MSEMEA JAMVINI
Member
- Mar 12, 2011
- 15
- 5
haya hongera ndugu mchambuzi anzisha ukurasa wa uchambuzi kwenye gazeti la mwana halisi...
Kama mumenisoma vizuri utagundua kwamba nachozungumzia mimi ni Chadema kutokuwa na defensive strategy inayohusiana na maswala haya. Tuna silaha nyingi sana za kuishambulia CCM na Mchambuzi katupa hints ni ngao zipi CCM inajivunia leo. lakini hapo hapo hakutazama kama Chadema nayo ipo uchi sana haina ngao zake isipokuwa silaha tupu za mashambulizi. Tukishambuliwa ktk Ukanda, Udini au Ukabila mara zote huja na mifano ya Zitto.. Yaani kweli Zitto pekee ndio sababu ya kutulinda ktk Ukanda, Ukabila na Udini. Nini ngao zetu? sisi tunaweza vipi kujivunia kutoshiriki ktk hizi tuhuma za KUJUANA tofauti na CCM ambao hadi kesho tunaunga mkono baadhi ya ushirika wao wenyewe. Hatuna majibu mkuu wangu tunaulizwa kila siku hapa JF mara zote majibu hutolewa na kina Mkandara au Mohammed Mtoi.. Mimi na Mohammed Mtoi tunaweza vipi kuwa na majibu ya uongozi wa Chadema inapokabiriwa na tuhuma nzito kama hizi hata kama najua sii kweli.. sema kweli maana janvi hili ni mawazo ya mtu mmoja mmoja sio janvi la chama.
Uvumi siku zote ndio hujenga imani za watu, wanasema Chadema ni chama cha Ukanda au udini, wewe huzioni, mimi zisioni na vile vile kumbuka hata mtu wa CUF anaamini hivyo hivyo. Na sidhani kama tunaweza kuonyesha Udini wa CUF lakini Je ni watanzania wangapi wanaamini CUF sio chama cha Waislaam au Wazanibar?..wamepewa majibu gani?.. maana ukweli ni kwamba CUF wenyewe hawana ngao, hawana majibu wala defence mechanism inayo onekana isipokuwa wao wenyewe wanajiingiza zaidi ktk ukimya.. Je ktk hali hiyo unafuu na credit zinakwenda wapi - CCM, uongo! I have done my study mkuu wangu na nakuhakikishia najua nilichokiandika..
DF Mallya,Mhe.Mkandara;
Nimesoma andiko lako lote kwa utulivu mkubwa,Nimefuatilia michango yote ya wadau wengine na majibu yako kwao. Naomba kuikubali kwa namna ya kipekee michango ya Mr.Nicholas. Naelewa na kukubali kuwa umetumia muda mrefu sana kuandika uliyoandika. Kama kawaida ni lazima kuna kilichokusukuma hadi kuandika 'Waraka' huu. Nilichogundua ni kwamba ungependa ushauri wako uchukuliwe wote bila kuhojiwa au kuonyeshwa kuwa pengine ulichoandika kilishatekelezwa na chama kipo Imara kuelekea kuchukua dola 2015. Ukiwa na mawazo ya aina hiyo ni dhahiri kuwa unaweza ukakwazika kuishauri CHADEMA kama 'Alivyokwazika' Mr.Pasco. Chama chochote cha Siasa kina mikakati mipya kila siku. CHADEMA imekuwa na mikakati ya kila siku yenye mafanikio makubwa. Ukitaka kwenda kukabiliana na adui yako unapaswa kubeba silaha zako na si kusubiri yeye arushe mshale uudake na kuutumia kama silaha yako. Kauli za udini na ukabila kwangu mimi ni nyimbo za zamani zisizosikilizika tena! Ni nyimbo za Nape ambazo aliziimba zikakosa nafasi kwenye masikio ya wananchi. CHADEMA kama chama kukubali kuzibeba kauli hizo na kuhangaika kuzijibu ni kupoteza muda badala ya kuendelea na harakati za kujikita kujenga imani kwa wananchi waishio vijijini. Nitakuwa na hamu ya kuona majibu official kutoka kwa uliowalenga kwenye waraka huu (Kama wataona inafaa kujibu).
Wewe unaitwaje Kiswahili?
Request dropped.....
Unaweza kutupa asilimia ngapi? kutoka kanda tofauti kwenye uongozi na ubunge wa chadema.
Mkuu nimekupata vizuri. Naona hawataki kukubali changamoto unazowapa. Nadhani hawataki kukubali kuwa, popotte pale walipo, Wachagga wote ni pro CDM na hawajifichi kwa hilo na wako mstari wa mbele kuwashawishi non chagga kuwasupport. Mtu akijiuliza why chaggas atakuwa amekosea? Na kwa kuwa
most of all chaggas ni wakristo tena wa kweli , hoja ya anti muslim hata kama si yao, lakini shombo lake lazima liwapate. Hii ni kama ilivyokuwa kwa CUF. Ilikuwa ni rahisi kuwabrand udini kutokana na uhusiano wao wa karibu na Wapemba. Kwa hiyo ni vizuri wakaelewa kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo wanapaswa kukabiliana nazo.
Mkuu siyo lazma ukopi uzi wote, wengine tunatumia vimeo vya mobile mnatuchosha bana
Mkuu WildCard, hakuna kitu kizuri kama ukweli "truth", na kuukataa ukweli ambao upo ni "denial" lengo lake ni kujifariji kwa kujipa false hopes, realty ikikuumbua, unaishia kuwa frustrated!.DF Mallya,
UDINI na UKABILA vipo. Kujifanya kwamba hatuvioni ni ujinga uliopitiliza. Jiulize maswali machache haya:
-Kwa nini KIONGOZI wa chama fulani cha SIASA anapokuwa dini au kabila fulani wafuasi wengi wa chama hicho wanakuwa wa dini au kabila la kiongozi wao?
-Moja ya vigezo vilivyotumika kumteua Pinda kuwa WAZIRI MKUU wetu ni DINI yake.
Mkuu Semilong, usemayo ni kweli tupu!.Mkandara
Nimesoma na nimejaribu kukuelewa lakini nilivyoelewa mimi tatizo ni Image appeal ya CDM, na nitaandika bila kumumunya maneno.
Mwanzo ilikuwa rahisi kukiita CDM chama cha kikanda kwa ajili klilikuwa kina wabunge kutoka upande wa kaskazini, na hii ni kutokana na ukweli kwamba kiliapata wabunge wengi kutoka kaskazini kuliko upande wowote. Sasa hivi huwezi tena kukiita chama cha kaskazini kwa ajili kimejipambanua kwenye maeneo mbali mbali, kwa maana nyingine kinayo kinga (ngao) dhini ya hii shutuma.
Kwenye swala la udini CDM bado haina ngao, bado CDM kiitwa chama cha kiikristu kujitetea ni shida sana. Sana sana watakutajia ZZK kama CUF watakavyokutajia Mtatiro. Swali je viongozi wa CDM wanafanya juhudi gani kuhakikisha wanapenya mikoa yenye waislamu wengi?
kuna mchangiaji mmoja amemwambia Bob Mkandara kuwa anataka waislamu wapewe vyeo vya bure ndani ya CDM na amepinga kitu hicho, mimi nasema hivi kama kuna muislamu ambaye unadhani ana influence kubwa na anaweza kubring in many votes, na CDM wanaweza kumsajili basi wasisiste kumsajili na kumpa cheo. CDM needs support of the muslims more now than ever before.
CDM wasirudie kosa walilolifanya CUF, lakuitwa chama cha waislamu na kutofanya juhudi zozote za kuhakikisha wanapata wakristu wengi.
Kuna wakristu wengi humu JF wanapinga hichi kitu, lakini huu ni ukweli, muslim block ni kubwa na ina control votes nyingi TZ kama wakristu wanavo control. Ni wakati wa wote (christians & muslims) na sio sisi.
Jana CUF walijaza jangwani na ukiangalia waudhuriaji wengi kutokana na mavazi yao ni waislamu, what is CDM doing kuvutia hawa watu??
CDM needs to do more to appeal to muslim voters.
Nawakilisha
Kiukweli, nilitukanwa sana, kuna wapenzi wa Chadema, wanawaabudu baadhi ya viongozi wao, hivyo ukiwaguza tuu, inaonekana kama ni kukufuru!. ZZK alipotaka kugombea uenyekiti kumpinga Mbowe, cha moto alikipata, kosa lake lilikuwa moja tuu, dini yake!. Profesa Safari alipojiunga Chadema, niliwaeleza huo ni mtaji!.Wanabodi,
Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa.
Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015.
Kwanza Freeman Mbowe, ajiuzulu uenyekiti, ampishe Dr. Slaa kwenye Usukani, Katibu Mkuu mpeni Zitto, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, ili Walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kuwapigia kura 2015.
Pasco, hivi hawa CDM mbona mnawapa ushauri (consultancy) ya thamani kubwa bila kuwacharge chochote? Mnawapendea nini hawa? au mpaka watakapoteua IGP awapige virungu ndio mtajua kuwa hawa watu hawafai!!! Chondechonde huu ushauri mnaotoa usije kuwatokea puani siku moja. Hao waacheni na kiburi chao waendelee kuwa chama cha maandamano, dola hawaiwezi hao watatuharibia nchi...Mkuu Semilong, usemayo ni kweli tupu!.
Kwenye ile mada yangu ya CCM Imechokwa Chadema Haijajipanga, nimelizungumzia hili
Kiukweli, nilitukanwa sana, kuna wapenzi wa Chadema, wanawaabudu baadhi ya viongozi wao, hivyo ukiwaguza tuu, inaonekana kama ni kukufuru!. ZZK alipotaka kugombea uenyekiti kumpinga Mbowe, cha moto alikipata, kosa lake lilikuwa moja tuu, dini yake!. Profesa Safari alipojiunga Chadema, niliwaeleza huo ni mtaji!.
Hakuna ukombozi wa kweli pasipo kafara, lazima Chadema kikubali kutoa kafara baadhi ya nafasi zake za uongozi wa juu na kuwapa Waislamu. Nlishauri hata ikibidi kuwapa mahakama ya kadhi, wapeni, mbona Kenya na Uganda mahakama hizi zipo na hakuna any conflict of interest!.
Mkandara amefungua pandora box la udhaifu wa Chadema, naamini ni kupitia uzi huu Chadema lazima mkubali ukweli na kubadilika, vinginevyo 2015, ni CCM tena!, mimi na mgombea wangu EL tutapeta kiulaini na tutakutana tena humu kupeana pole!.
Pasco.
CHADEMA hata wamteue Ponda Issa Ponda kuwa Mwenyekiti na mgombea wao wa URAIS hakuna atakayewaondolea doa hili. Walichelewa kuing'amua ile SILENT CODE ya CCM nao waitumie au waipigie kelele waziwazi. Ni kama ambavyo CUF hawawezi kuuvua UISLAAM hata kama Askofu Kilaini angeteuliwa kuwa Mwenyekiti wao.Mkuu Semilong, usemayo ni kweli tupu!.
Kwenye ile mada yangu ya CCM Imechokwa Chadema Haijajipanga, nimelizungumzia hili
Kiukweli, nilitukanwa sana, kuna wapenzi wa Chadema, wanawaabudu baadhi ya viongozi wao, hivyo ukiwaguza tuu, inaonekana kama ni kukufuru!. ZZK alipotaka kugombea uenyekiti kumpinga Mbowe, cha moto alikipata, kosa lake lilikuwa moja tuu, dini yake!. Profesa Safari alipojiunga Chadema, niliwaeleza huo ni mtaji!.
Hakuna ukombozi wa kweli pasipo kafara, lazima Chadema kikubali kutoa kafara baadhi ya nafasi zake za uongozi wa juu na kuwapa Waislamu. Nlishauri hata ikibidi kuwapa mahakama ya kadhi, wapeni, mbona Kenya na Uganda mahakama hizi zipo na hakuna any conflict of interest!.
Mkandara amefungua pandora box la udhaifu wa Chadema, naamini ni kupitia uzi huu Chadema lazima mkubali ukweli na kubadilika, vinginevyo 2015, ni CCM tena!, mimi na mgombea wangu EL tutapeta kiulaini na tutakutana tena humu kupeana pole!.
Pasco.
Mkuu WildCard, hakuna kitu kizuri kama ukweli "truth", na kuukataa ukweli ambao upo ni "denial" lengo lake ni kujifariji kwa kujipa false hopes, realty ikikuumbua, unaishia kuwa frustrated!.
Kwa wale mliomsoma Hutaki Unaacha, alitumia kuhusu two sets of silent rule ya CCM kwa marais kupokezana kati ya bara na bara na visiwani, na kati ya Mkisto na Muislam!. Akimaanisha japo haikuandikwa popote, ilikuwa rais akitoka bara, anafuatia ni visiwani, then bara, then visiwani, akitoka Mkiristo, anafuatia Mwislamu etc. Hivyo, baada ya Nyerere -Mkisto(Bara), alikuja Mwinyi-Muislam (Visiwani), then Mkapa-Mkisto (Bara) na aliyemfuatia Mkapa ilitakiwa lazima awe Muislamu na atoke Visiwani!.
Kwa vile tayari mle mtandao wa hatari chini ya "the King Maker" ulishaundwa, hilo walilitambua na the next in line kumpokea Mkapa, alikuwa ni Dr. Omar, amini usiamini, he had to be eliminated silently ili ku create loop hole kuwa japo 2005 ni zamu ya Zanzibar, then ikajengwa hoja kuwa Zanzibar had no one, wengi mnakijua kilichompata Dr. Salim na shukrani za waliomshughulikia mnazijua!, hivyo JK akateuliwa as the only option kwa sababu ni Muslamu!. Hakuna ubishi mpaka leo, mpaka kesho, Dr. Salim would have made a beter president 100 times more than JK!. Hakuna ubishi Prof. Mwandosya would have made a better president 100 times more than JK!. Hakupigiwa kura kwa sababu ya ile silent code, "hawezi kutoka Mkapa Mkristu, akaingia Mwandosya Mkristu!, Na baada ya JK Muislamu, na bara tumefululiza, 2015 kwa CCM ilitakiwa iwe ni zamu Mkristo na ni zamu ya Zanzibar. Zilifanyika juhudi za Kumuelevate Brig. General Adam Mwakanjuki (RIP), watazama mbali hilo walisha liona na zamani walikwisha mshughulikia!.
Kihalali, kwa mujibu wa hiyo silent code ya CCM, zamu ya Zanzibar ndio imeshapita kwa kushikwa na JK na zamu ya Muislamu imeshapita, hivyo rule out Shein, rule out Dr. Asha Rose or Muislamu yoyote, game la 2015 ndani ya CCM lazima awe ni Mkristo!.
Ndani ya ukiristo nako kuna kiji secret silent code, kuwa zamu ya rais wa nchi hii kuwa Mkiristo, sio tuu kuwa ni Mkisto ili mradi ni Mkristo, bali Mkristo Mkatoliki!. Hivyo tangu JK anaingia, the 2nd most poweful na probale ni EL, tatizo yeye sii Mkatoliki!, akaundiwa zengwe akapigwa paranja!. 3 rd most powerful na probable ni Samwel Sitta tatizo yeye ni Muangalicana, kilichomkuta mnakijua hivyo the only one left kuteuliwa na CCM 2015 ni Membe, yeye ni Mkatiliki!.
Wa kwanza kuipinga hii secret silent code ni EL, haiwezekani kila rais Mkistu lazima awe Mkatoliki, akaambia huo ndio ukweli wa mambo, lakini kwa vile mkewe ni Mkatoliki, EL akashauriwa ili aweze kuteuliwa kugombea na kuchaguliwa kuwa ni rais wa nchi hii, lazima awe endorsed na Wakatoliki, ndio maana mmemshuhudia EL akijitoa kweli kweli kuchangia harambee za Makanisa ya Katoliki ili kupata hiyo endorsement!. Sitta is finished, just count him out!.
Wale wenye kumbukumbu, nawaombeni sana mlikumbuke bandiko hili, ingawa mimi namsuport EL ndie ateuliwe na CCM kwa sababu ni kupitia kwake, yeye ndiye mwenye uwezo wa kutupatia ukombozi wa pili na wa kweli wa Mtanzania, yale makosa mengine yote ya ufisadi ni mizigo tuu ya watu, ataitua kabla ya 2015, ila atakayeteuliwa ni Membe, sio kwa sababu ya kingine chochote, bali Ukatoliki wake na ndio maana huwezi kuwasikia Katoliki wengine wowote, Pinda, Magufuli etc wakiunusia urais!.
Udini upo, mkubali mkatae!, ila pia ukanda upo, na ukabila pia upo!.
Pasco.
Paco, kwanini umeniwahi na kunukuu yale nilotaka kusema. Huo ndio ukweli nami nitakuwa shahidi wako Januari 2016 wakati wakatoliki watakapoiacha CDM kwenye mataa na kuinyanyua CCM mgombea akiwa Membe. Kaeni mikijua madhehebu mengine ya kikiristo hufuata upepo wa maamuzi ya wakatoliki kwa mfano waraka wa kanisa katoliki, madhehebu yote waliupigia upatu na hata CDM wamepata nguvu 2010 kwa sababu ya uungwaji mkono na kanisa katoliki(Slaa)"HUTAKI UNAACHA". Kumbukeni askofu Kilaini na maneno ya JK ni chaguo la Mungu.