Warioba Anataka Nini Hasa?

Warioba Anataka Nini Hasa?

Warioba amesema "eti mwalimu akirudi ghafla akakuta maraisi wawili wanapigiwa mizinga 21 angeshangaa sana" Huyu mzee ni bure kabisa mizinga hata maiti ya mwanajeshi inapigiwa sasa hapo mizinga ina thamani gani mpaka ikawa ni hoja?

Mizinga ni kwa wanajeshi hata akiwa maiti. kikwete ni Amiri Jeshi. Shein anapigiwa mizinga kama nani?
 
Tume ya Warioba ni tume ya tatu. Tume ya kwanza ilitoa mapendekezo ya wananchi kuwa ni serikali tatu, Chama tukakataa, tukaunda tume ya Pili, nayo pia ikaja na maoni yaleyale ya serikali tatu, chama tukasema HAPANA. tumeunda tume ya tatu, nayo pia inasema maoni ya wananchi ni serikali tatu. Chama hatuwezi kukubali kwa kuwa hawakusema tunachotaka. Katiba hii ni ya chama au ya wananchi?

Maoni ya LUKUVI, WASIRA, na kiongozi wao J M K
 
Kwa mbumbumbu asiyependa kujibidisha, hata kichaka kidogo kwake ni msitu...wake up dude, ungali mdogo bado!
 
Warioba eti anasema "wasizungumzie takwimu au gharama watafute majibu ya hoja na maswali"
hivi kweli kuchakachua takwimu siyo hoja? au gharama siyo hoja? Warioba amejidhalilisha kweli.

basi zungumzieni kero zilizoainishwa za wazanzibar na watanganyika ni kueleza mtazitatua vipi na lini zitakuwa zimetatulika.
 
maneno yasemwayo na waunguja kuwa hata umtendee wema mpemba kiasi gani hana shukrani.
Kwa hiyo warioba aache polojo zake waunguja ambao ni wengi na ambao asili yao ni bara wanataka muundo huu uendelee ila uboreshwe tu bado wanawataka ndugu zao wa bara hao wapemba kwanza wengi wao walishaukana uafrka na wanajiconsider wao ni waarabu ndo wanaotaka kujitenga wajiunge na nchi za kiarabu kwa hiyo warioba dont be pawn in a chess game which you dont even know father.
Kikubwa kabisa wewe ni mbaguzi. Na utakuwa umeona jinsi wabaguzi wanavyoadhibiwa Ulaya (mfano kwenye michezo).
Hivi Jaji Warioba ndiye aliifanya Zanzibar iwe na kiti UN?
Unavyosema 'undugu', kwana Watanzania hawana ndugu Msumbiji, Malawi, Zambia, Congo, Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya na kwingineko ...mbona hatutaki kuungana na hawa na kufanya serikali mbili!????
Nimemsikia Mh. Zitto BBC (japo simwamini sana) lakini anasema Watanzania hatuna utamaduni wa kufikiri zaidi ya tunachokiona na hata wale wanaoweza kufikiri japo kidogo hawajui (hawana utamaduni) wa kujadiliana. Matokeo yake tunaishia kuleta mambo ya kibaguzi kama haya.
Dunia ni moja na binadamu tutaendelea kuwa wamoja bali kwa hiari na sio kwa mkono wa chuma na kulazimishana. Omba miaka 200 ijayo ikukute hai alafu uone kama hii mipaka ya nchi za leo itakuwa hivi (refer EU kwa sasa).

 
Huu ni uwongo Ilala ni kifupi cha la ila ilala wa wasiojua wakapaita ilala lakini ni kifupisho cha neno lefu na ilimaanisha zamani maeneo ya boma kuja mpaka karibu na buguruni ni sehemu iliyokuwa makazi ya waarabu na wasomali na waswahili.

Malawi pia wanayo Ilala kwa taarifa yako,Inabidi urudi darasani ukajifunze historia ya lugha ya kiswahili na lugha ya kibantu kwani nina uhakika hujasoma hayo mambo ukisoma nahisi utachanganyikiwa sana.Nilikuwa nchi flani ya kusini mwa Afrika,Nilikuwa nime-chill somewhere na wadada flani wa nchi hiyo katika mazungumzo yao yaliyotawaliwa na lugha ya asili ya kabila lao (Ovambo) nikasikia wakitamka neno m-a-s-a-b-u-r-i nikashtuka sana,nikajikuta nacheka na kuyaingilia mazungumzo yao,nikawauliza tena.."come again,did you say m.a.s.a.b.u.r.i?" wakasema ndiyo kwa kujiamini wakidhani sikuelewa maana ya lile neno.Nikawaambia hilo neno kwa maana ya kiingereza wakashangaa sana then nikaja kuelewa kuwa kumbe maneno ya kibantu yapo mengi sana na yanatumika katika mawasiliano yetu ya kila siku sehemu mbalimbali za Afrika.Wazambia na Wamalawi wanaoongea lugha ya kilozi unaweza ukawaelewa vizuri kutokana na maneno yaliyomo kwenye lugha hiyo pia kutumika kwenye ya kiswahili.Soma sana historia mbalimbali ili upanue ufahamu wako mzee.
 
Nyie watoto wa cccccmaf ambao mmeandaliwa kurithi madaraka ya nchi ya Tanzania tulieni dawa iwaingie. Maana Warioba sasa anawaingizia dawa, Tulieni tu katika TANGANYIKA hamtarithi madaraka.
 
Warioba na wajumbe wenzake wa tume wameleta maoni na mapendekezo ya wananchi. Aliyewatuma ni rais. Acha kupiga porojo wenzako wamefanya utafiti kisayansi. Hao waunguja ulikutana nao wapi na unatakwimu zozote kuthibitisha hilo?

Warioba alisema kwamba mwaka 90 ilipigwa kura ya maoni kuhusu mfumo wa vyama vingi 80% yao wote walitaka chama kimoja lakini 20% waitaka vyama vingi tu lakini wakachukua maoni ya 20% wakasema sababu walikuwa wanajua kinachoendelea,pia warioba huyo huyo anasema kuwa tume ya jaji nyalali na kisanga ilipendekeza mfumo wa serkali 3,kwa hivyo kama wao walipendekeza hoja ya serkali 3 kuna haja gani yeye akipendekeza tena hoja hiyo na kuacha maoni ya waliowengi ambao ni 60% kama mwaka 89 kwenye maoni ya vyama vingi na kuacha 80% waliotaka chama kimoja??
Sasa basi kama ni hivyo angalieni huyu mzee anavyojichanganya sana takwimu siku zote zina-change kila wakati mfano wakati obama anaingia madarakani 80% alikuwa na approve rate ya 80% ya wamarekani na 90% ya dunia nzima lakini miaka 2 baadae approve rate yake ikaporomoka kufikia hadi 46%!! WHY? Sababu people opinion always fluctuate according to governing trend of leader.sasa mwaka 89 wakati watanzania walipotoa maoni ya 80% ni kweli wengi walikuwa hawakusoma wala hawakujua faida za vyama vingi lakini sasa hivi uchukue mawazo ya watu 13% ukapandikize kwa mawazo ya watu almost 70% nani ambaye hajasoma sasa hivi??au ni nani ambaye hajui kile anachokipendekeza sasa hivi??
Pili warioba anasema kuwa kwa kuwa jaji kisanga na nyalali walipendekeza serkali 3 kwani yeye kuna ubaya gani akipendekeza hivyo kama wao ingawaje 70% kwenye maoni wameonyesha wanataka muundo wa sasa ueendelee??
sasa kama ni hivyo kweli kumbe yeye alishakuwa na wazo lake la jaji nyalali na kisanga sasa mbona alisumbuka sana kwenda nchi nzima wakati angependekeza tu pale pale bwana mh.rais mi napendekeza serkali 3 ka majaji wenzangu waliopita pili hajui kuwa opinion change according to time kama watanzania mwaka 92 walitaka serkali 3 haiwezekani wazo hilo liendelee kuwa hivyo miaka yote ni uwongo watu sasa hivi wamesoma na wanajua walichopendekeza asitake kuwacrash na kuweka mawazo yake huo ni udikteta,almost 70% wametaka muundo wa sasa uendelee sasa kwa nini wasisikilizwe??
 
Malawi pia wanayo Ilala kwa taarifa yako,Inabidi urudi darasani ukajifunze historia ya lugha ya kiswahili na lugha ya kibantu kwani nina uhakika hujasoma hayo mambo ukisoma nahisi utachanganyikiwa sana.Nilikuwa nchi flani ya kusini mwa Afrika,Nilikuwa nime-chill somewhere na wadada flani wa nchi hiyo katika mazungumzo yao yaliyotawaliwa na lugha ya asili ya kabila lao (Ovambo) nikasikia wakitamka neno m-a-s-a-b-u-r-i nikashtuka sana,nikajikuta nacheka na kuyaingilia mazungumzo yao,nikawauliza tena.."come again,did you say m.a.s.a.b.u.r.i?" wakasema ndiyo kwa kujiamini wakidhani sikuelewa maana ya lile neno.Nikawaambia hilo neno kwa maana ya kiingereza wakashangaa sana then nikaja kuelewa kuwa kumbe maneno ya kibantu yapo mengi sana na yanatumika katika mawasiliano yetu ya kila siku sehemu mbalimbali za Afrika.Wazambia na Wamalawi wanaoongea lugha ya kilozi unaweza ukawaelewa vizuri kutokana na maneno yaliyomo kwenye lugha hiyo pia kutumika kwenye ya kiswahili.Soma sana historia mbalimbali ili upanue ufahamu wako mzee.

Unanifundisha mimi tena??we ndo urudi darasani hapo ilala hakuna hata mmalawi au mnyasa mmoja sasa unalazimisha nini kufanana kwa neno siyo lazima iwe ndo asili yake.Neno ilala ni kifupi cha neno la ila ila Allah na lilikuwa kwenye bango kipindi hicho na ndo asili ya neno ilala kama kifupisho hayo ya malawa yametokea wapi mbona hakuna mnyasa hata mmoja ilala kwenyewe zaidi ya waarabu na waswahili kwani wazungu walilitenga eneo hilo liwe makazi ya waarabu na wasomali.sasa unabisha nini??
 
Tatizo lako we kijana unadhani wanaotaka Tanganyika ni CHADEMA peke yao, mimi sina kadi ya chma nachokitaka ni Tanganyika yetu, wewe endelea kupewa hivyo viposho kwakuwa unataka kula bila kutoka jasho lakini kaa ukijua kama Zanzibar haitaki kupoteza identity yake, haiwezekani Tanganyika ipotee.
Nakupa angalizo mimi siyo siyo mtu wa umri wako, nimekuwepo tangu Miaka ya azimio la ARusha hivyo tumeiona hii nchi toka enzi hizo hadi leo. Mzadiki mkubwa wewe.


Ni wewe ndo unayeutaka utanganyika siyo sisi wote mtoto soma ndo mana ukaambiwa msome msisubiri kina tundu lissu wawasomee matokeo yake ndo haya sasa kila wanachokisema mnaona ni kweli tu kama wao miungu,unaongea maneno hayo sembuse hata miaka 38 hujafikisha halafu unang'aka ooh naitaka tanganyika we uliiona hiyo tanganyika?? je kama tanganyika ni jini je likija likakumeza we utajuaje? ndo mana mkaambiwa msome vijana sio polojo tu kisa dr.slaa kasema mkipingwa kidogo mnasema oo huyu katumwa oo huyu CCM!! katumwa gani basi nyinyi ndo madikteta wakubwa mana mtu akiwapinga kidogo tu kwenye mtazamo mnamwita mamluki mnataka kila m2 na kila mwanachama wa chadema afikirie kama kile anachofikiria dr.slaa na tundu lissu sasa kama ni hivyo mungu alikuumba na ubongo wa kazi gani wewe dogo??
fikiri kabla hujaongea zito kaja na hoja za uzalendo kawasifu ccm pale wanapopatia mnasema kibaraka!! mbona marekani leo hii kuna republican wengi tu walimwunga mkono obama kwenye obamacare na walimpigia kura kwenye congress?? sasa na wale ni wasaliti?? huo ndio maana ya uzalendo kwa nchi yako dogo sio unakurupuka tu ukadhani wote tuko sawa wenzako tunafikiri na kuumiza kichwa kabla hatujaandika!! umeshaambiwa wanaoshabikia kuvunjwa muungano wote ndo hao hao wanaotaka serkali 3 pia znzbr haina mapato mengi kuweza kutoa kama tsh.bilioni 5 kwa serkali ya muungano ila bara uwezo tunao sasa serkali ya znzb ikishindwa kupeleka fungu lake kwa serkali ya muungano miaka mi 4 tu muungano haujafa huo?? tumia akili zako dogo.
 
Hata lingekuwa jina la Kiyao au Kimakonde na hata Kibende au Kinyambo wala Kipare, Kidigo nk, jadili facts usiwe mawazo mgando wenzenu mlionao hapo Lumumba(Wazanzibar) wanawacheka sana mnavyoikana nchi yenu, mbona wao waliungana huko visiwani na kutengeza katiba ambayo leo inautingisha MUUNNGANO, watu kama wewe nadhani wanatumia 0655 kufikiria.
Utanganyika utakupatia tonge? Tanganyika ni jina tu kwa taarifa yako Tanganyika ni jina la kimanyema na wamanyema asili yao Congo kwa hiyo Tanganyika ni jina la Kikongo ndiyo maana kule Kigoma waliongoza kwa kudai Serikali tatu
 
Tatizo lako we kijana unadhani wanaotaka Tanganyika ni CHADEMA peke yao, mimi sina kadi ya chma nachokitaka ni Tanganyika yetu, wewe endelea kupewa hivyo viposho kwakuwa unataka kula bila kutoka jasho lakini kaa ukijua kama Zanzibar haitaki kupoteza identity yake, haiwezekani Tanganyika ipotee.
Nakupa angalizo mimi siyo siyo mtu wa umri wako, nimekuwepo tangu Miaka ya azimio la ARusha hivyo tumeiona hii nchi toka enzi hizo hadi leo. Mzadiki mkubwa wewe.


inavyoonekana wewe ni wazi ulikimbia umande wewe,kwanza sidhani una umri huo unaojisifia haa kutokana tu na maandisi yako we hata ukitaka kujiita kibibi kizee mi sina shida na wewe,tatizo zamani hata kufika form 6 ilikuwa ishu bila shaka we uliishia form 4 nawe leo unajiita msomi,kama kweli ni hivyo wasomi wamekwisha.
 
Hii thread yangu ilikuwa nzuri hawajamaa washaniharibia kuichanganya sijui na kitu gani kwa ma-mods tatizo ni nini? Space?? Si mnunue vyombo zaidi kuliko kumvurugia mtu thread yake. Tchaoo.
 
Utanganyika utakupatia tonge? Tanganyika ni jina tu kwa taarifa yako Tanganyika ni jina la kimanyema na wamanyema asili yao Congo kwa hiyo Tanganyika ni jina la Kikongo ndiyo maana kule Kigoma waliongoza kwa kudai Serikali tatu

Kada wa CCM aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Katiba, ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa kuchoshwa na matusi ya wana-CCM asema:

"...Tuna taarifa nyingi kwenye tume na ushahidi wa kutosha, maoni ya Rais wa Zanzibar, Ofisi ya Waziri Mkuu na Baraza la Mawaziri yalikuwa ya serikali tatu..."

Chanzo:

TANZANIA DAIMA, April 30, 2014 (leo), pg. 02, column 05, paragraph 03
 
Ndiyo maana hata serikali ilimshinda wakati akiwa waziri mkuu mpaka akajiudhuru wadhifa wake ni miongoni mwa watu wa hovyo kabisa wanaopenda kulazimisha mambo hata kama hayana maana yapite.

Kwa taarifa yako,Warioba hakujiuzulu uwaziri mkuu,bali muhula wa kwanza wa Mzee ruksa ulipomalizika na kuitishwa uchaguzi mkuu mwaka 1990-1995,Rais Mwinyi,alipotangaza baraza lake la mawaziri awamu ya pili na ya mwisho ,ya utawala wake jina la Warioba halikuwepo.
 
W. J. Malecela wewe uache unafiki kwani mtanzania haruhusiwi kusema kile anachokiamini, nyie bungeni mmemsema yeye,pale anawajibu kama mwananchi mwingine.
 
Wakubwa tatizo la mtu mjinga ni kujadili watu badala ya issues. Tunawezaona aina ya mtu aliyeleta huu uzi na hoja aliyojenga, isivyo na mashiko.
 
Lemutuz unatudharirisha watoto wote wa nje ya ndoa au haramu kuwa uwezo wetu kiakili ni mdogo na hatuwezi kufanya lolote la maana kama wewe. Jambo ambalo ni tofauti sana ndugu yangu. wapo watoto haramu ni majembe na tegemeo kwa familia. Hebu ruhusu kutumia akili yako wewe si mtu wa kujaribu kumbeza Warioba kakuzidi uadilifu kwa mbali kuanzia wewe mpaka baba yako mzee Jumanne!
 
Huyu Mzee hana hatia hata kidogo,alichoongea kina ukweli ndani yake.Niliwahi kusoma humu JF hansard ya Bunge la wawakilishi ambao walikuwa wamepigia kura sheria ya Watanzania Bara wakienda kufanya kazi Zanzibar lazima wafuate sheria na masharti kama wageni wanaoenda kufanya kazi huko.

Najiuliza hivi wakati wanapiga kura na wajumbe wa CCM walikuwepo na sheria hiyo ilishindwa kupita kwa kura moja au mbili,leo najiuliza aliyepigia kura sheria hiyo na Mzee Warioba nani asiyeitakia mema nchi yetu?

Hivi aliyevunja Katiba ya nchi yake na aliyesema ukweli kuhusu hilo nani anayeitakia mabaya Tanzania?Tusikwepe ukweli tukadhani bado tupo miaka ya 60,kwa sasa kila kitu kinatafutwa,vijana wa sasa siyo wale wakudanganyika anatafiti na kutaka kujua zaidi na zaidi.

Nafuu matusi kwa Mzee huyu sasa yangekwisha maana vijana wa leo watatafiti hata mkilazimisha serikali mbili bila marithiano suala hili baada ya miaka miwili litarudi tena.Wazee wanasema nafuu nusu shari kuliko shari kamili.Wanasiasa msitupotezee vijisent vyetu kwa ujinga mnaofanya hapa Dodoma,inatosha aibu mliotuletea kama taifa.

Hebu fikiria ni wangapi walikuwa wanaangali ile Ze-Comedy ya Dodoma pale Mjengoni,na nchi ngapi zilikuwa zinafuatiliwa na ukiangali kwa wakakti huu hata paka wa mzungu anajitahidi kujua kiswahili.
 
Back
Top Bottom