Warembo wananikataa, sijajua nakosea wapi I'm really stressed up

Warembo wananikataa, sijajua nakosea wapi I'm really stressed up

Sasa kama mtu ana hela,then anashindwa kumiliki watoto wazuri,sijui asaidiweje huyu ndugu yetu!
Inabidi wapatikane wadada wa mujini wamsaidie kutumia hela!!
Atakua ni MTU anaeboa pia akikaa na warembo. MTU haenjoy uwepo wake hata Kama hela IPO. Anakaa na MTU hata kumchekesha hawezi
 
Pole sana...

Umetaja sifa zako nzuri tu, weka na mapungufu yako pia... hayo ndiyo yatakua yanawakera wanawake...


Cc: mahondaw
 
Hbr JF,

Naombeni msaada wenu wa mawazo. Kwa zaidi ya miaka sita sasa nimeshindwa kupata relationship inayoeleweka, nyingi zinakufa hata kabla hazijaanza. Relationship yangu ya kwanza ilikufa kwa kua gf alitaka ndoa na mie ndio nilikua nimetoka chuo sina mbele wala nyuma akaamua tuachane. Baadhi ya wadada ambao niliwasihi sana waniambie kwa nini wanahisi hawawezi kua na mimi wameishia kusema "I'm too good to them", "I 'm too kind" wanaogopa kuniharibia....hivo. etc

My last attempt ilikua weekend iliyopita, nilitoswa baada ya kufukuzia kwa muda mrefu sana. Yaani naambiwa tu kama ni urafiki wa kawaida it's ok ila sio mahusiano na mdada ambae anakiri kua hana mtu na tumekua marafiki kwa miezi zaidi ya 6. Katika urafiki wetu huo nimejitahidi kua karibu nae, zawadi zawadi hata outings kwa sana tu hadi najiuliza nifanye nini zaidi na hawa viumbe.

Binafsi sio mbahili na pesa sio tatizo sana namshukuru Mungu kwa hilo, ila pia kutokana na shughuli zangu nakua busy mno kwa hiyo inaniuma vile navyoweza ku sacrifice muda wangu kua karibu na mtu nikiamini kuna kitu nakijenga kumbe nampigia mbuzi gitaa. Imefikia hatua nawaogopa wadada wa kibongo, natamani labda nitafute raia wa nchi nyingine / mzungu etc.

Wiki hii nzima nimekua nikiwaza na kuwazua nakosea wapi. Umri nao unasonga, hakuna gf wala mchumba inanipa stress sana sana. Kijana ukishafika miaka 30+ , shule umeenda na una ajira/shughuli za kukuingizia kipato cha kutosha kila mtu anatarajia kuona unakua na familia, maswali ya unaoa lini yamekua mengi hadi wakati mwingine napanic vibaya sana.

Kama kuna mdau anaemfahamu mwanasaikolojia wa mahusiano , naomba aniunge nae nipate na ushauri wa kitaalamu pia.
Tatizo lako nilifahamu ngoja nitarudi nikushauri.
 
We unakaa na demu miezi 6 ujamtongoza c uzwazwa huo hata CIA hawawezi kuchunguza kwa muda wote huo we hata ukikutana nae cku ya kwnz mtongoze wazungu hawakukosea kusema love at the 1st sight asee
 
Tatizo lako wanawake wanakuona kwa mtizamo tofauti huna mvuto upo ka kinyago cha mwenge, tumia ndoo kuoga ukimaliza kuoga bakisha maji kidogo yasukume kwa mguu wa kushoto alafu taja jina la mwanamke ambae utamtongoza zingatia jina unalitaja mara tatu
Senior Gambler... mzee wa kubeti kumbe na ww upo upo kwenye mambo ya mahusiano mi nikajua we ni mzee wa tips tu
 
We unakaa na demu miezi 6 ujamtongoza c uzwazwa huo hata CIA hawawezi kuchunguza kwa muda wote huo we hata ukikutana nae cku ya kwnz mtongoze wazungu hawakukosea kusema love at the 1st sight asee
Ndio tatizo lake yuko too nice ndio maana mpaka mademu wanamuonea huruma wew kama mwanaume unamuweka demu miezi sita ndani ya miezi sita huyo demu kashatongozwa mara mia moja wewe bado unajivuta.
 
Ok iko hivi, wanawake wengi wenye upeo kidogo (group ambalo nahis ndo unalolizfukizia) wanataka mwanaume ambaye atamu outsmart kidoogoo sana.... kama wew uko waay beyond ina maana unamjengea hofu tayari, atakuogopa wakati yey anachohitaj ni mtu ambaye atleast they could play an equal part when it comes to building a relationship and life.
Na kama yeye ndo ataku outsmart that means she will get bored easily so no future there....
Kwa wanawake ambao wana upeo na wako mature enough na hawako desperate wanakuwaga na hesabu kali sana... which is very easy for them to spot vitu wasivyovitaka kwa mwanaume mapemaaaaa na kujua kabisa wanaku categorize wapi wew kama a potential suitor au friend zone type of a guy....
Jichunguze na jitathimn...
N:B wanawake wenye upeo are very choosy so be careful around them......
 
Wewe bwana fanya ninayokwambia halafu utakuja kunishukuru

Hakuna mkate mgumu mbele ya chai


Hahaha labda mwanaume uwe mfanyabiashara mwenye pesa nyingi kama za Reginald mengi, ndo utumie kuwapata wanawake wazuri wasiokupenda, la sivyo utafilisika na kufa muda ambao si wako..mm kwakweli kwa hali nliyo nayo mdada kama atataka kunichuna labda anichemshe aninywe supu. Shunie
 
Baadhi yetu tumekuwa tunaishi tu. Hatuna mpenzi. Hatujaribu umalaya. Hatumpendi mtu. Hakuna anayetupenda. Tunajishughulisha tu na kazi zetu, tunakula, tunalala, na kuishi maisha.
nakuja pm unifundishe kua hvi
 
Back
Top Bottom