Manyerere,
Hivi kweli Rwanda hana maslahi Congo? Mnyonge mnyongeni haki yake mpe. Mwaka 1994 kulitokea genocide. We unawaonea huruma waliokufa kwenye ndege ya rais, na sio wanawake, watoto, nk. walliouwawa kikatili sana na wahutu wenye msimamo mkali, ambao baadae walienda Congo, ambako wapo hadi leo. Na viongozi wao ni walewale waliopanga na kufanya genocide.
FDLR kazi yao ni moja, kuja kumaliza kazi. Hivi pale Congo kungekuwa na kikundi chenye msimamo wa kuiangamiza Tanzania tungekaa na kusubiri tu? Nadhani Rwanda kuwa na mkono wake Congo kuna self-defence justification.
Kuhusu wizi wa madini, ndio, lakini uje kuwa haya madini yanaenda ngambo, yanachimbwa na watu wenye mtaji na teknologia, sio wana-mgambo wa M23 wenye afya mbaya.
Kuhusu EAC, some Treaty inasemaje, kasha uishauri Tanzania cha kufanya, usi-argue kama watoa maoni wa JF. Kuhusu bandari, hili sio suala la uzalendo, ni suala la biashara, watanzania wengi hupitisha magari yao Mombasa, then Horiri.
Kuhusu Watutsi, sioni kama ni jukumu lako kama mwandishi kushambulia kabila Zima, kama Kagame ana siasa ambazo hazikupendezi, basi shughulika nae.
Sidhani kama ni sahihi kuwashambulia Wakwere kwa makosa ya JK, hiyo ndo inachochea genocide. Ndege ya rais ilivyotunguliwa, wahutu walisema imetnguliwa na Watutsi, wakaua hadi motto mchanga, wakati maskini labda alikuwa ni Kagame na jeshi lake.
So, ninaposema ume-nidsappoint, ni kwamba mwandishi mwenye hadhi yako, hapaswi kuandika akiwa na hasira, anaandika kwa hoja kuisaidia jamii kufanya maamuzi sahihi. Au la, usiitumikie jamii kama mwandishi, nenda omba kazi jeshini, fanya mambo ya kizalendo zaidi, au hata mgambo.
Lakini kumbuka kalamu yako inaweza kuanzisha vita saa yoyote, ndoo maana waandishi wa Rwanda wamehukumia ICTR, yule Joshua Arap Sang wa Kenya yupo the Hague, etc. Leo hii humu ndani kuna uchochezi, mgao wa umeme Kagera wanasema ni Kagame, Bandari watu walitunga uongo, vichwa vya habari eti ni kagame., etc. hata kama hatumpendi waandishi wa habari lazima wawe weledi sio wachochezi