Waraka wangu kwa JWTZ, Watanzania

Mkuu Manyerere kula "like" yangu. Sikuzote umekuwa role modal wangu.

Kimsingi watanzania tunawapenda majirani zetu but hatuwapendi majirani wakorofi na watata,binafsi pamoja na uvivu wa watutsi katika kufanya kazi bt huwa nashirikiana nao kwenye kazi bt namchukia sana PK coz ni dikteta na mpenda vita,maeneo ya Kagera karagwe ,ngara,Manyovu Kasulu wamejaa watutsi pia maeneo ya Kibondo eneo moja ni kijiji Kinaitwa Nabuhima kina wakazi wengi ambao ni Watutsi na neno Nabuhima linatokana na mnyumbuliko wa Hima a.k.a Abhahima wanapenda vita sana na kutawala wenzao.

Madamu Kagame amelianzisha, nasema Jk aongezee makamanda wetu na kama watakuwa wanampango wa Recruit wanajeshi wapya special kwa ajili ya kumng'oa Paulo Kagame nami nitajiunga haraka tena waje haraka tu mng'oe Pk ili kufikia mwezi wa 4 tunywe chai na ubwabwa wa easter Kigali huyu jamaa ni wa kumuua kabisa tena simple Kagame hana akili anapambana na Tz yenye mshikamano kwenye mambo ya msingi while anajua yeye nchi yake kuanzia nje mpaka ndani kuna maadui na nchi imepasuka pasuka tukiamua tunawasapoti kina jenerali Nyamswa then Interahambwe wanakuja kumng'oa wakiwa front cc middle mpaka Kigali japo natambua Museveni amekuwa na hamu ya kulipiza kisasi cha Kipigo tulichompiga Nduli Idd Amin dada, Pk bai bai na uroho wako wa madaraka.

Waandishi wengine wathubutu kuandika kuwapa moyo wanajeshi wetu na wafanye propaganda za vitisho kama hizi
 
Manyerere,

Hivi kweli Rwanda hana maslahi Congo? Mnyonge mnyongeni haki yake mpe. Mwaka 1994 kulitokea genocide. We unawaonea huruma waliokufa kwenye ndege ya rais, na sio wanawake, watoto, nk. walliouwawa kikatili sana na wahutu wenye msimamo mkali, ambao baadae walienda Congo, ambako wapo hadi leo. Na viongozi wao ni walewale waliopanga na kufanya genocide.

FDLR kazi yao ni moja, kuja kumaliza kazi. Hivi pale Congo kungekuwa na kikundi chenye msimamo wa kuiangamiza Tanzania tungekaa na kusubiri tu? Nadhani Rwanda kuwa na mkono wake Congo kuna self-defence justification.

Kuhusu wizi wa madini, ndio, lakini uje kuwa haya madini yanaenda ngambo, yanachimbwa na watu wenye mtaji na teknologia, sio wana-mgambo wa M23 wenye afya mbaya.

Kuhusu EAC, some Treaty inasemaje, kasha uishauri Tanzania cha kufanya, usi-argue kama watoa maoni wa JF. Kuhusu bandari, hili sio suala la uzalendo, ni suala la biashara, watanzania wengi hupitisha magari yao Mombasa, then Horiri.

Kuhusu Watutsi, sioni kama ni jukumu lako kama mwandishi kushambulia kabila Zima, kama Kagame ana siasa ambazo hazikupendezi, basi shughulika nae.

Sidhani kama ni sahihi kuwashambulia Wakwere kwa makosa ya JK, hiyo ndo inachochea genocide. Ndege ya rais ilivyotunguliwa, wahutu walisema imetnguliwa na Watutsi, wakaua hadi motto mchanga, wakati maskini labda alikuwa ni Kagame na jeshi lake.

So, ninaposema ume-nidsappoint, ni kwamba mwandishi mwenye hadhi yako, hapaswi kuandika akiwa na hasira, anaandika kwa hoja kuisaidia jamii kufanya maamuzi sahihi. Au la, usiitumikie jamii kama mwandishi, nenda omba kazi jeshini, fanya mambo ya kizalendo zaidi, au hata mgambo.

Lakini kumbuka kalamu yako inaweza kuanzisha vita saa yoyote, ndoo maana waandishi wa Rwanda wamehukumia ICTR, yule Joshua Arap Sang wa Kenya yupo the Hague, etc. Leo hii humu ndani kuna uchochezi, mgao wa umeme Kagera wanasema ni Kagame, Bandari watu walitunga uongo, vichwa vya habari eti ni kagame., etc. hata kama hatumpendi waandishi wa habari lazima wawe weledi sio wachochezi

Hapo kwenye red nilikuuliza jana hicho kisingizio cha FDLR kimeshachuja.....nitajie ni kiongozi gani wa FDLR ambaye either alikamatwa au alijisalimisha ambaye amefunguliwa mashtaka Rwanda...? Viongozi wote wa FDLR wameishia kupewa madaraka Rwanda, na wapiganaji wa zamani wa FDLR waliojisalimisha mmeishia kuwarudisha kwenye mapigano Congo kwa kutumia proxy forces zenu CNDP = M23. Mfano wa viongozi wachache wa FDLR niliokwambia ambao umekacha kujibu ni hawa Major General Paul Rwarakabije, Lieutenant-Colonel Samuel Bisengimana, Lt. Col. Idrissa Muradadi, n.k .......! Kama kweli FDLR wangekuwa ndio wote wahusika wa genocide kwanini hao waliojisalimisha hamjawafungulia mashtaka? Leo hii Mpiranya akijisalimisha popote alipo atapewa kazi UN au atapelekwa Arusha ICTR.......?

Kikubwa ni kuwa kwa kutumia jina la genocide na mafuvu ya watu walioawa bila hatia na FAR pamoja na RPF, Kagame na kagenge chake cha wahuni bado wana kiu ya damu ya kuua watu wasio na hatia na dunia imesema basi. Kagame na kagenge chake cha wahuni walianza mauaji tangu wakiwa Uganda, waliua watu wengi sana kule Northern Uganda mpaka Museveni akaona imetosha, wakahamia Rwanda wakaendelea kuua...! Ndio maana hata alipoulizwa na Gen. Romeo kwanini hasitishi mapigano Kigali na kuokoa maisha ya watu hata Watutsi wenzake yeye Kageme alijibu 'acha hao watutsi wafe kwa vile hiyo nayo ni sacrifice yao katika vita'.....hii ipo kwenye records..!

Inshallah....with JWTZ tutakunywa chai Kigali...!
 
Hehe Propaganda bwana.... kuna warwanda wanajifanya watanzania humu. Hehehehee
 
nenda nawewe ukaichukue hiyo thawabu kubwa! mkuu hebu acha kejeli kwa wafiwa hujui wategemezi wao wanabaki katika hali gani! unachefua sana! nilikuwa nakuheshimu sana kabla!
Usitake kuleta itikadi kiraia kwenye Jeshi,unafikiri ni hizo kazini za kiraia,hujui wanakula kiapo gani?,usituletee jeshi la mbu hapa,ndio mnapelekwa mafunzo muondolewe uraia..
 
wahutu waliitungua ndege yao wenyewe ili kuhalalisha mauaji ya kimbari..(tafuta matokeo ya uchunguzi uliofanyika hivi karibuni)
-Kongo wamekuwa kwenye vita kabla ya m23, kagame na M7 na Tanzania tumekuwa neutral miaka yote hiyo,kwa nini leo uone ni wakati muafaka kwa Kuikomboa kongo?
-Rwanda ni nchi ya pande mbili tu,Hutu au Tutsi..pamoja na matatizo yote ya KP , ameweza kuidumu Rwanda vizuri sana, KP akitoka madarakani kwa kupinduliwa....tutayaona ya Kimbari tena, sema tu mara hii na technolojia hii(sio mapanga kama 1994) yanaweza kuvuka mipaka.
 
Nimesoma waraka wako nimeshindwa kuelewa;

1.0 Kichwa cha habari na content yenyewe. Kwa nini uliamua kuuita waraka kwa JWTZ??

2.0 Vita ni fedha. Kwa hali ya sasa ya Tanzania hatutakiwi kupigana vita yoyote ile. Nchi iliyoshindwa kujitegemea kibajeti tokea uhuru mpaka leo, bado inategemea misaada ku "subsirdise" bajeti yake halafu ikapigane vita!!!

Nashindwa kuelewa mwandishi kama wewe unameshindwaje kuelewa kuwa Tanzania ya JK hali ya uchumi ni mbaya labda kuliko hata Mkapa alipokuwa akiondoka. Kama serikali inashindwa kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kukosa fedha itawezaje kugharamia vita ambayo ni ghari kuliko miradi ya maendeleo??? Deni la Taifa kila siku linakuwa kama mimba lakini hatuoni kinachofanyika kisha tukapigane vita!!! Ni jambo la kushangaza sana.

Ukweli kama hujui tukusaidie, serikali ya sasa imebaki kulipa mishahara tu na kupiga propaganda kuwa uchumi unakuwa kwa asilimia fulani huku mwananchi wa chini akizidi kuzama katika dimbwi la umaskini.

3.0 Umeshawahi kujiuliza athari za vita tuliyopigana ya kumng'a Iddy Amini?? Ile vita ilikuwa haikwepeki lakini uchumi wa nchi ulitetereka sana, itakuwaje leo Taifa la kujisifu kwa kupewa misaada tukapigane vita??

Kwangu mimi huu ni waraka wa kishabiki na kipuuzi kabisa.
Unataka kuniambia uchumi hauruhusu kwa iyo ukishikwa makalio we cheka tu,inama uitikie ndio afande.,we akili zako nukta,shujaa ni yule anaejitetea mpaka tone la mwisho..
 
Mnhhhhhh....atleast i have a bunch of fellow and true tanzanians who are ready and morally prepared to rid this "slim-shady" president....kwa ufupi ni kwamba haya mapambano yetu dhidi ya m23 hayatokuwa na maana hata kidogo endapo hatutomtoa kagame madarakani rwanda na kuikalia rwanda mpaka itapo-pata serikali ya kidemokrasia

na wakati huo tunahakikisha jumuiya ya africa mashariki inasikiliza nini waasisi wake tunasema na sio kila tom, harry n dickens wameingia juzi wanapiga kelele za kitotototo tuu...mjara sahivi wanataka kuwaingiza somalia na juba....upuuzi mtupu.

Kenya naye anatakiwa aelewe...bila tanzania hakuna east africa kwa sababu tanzania ni almost 65% ya kila kitu kinachoifanya jumuiya iitwe africa mashariki...kama haamini tutoke aone wataiitaje hiyo jumuiya yao ya kenya uganda rwanda burundi, juba na somalia....

Jk pia anatakiwa aelewe kitu kimoja..watanzania pamoja na kuwa hatumpendi kwa sababu ya tofauti zetu kimtizamo..kwa hili tuko pamoja naye..na akumbuke pia wakati wa mkapa wengi wetu tuliikataa hii jumuiya ila ni ubabe wa mkapa uliotufikisha huku.....tutafurahi sana jk ukitamka kuwa tumejitoa mpaka hapo tutakapo-watangazia tena kurudi kwenye hiyo jumuiya na tunaweka sheria zetu ku-deal na uchumi wa nchi jirani za kenya uganda rwanda na burundi huku mipaka ikiwa wazi kwa nchi za sadc.

Jk...kuwa amiri jeshi mkuu ni pamoja na kutoa maamuzi magumu ikiwamo pia kulinda mipaka ya nchi kabla haijashambuliwa....kagame ni red alert threat...anatakiwa awahiwe mapema kabla haja-tuwahi..na muda ni huu ukimkosa hapa utaiachia nchi yetu majuto na mwiba wenye sumu kwa wajukuu na hasa mabinti wa mwanao riz....

Najuwa kimoyomoyo nzee nkapa anajuuta kutuingiza eac ya kagame...anajuuta kwa yale wananchi tuliyoyakataa na hakutusikia sasa anayaona na hana jinsi ya kufanya...pole nkapa...tafadhali nshauri nzee jk.

Tukiwachapa hao m23..jeshi letu thabit lirudi nyumbani haraka sana kwa njia ya miguu na anga likipitia short-cut ya chigali tukawapokee rusumo na kuadhimisha ushindi pale kambi ya kaboya.

Mungu ibariki tanzania mungu ibariki africa....na mungu mbariki jk afanye haya watanzania tunayomshauri.
 
Tumeanza kuwatambua watutsi humu JF. Tujadili mada, kejeli na matusi tuviweke pembeni.

Manyerere - wala usiumize kichwa. Huyo jamaa ni mtusi na subiri wengine wanakuja. Inasemekana Hitler mdogo kapeka battalion mbili kuelekea Goma. Sasa inabidi aamue kusuka au kunyoa. Aendelee mbele akutane na wanaume au arudi nyuma. Yote mawili aibu tupu. Itabidi achague iliyo nafuu.
 
Ukifa wakati ukiwatetea wanyonge wenzako ni thawabu kubwa. Mungu akipenda tutaushuhudia ukombozi wa Wacongo kabla ya kufa kwetu.


Huu ni upumbavu na ulimbukeni, uko wapi ushujaa wako endapo umeshindwa kutumia kalamu yako kuiokoa tanzania isiteketee dhidi ya maradhi ujinga na umasiki? Ni watanzania wangapi wanakufa hapa nchini wakikosa matibabu na umefanya nini kuhakikisha vita dhidi ya umasikini maradhi na ujinga inatoweka kwanza kabla hujatupeleka machinjioni DRC?

Dunia yasasa kushabiakia vita vya Risasi na mabomu ni kwa wajinga na wapuuzi kama wewe. Tunahitaji kupigana vita ya kimaendeleo katika taifa letu na kuhakikisha tunapiga hatua bora dhidi ya hao kenya, Rwanda, nawengine wengi sio kuenda kupigana nje ya nchi tukiacha watanzania wakiteseka
 
Unataka kuniambia uchumi hauruhusu kwa iyo ukishikwa makalio we cheka tu,inama uitikie ndio afande.,we akili zako nukta,shujaa ni yule anaejitetea mpaka tone la mwisho..

Haya ndiyo matatizo ya kujibishina hoja na vijana waliomaliza Form Four mwaka jana. Hivi umesoma between line au mekurupuka tu???

Pigana vita isiyoepukika mfano vita za uvamizi wa nchi, kudhalilisha utaifa wa mtu na maslahi lakini siyo kama hiyo mnayotaka kutetea.

Hapo jambo la msingi ni kuwapiga M23 kisha kulijengea Jeshi la DRC uwezo wa kulinda mipaka yake na watu wake na siyo kwenda kupambana na Kagame pasipo na ulazima.
 
Sikutaka kukujibu, lakini ngoja nijaribu. Hoja yako ya kwanza sijajua wapi huelewi. Unaweza kuwa sahihi kwa sababu headline za kifilosofi huwa zinawasumbua wengi pale wanapojaribu kuunganisha na hoja iliyo ndani. Pili, hii vita inagharimiwa na UN, ndiyo maana kuna majeshi hadi kutoka Afrika Kusini. Tunachojaribu kukifanya hapa ni kuhakikisha tunakuwa na minimum causalities kwa askari wetu. Tatu, kuna maeneo ambayo amani haiji isipokuwa kwa ncha ya upanga! hatushangilii vita, lakini tuangalie namna Kagame anavyosumbua eneo hili la maziwa makuu.

Tukiachana na yote hayo lakini ningefurahi sana kama ungesema kuwa baada ya M23 kupigwa basi TPDF ifikirie kulifunza Jeshi la DRC ili kuweza kulipa uwezo jeshi hilo liwe na uwezo wa kulinda mipaka yake na watu wake badala yake unasema eti Kagame apigwe na majeshi yaliyopo huku kwa gharama za UN badala ya UN kufadhili vita na Rwanda.

Kiini cha tatizo la DRC ni ukubwa wa nchi yenye rasilimali kubwa kulinganisha na uimara wa serikali iliyopo madarakani hasa jeshi lao. Kama ungetembea humo ningekusupport.
 
Sioni kwanini tusianzishe Jumuiya yetu kwa kuwakaribisha DRC na Burundi. Sisi ni taifa kubwa. DRC ni taifa kubwa pia. DRC na Tanzania tuna rasilimali nyingi mno. Faida za kujitoa EAC ni kubwa kwetu kuliko kuendelea kuhangaika na hawa wapenda vita. Tuwaache waanzishe yao, na sisi tuanzishe yetu. La, hilo kama haliwezekani, tujikite zaidi SADC ambako kuna soko pana kuliko EAC.
Tukijitoa EAC atakayeumia zaidi ni Kenya maana bidhaa na uwekezaji wake mkubwa kauelekeza Tanzania. Soko lake kubwa lipo Tanzania. Wanajidanganya tu.

Tusiendelee kuwabembeleza watu wasiokuwa na shukrani. Tuwatakie heri katika ndoa yao hii mpya ambayo sioni uhai wake. Hizi ni hasira za mkizi ambazo mara zote humnufaisha mvuvi. SADC ni bora zaidi. Tupeleke nguvu zetu kwenye SADC.

Kagame na Museveni walisaidiana kuichukua Uganda. Museveni alimsaidia Kagame kuitawala Rwanda. Sasa wanasaidiana wachukue sehemu ya DRC. Museveni anamsaidia Kagame katika hili. Tutambue kuwa inayofuata ni Tanzania. Si ajabu wale Wanyarwanda waliokuja siku nyingi sasa wakadai wanabaguliwa, na kwa sababu hiyo wakaanzisha vita ya kutaka kutambuliwa au kujitenga na kuwa sehemu ya Rwanda na Uganda (Bahima Empire).

Njia pekee ya kumwondoa Rais Kagame ni hii aliyotusaidia kuiweka, yaani vita. Kuichokoza Tanzania ni njia ya kuelekea ukingoni mwa utawala wake. Amepigana kwa muda mrefu na wasiojua vita. Amejaribu kuitisha Tanzania akidhani atafanikiwa. Kinachotakiwa sasa ni kumwonyesha kazi. Safari iliyoanzia Goma inastahiki ihitimishiwe Kigali. Kama kasahau, arejee kwenye historia ili ajue kilichompata nduli Iddi Amin Dadaa. Buriani Kamanda Khatibu Mshindo.

manyerere@hotmail.com


[/COLOR][/SIZE]
Nimekusoma vizuri nadhani yote uliyoyaandika yana ukweli nimesikitishwa na habari za Rais wetu kutaka kikao cha usuluhishi kitu ambacho nikosa sana!!https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...kuitisha-kikao-cha-usuluhishi-ahuna-kosa.html
 
Haya ndiyo matatizo ya kujibishina hoja na vijana waliomaliza Form Four mwaka jana. Hivi umesoma between line au mekurupuka tu???

Pigana vita isiyoepukika mfano vita za uvamizi wa nchi, kudhalilisha utaifa wa mtu na maslahi lakini siyo kama hiyo mnayotaka kutetea.

Hapo jambo la msingi ni kuwapiga M23 kisha kulijengea Jeshi la DRC uwezo wa kulinda mipaka yake na watu wake na siyo kwenda kupambana na Kagame pasipo na ulazima.
Wewe ndio unaonyesha jinsi gani hata form two hujamaliza,kama issue nikumng'oa M23 hizo troops za PK alizopeleka mpakani anataka kuhalalisha nini?,JWTZ walioko DRC ikitokea Pk anarusha makombora DRC hata wapiga hata kama wanailinda Goma bali atawapiga Wanajeshi wa Congo,na ikitokea kawaua Jwtz tukae kimya sio...idiot
 
Nimekusoma vizuri nadhani yote uliyoyaandika yana ukweli nimesikitishwa na habari za Rais wetu kutaka kikao cha usuluhishi kitu ambacho nikosa sana!!https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...kuitisha-kikao-cha-usuluhishi-ahuna-kosa.html


Majadiriano na mapatano kupitia mjadala mezani ndiyo njia sahihi ya kutatua matatizo na migogoro bila kuingiza mataifa katika gharama zisizo za lazima.

Tutakapo lazimisha mgogoro huu ambao ni mdogo sana na wakipuuzi ufikie hatua ya vita nikutowatendea haki watanzania kwa ujumla wake, sasa hivi watu wanalipwa mishahara duni isiyokidhi mahitaji ya lazima, hela haitoshi hata huko serikalini kiasi kwaba baada ya kushindwa kwenye njia zote sasa wanahamishia kodi mpaka kwenye kadi za simu.

Nisababugani hasa za lazima kutuingiza vitani? mh kikwete akaye na Kagame wayaongee kikubwa yaishe.
 
ukiulizwa sababu hasa ya sisi kupigana na Rwanda utajibu nini?unajua gharama za vita au unatunga verse tu humu!tuache siasa za kanga moko hapa tuangalie mustakabadhi wa nchi yetu tukisha wapiga Rwanda ndo itakuwa nini sasa??au huyo jemerali ni nduguyo mbona kule sudani tulipoteza wanajeshi wengi zaid ya huyo jenerali!
 
Back
Top Bottom