dada usishangae, hata siku ile ya pentecost pale yerusalemu wanafunzi wa Yesu waliposhukiwa na Roho Mtakatifu wakawa na ndimi kama ndimi za moto ukiwakalia juu ya kila mmoja, wanayerusalemu walisema "watu hawa wamelewa mvinyo asubuhi hiii", walikuwa wanashangaa kama wanavyoshangaa wasabato.
kumbuka yafuatayo, imeandikwa kwamba, "lakini awaye yote asiye na huyo Roho wa Kristo, huyo si wake" ikiwa na maana kwamba hata ukiwa mkristo kama hauna Roho Mtakatifu moyoni mwako wewe si wa kristo.
Yesu atakapokuja kunyakua kanisa lake akiwa mawinguni ni wale tu wenye Roho Mtakatifu ndio watakaonyakuliwa. Roho Mtakatifu ni Mungu mwenyewe kama hauna huyo Roho moyoni mwako ni kwamba Mungu hayupo moyoni mwako. kuwa mkristo ni challenge kubwa sana ambayo mtu inabidi ajikane mwenyewe na atoe garama ya kuyakataa mambo mengi ya dunia ili ayapate ya rohoni kwasababu kuwa wakristo wengi sana ambao hawana Mungu katika maisha yao.
ukiwa na Roho Mtakatifu, atakusaidia kuomba, unajua hautakiwi kuomba kwa akili tu muda wote, kuna wakati maombi ya akili hayafiki mbinguni kwasababu kuna wakuu wa giza na wakuu wa anga huwa wanazuia maombi wakati mwingine kama maombi hayo hayana moto. kasome kitabu cha Daniel utagundua daniel alipokua akiomba siku 21 malaika alishuka kuja kumletea majibu akasema alishajibiwa sasa alicheleweshwa na mkuu wa anga la uajemi hadi alipopata msaada wa malaika mwingine kumshambulia huyo malaika wa giza/mkuu wa anga la uajemi.
maombi ambayo hayana moto wa Roho Mtakatifu yana asilimia ndogo sana kufika kwa Mungu. ila maombi yenye upako wa Roho ndiyo yana asilimia mia kuwa yamefika kwa Mungu na hakuna pepo wa kukaa angani kuyazuia. kumbuka kuwa, Roho mtakatifu hutuombea kwa Baba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa, pale anapolia aba, hivyo kama hauna Roho hauna mwombezi. maombi ya Roho Mtakatifu/ukijawa Roho na kunena kwa lugha ndio maombi pekee ambayo Roho Mtakatifu anakuombea kwa mapenzi ya Mungu kwani tukiomba kwa akili tutaomba kwa upumbavu wa kidunia tu kuomba magari kuomba vyakula kuomba vitu ambavyo si vya faida, ila Roho akiomba anaomba vyooote kwa pamoja na hata mambo ambayo Mungu ameyaona yako mbele yako na atakuombea kukuokoa au kukubariki n.k. na Neno la Mungu limeandikwa kwamba '' na ishara hizi zitaambatana na wote watakaoamini, kwa Jina langu watatoa pepo, ....watasema kwa lugha mpya....", that means, ukiamini unatakiwa kusema kwa lugha mpya, na huo ndio ukristo. HAUTAJUA MAMBO HAYA KAMA HAYAJAKUPATA, ILA WALE WENYE NEEMA AMBAO WALISHAYAPATA WANAJUA KUWA ROHO HUA ANAWAFUNULIA HAYA MAMBO HALAFU UNAKUWA HUNA HATA MASWALI YA KUJIULIZA MAJIBU YOTE UNAYAPATA KWA SAUTI YA UKIMYA ROHONI MWAKO AU KWA NJIA MBALIMBALI AMBAZO MUNGU HUONGEA NA WANADAMU. Mungu akubariki sana ndugu.