini kuwa wakristo wengine hawataweza kwenda mbinguni isipokuwa wasabato.

Mkuu hao wanaochukia wengine sio Waadventista Wasabato bali ni mfano..

Biblia inasema "Na kondoo wengine si wa zizi hili, nao watakapo isikia sauti yangu wataungana na wa zizi hili"

Sasa huyo anayewachukia wengine sio....
 
Wasabato ni genge la wahuni,wana mambo kama ya kiislam,eti elen g white ndie nabii wa mwisho kama mtume alivyo wa mwisho. Kwao mtu yeyote anaeitwa nabii baada ya white ni wa uongo, hawasomi biblia,wanasoma vitabu vya nabii white aliyewahi kusema watu weusi ni zao la shetani.

Wafuasi wa elen g white na wafuasi wa mtume wote akili yao ni moja.
 
asante ndugu ningefurahi zaid kama ungenisaidia jibu kwanza la swali langu

Sorry Ameline netwk inanisumbua sana kufungua ninapoquote mtu; then here we go!!

Wasabato hawajisumbui na pete za ndoa kwa sababu hazina andiko lolote katika biblia. Mambo yanayofanyika pale katika ufungishaji wa ndoa yanafanyika kwa msingi wa maandiko. So usijetegemea kumsikia Mchungaji wa Kisabato anaitisha kuvishana pete pale madhabahuni maana hazina maana yoyote katika msingi wa ndoa takatifu! Fika pale kanisani ujifunze zaidi kila Sabato. Kuna vipindi vizuri vya kuuliza maswali ya namna hii kila Sabato kuanzia saa 4.00 hadi 4:45 na majibu yanatolewa pale!
 
Ndugu zangu wasabato.Msijenge imani yetu tu kwenye muujiza wa kufasiri.1korintho,14;2 iinasema hivi.maana yeye anaenaye kwa lugha hasemi watu bali na Mungu maana hakuna asikiaye.but anena mambo ya siri ktk roho yake.Marko 16:17 inaelekeza ishara za mtu aliyeokoka na kunena kwa lugha mpya.Nilisha waambia wasabato hawawezi kuyajua haya maana hawana Roho Mtakatifu ambae ni mwalimu wa maandiko.Rejeeni.yani ninyi akikosekana wa kutafsiri ni Roho chafu. Tubuni maana mnamkufuru Roho mtakatifu.
 
Naona watu wanaelewa. Mnakaribishwa kutembelea makanisa ya SDA popote pale ulipo, kwa walio Dar waweza sikiliza Morning Star 105.3 kuna mafundisho mazuri sana na sabato nyingine huwa wanarusha moja kwa moja mahubiri kutoka makanisa tofauti tofauti.
Bwana anawapenda na anapenda kila mmoja afike Mbinguni, uchaguzi ni wako
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom