Ntuzu
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 17,418
- 10,877
Kuhusu sabato tusome kutoka12;16, Matendo 20;7 Mungu aliagiza kupumzika siku ya kwanza juma na siku ya saba ya juma ambazo ni jumapili na jumamosi. Na Paulo alimega mkate na kuhutubu siku ya kwanza ya juma, maana yake walifanya ibada siku ya jumapili. Kuthibitisha siku ya kwanza ya juma soma Marko16;1-2 baada ya sabato kupita siku ya kwanza ya juma ndiyo siku aliyofufuka Yesu Kristu. Sasa wasabato wana ushirika na yule mpinga Kristu? Kwa sababu wanadai tunaoabudu j'pili tunabadili majira na nyakati,tena wakrisu wenzao wakati Mungu ameagiza kupumzika j'mosi na j'pili,na mitume waliabudu j'pili inakuwaje wakati kuna jamii ambayo haiabudu j'pili wala j'mosi hawaisemi ila wakristu wenzao wanaofuata maandiko? Tunajua shetani adui yake mkubwa ni kanisa je ameshapata sehemu ya kushambulia kanisa? Wasabato mnanitisha
Mkuu Naona unaongea vitu via ajabu tu tena bila maandiko!
Mungu ametuagiza kupumzika Siku ya Saba na ni sabato Yake! Wapi Ktk maandiko tumeagizwa kupumzika Siku ya kwanza ya Juma?