Ukiangalia Agano la kale hata Waislam wanazungumzia yaliyomo, ukiona jinsi msisitizo wa ufuataji wa sheria ulivyo kwa Waislam hata Wasabato ni hivyo hivyo, wasabato si wakristo! kama watasema wanamkiri kristo hata Waislam wanamkubali (Nabii Issa). Acha kuvutiwa na upande mwingine, wala usisikilize maongezi yao kwa kuwa ni shetani. Yesu aliahidi kuleta msaidizi hakuahidi kutukuza Sabato kwa kuwa alijua ukiongozwa na roho mtakatifu umewekwa huru kwelikweli wala hufungwi na sheria utakuwa mtenda mema na mcha MUNGU si wa unafiki bali wa kweli. Siku imewekwa na wanandamu kuitwa jumamosi au jumapili lakini roho mtakatifu imewekwa na MUNGU mwenyewe kupitia ahadi ya YESU KRISTO mfufuka. Waache wadanganyane kwa kufuata maneno ya aliyeingiwa na pepo Ellen G. White. MUNGU akufungue macho ya Rohoni uweze kutambua ukweli wake.