MT KILIMANJARO
JF-Expert Member
- Apr 19, 2013
- 4,215
- 761
Mleta mada, nimesoma bandiko lako lkn sikumaliza, uneishia kumtuhumu Warioba kama CCM wanavyofanya. Umeshindwa kujenga hoja, mbaya zaidi, umeshindwa kujibu hoja za Warioba hata moja! Warioba, ameshajibu hoja zenu zote, na akauliza maswali saba ambayo si Jk, Pinda, Shein, wala Dk Migiro na wajumbe wote wa BLMK ambaye amejibu hata swali lake moja.
Tangu lini mwana ccm akawa na uwezo wakujenga hoja? Hao ni vichwa panzi wamekaririshwa na mwenyekiti wao. Kuanzia Lumumba mpaka kule chamwino dodoma hakuna mwenye akili na uwezo wakujibu yale maswali7 ya warioba.