Waraka: Kanisa Katoliki laandaa waumini uchaguzi 2010

Status
Not open for further replies.
Niliposoma hizi document nimegundua kuwa kanisa lingejitanga moja kwa moja kwamba ni chama mbadala na katiba iruhusu vyama vya kidini haraka iwezekanavyo wananchi wachague christian party kama wanaona itafaa kwasababu zifuatazo:-
a) watoa elimu hiyo kama ilivyo ainishwa katika ngazi ya famili, vigango, ktiongoji etc...ni viongozi wa kanisa na wakristo..kwa vyote vile lazima wana conflict of interest hivyo waruhusu vyama vya kidini
b) Report system: wakisha fanya mikutano na kutoa elimu wanareport kwa wakubwa kwenye hierachy ya kanisa ili kupata nini? directive? au nini wakubwa lazima wana conflict of interest na watu ya dini yao???
c) Ni dalili mbaya na ni aibu kwamba imetoka kwa maaskofu wa Tanzania shame on them!!!
NB. Nafikiri waislamu waanzishe the same move na katiba iruhusu kuwepo na vyama vya kidini watanzania waamue chama cha dini gani zipongoze kwa kuangalia sera na dira yao
Otherwise: huu ujinga wa maaskofu wa Tanzani ukomeshwe mara moja...

Lol....udini umekukaa hata huoni kitu!
 
"Ninachowataka wanasiasa wote washiriki ni kupiga vita ufisadi. Asiyetaka kupigana na ufisadi tusimchague, na ndivyo mwongozo huo unavyosema,"

nafikiri mstari unaowaumiza wengi ni huo hapo juu, i'm just thinking...
 
Mwanakijiji,
Shukrani kwa hekima zako. Nadhani moderator aingilie kati na kuchuja pumba na mchele.
Kwa utaalamu wangu wa masuala ya Afya ya akili,Tumaini ni mtu wa kuonewa huruma kwa maana kama unashindwa kutoa critical anaysis ya kitu na kuishia kufoka na kutoa shutuma. Hii inaonyesha udhaifu wa akili ktk kupambanua hoja na anatakiwa apate tiba.

Inawezekana pia akawa anatumiwa na watu ambao lazima wamempa pesa. Uzoefu unaonyesha kuwa mtu aliyehongwa,huwa anaazima akili ya mhongaji na kuanza kufikiria kama anavyotaka mhongaji.

Ni vema Tumaini na waliomtuma wakaja na waraka wao kisha tukaweza kupata good product kwa manufaa ya nchi yetu. Ikumbukwe kuwa nia ni kuwa na nchi bora. Kama mambo yangekuwa yanaenda vema,huo waraka wala usingetungwa na ndugu yangu asingekuwa na hasira na kufoka kusingekuweko!
 
Hapana Kalunguyeye....huop sio udini...ni mtazamo tu wake Hata wewe unaweza kuwa namtazamo tifauti na huo..., au unataka kila jambo linalotolewa na kanisa basi watu waunge mkono tu...hata kama linaonekana ni la hatari..
 
Ila wewe choka mbaya, nafikiri pia umechoka kweli mbaya..kiasi kwamba ukawa na upogo wa kuweza kung'amua mambo kwa jicho la yakini. Kwanini kila mtu ukiwemo wewe..mnamlaumu Tumaini?? kwani kosa lake ni nini?? ni kule kuonesha tofauti na mtazamo wako na wenzako?? hapo iutakuwa unaitumia akili yako vibaya, ambapo ni makosa sana kufanya hivyo. We nawe toa hoja zako katika hilo ili sie tupate kuchambua hayo mambo, lakini ukianza kumchambua mtu na kumuona hana akili na mwenye akili ni wewe....hapo wakosea.
 
Ila wewe choka mbaya, nafikiri pia umechoka kweli mbaya..kiasi kwamba ukawa na upogo wa kuweza kung'amua mambo kwa jicho la yakini. Kwanini kila mtu ukiwemo wewe..mnamlaumu Tumaini?? kwani kosa lake ni nini?? ni kule kuonesha tofauti na mtazamo wako na wenzako?? hapo iutakuwa unaitumia akili yako vibaya, ambapo ni makosa sana kufanya hivyo. We nawe toa hoja zako katika hilo ili sie tupate kuchambua hayo mambo, lakini ukianza kumchambua mtu na kumuona hana akili na mwenye akili ni wewe....hapo wakosea.

Hebu tukumbushe ni hoja gani aliyoitoa Tumain ambayo inahusiana na mada..Usikimbie maana umelianzisha mwenyewe hili
 
Mi nawashangaa watu wanokupa thanks..wanakupa kwa hoja gani,...? Udini..? au upogo..? kweli siku hizi ustaharabu hamna kabisa...yaani mtu anamtukana mwenzake then kuna watu wanshangilia...kweli dunia imekwisha.
 
Sijaona sehemu iliyotamka kuwa wakristu tuwachague wakristu wenzetu.Kanisa lina structure ambayo imezingatiwa ili malengo ya waraka huu yawezwe kuwafikia walengwa. Kwa hali ya mambo ilivyo, kanisa kama taasisi nyingine za kidini zenye wajibu wa kuongoza waumini wao, ni lazima lionyeshe njia. Suala la kuchagua viongozi bora ni suala lisilopingika na sioni kama ni udini. mambo yakienda vibaya hapa kwaajiri ya kulea matatizo yaliyopo, wote tutaathirika including kanisa.
 
Tusipoteze lengo. Kanisa lina wajibu wa kuwatumikia waumini wake na kuwapa mwongozo wa kiroho. Enzi za "heri masikini, utawala wa mbingu ni wao" zimekwisha...hata kanisa lingependa kuwaona waumini wao wakijisaidia..na kwa kuanzia ni kuwaelimisha namna ya kuchagua viongozi bora wa kuwafikisha huko....Hivi mnafikiri kama serikali ingekuwa inatimiza wajibu wake..wavunja sheria (papa na nyangumi) wanapelekwa mbele ya vyombo vya sheria, viongozi wanawajibika ipasavyo, kodi ya wananchi inatumika ipasavyo..unafikiri kanisa lingekuja na waraka kama huu? Kanisa linajaza ombwe (vaccum) iliyoachwa na serikali...kwa sababu watawala wameshiba wakajisahau..

Kinachotokea hapa ni kwamba serikali imeshindwa kutoa elimu ya URAIA, imeshindwa kuwashirikisha wananchi katika process nzima ya kufanya maamuzi (na si kwa bahati mbaya bali kwa makusudi ili kulinda status quo-inataka wananchi waendelee kuwa wajinga). Kanisa wameliona hili..wakasema..well, wananchi/waumini wetu hawastahili kuishi hivi..lets do something. Hawajasema ..wapigieni kura CHADEMA, CCM, CUF NK..wao wameweka vigezo vyao..sasa wewe kama ni fisadi..ni shauri lako lazima uogope. Kama umezoe kutoa kanga na kimpumu/komoni kwa wapiga kura masikini.....lazima ujue Baba askofu means business against you!

Mfano: Mimi kama mkatoliki..sijaambiwa nani nimpigie kura..hilo ni swala langu..kwamba wanaingilia uhuru wangu..mimi na askofu wangu ndo tunajuana..kama ananidanganya au la.. Serikali inabidi iamke..hata hawa maaskofu ni wananchi kama mimi na wewe..wana wajibu wa kupambana na uovu na uzandiki na dhuruma kama wewe na mimi. Tumejaribu vyama vya siasa..wameshindwa..tumejaribu NGOs..wameshindwa, tumejaribu pressure za wafadhili hakuna kitu.....sasa twende wapi? Ngoja labda kanisa lijaribu kutoa elimu ya uraia..watu waamke.

Infact kuna NGOs kibao wanategemea kupata millions kutoka kwa wafadhili "kupeleka elimu ya kupiga kura vijijini" lakini ukweli ni deal la kula tuu..sasa kanisa litafanya hivi kwa kutumia network zake...lazima watu waogope..ulaji wa NGOs umetishiwa..na serikali inajua kabisa kanisa lina ushawishi mkubwa..And wait a minute...CCM hii hii..inatumia network za nyumba kumi kumi..kuwaumiza upinzani..sasa na kanisa litatumia network hizi hizi..kuwaonyesha wanachi ni jinsi gani serikali ilivyo out of touch na maisha yao...

Hizi hoja kwamba kanisa na siasa ni tofauti ni hoja mfu...kanisa halijatwambia sisi waumini tumpigie kura nani (kwa nini sisi hatuna akili zetu?)..bali linajaribu kutupa mwanga..ni mambo gani tunayastahili na tutayapataje..kwa kuchagua viongozi bora! Tawala zote za kiimla na kigaidi ..ziliondolewa kwa nguvu ya kanisa..Poland (Papa Yohana alisaidia), South Africa..mpaka askofu Tutu kapewa Nobel.....kwa kupinga utawala dhalimu wa makaburu. Leo Kilaini anakemea ufisadi (ambao ni silent killer) tunasema asichanganye siasa na dini? Are we real?

Hapa hakuna swala la dini wala siasa..Infact ingekuwa vyema hata waislamu, wapagani nk wangeweka miongozo yao kwa waumini wao.....as long as inatoa mwanga, elimu na vigezo vya kuchagua viongozi wanaotufaa. Tungepata maendeleo ya haraka sana.

Tatizo wote wanaopinga na kuuona huu waraka kama adui..ni kwa sababu wanahofia nguvu na ushawishi wa kanisa...wamezoea vya bure na kuwarubuni wananchi wasioelewa..(wanaelewa lakini kwa sababu ya umasikini akili inapotea)..sasa wakitokea watu wenye uchungu wa taifa letu wa kweli kuwaelewesha..wataitwa vibaraka, wahuni..na majina kibao. Ultimately ufinyu wa mawazo yetu ndo unatufanya kuendelea kuchagua viongozi wale wale..tukitegemea mabadiliko..FMES kila siku anasema hapa..."viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe.." sasa kanisa linataka ku-challenge huu usemi!

Na I can assure you, kanisa litawaamsha wananchi..kuhusu haki zao. Sasa ni wajibu wa serikali..either iwe responsible kwenye shughuli zake..au wawe tayari kupambana na akina Kilaini na Pengo. HABARI NDIYO HIYO.

Waumini tunausubiri huo waraka kwa hamu sana kwenye jumuiya zetu!

Masanja,

Bravo Masanja nadhani umesummarize vizuri hoja hii, it is only and only those who have personal agenda in reflexion to what benefits them individually ndio wanaona waraka huu kama tishio. And this tells me kumbe kuna watu wanafurahia au kuunga mkono jambo jema iwapo tu kuna alignment na dini yake, kabila lake au region yake. This is very low and is what brought our country to where we are now
 
Mimi nadhani kama watu tungetumia nafasi japo dakika chache kuusoma waraka wenyewe kipengele kwa kipengele tungeona nini kinachokusudiwa na waraka huu. Tatizo linaonekana kuwa umetolewa na taasisi ya dini, basi tunaegemea huko huko.
Waraka umesema mambo mengi, ambayo yote yanaonekana ni mapungufu yaliyotokea na yanayoendelea kutokea katika serikali au wananchi au taasisi hizi zenyewe. Sasa waendelee kukaa kimya?

Nimependa hitimisho lao:
"Naam, nchi ina utajiri mkubwa wa rasilimali na utaalam, na pia kuna fursa nyingi ambazo hazijatumika. Na bado nchi ina vikwazo vingi vya kiurasimu ambavyo huruhusu wachache kunyonya kwa faida yao binafsi. Tunahitaji kuweka mfumo wa kuweka mikakati na kuanzisha chombo cha kujitoa kweli katika kuhamasisha na kulinda manufaa kwa wote na mafanikio mazuri kabisa kwa ajili ya urithi wa kitaifa."
 
Msambya hajawatendea haki wananchi wa tz kwa ku conclude kihuni vile bungeni.

Ukisoma muongozo na ilani yao unajifunza mengi ya maana kwa mustakabali wa nchi yetu.

Pengine angelilenga directly kwenye issue ya oic na kadhi ilivyozungumzwa mle ktk ilani, lakini hata hiyo nayo wao wameamua kuwa wakweli na wawazi juu ya kile wanachokipenda na wasichokipenda tena in writtings, ni suala la serikali kuchagua kuwasikiliza au kutowasikiliza.
Nawasilisha
 
Wao kama Kanisa wameona ni muhimu kutoa elimu ya uraia pamoja na masuala ya kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu ambao ni haki ya kila raia kuchagua kiongozi anayeonekana anafaa. Kinachoonekana na wengine ni kama nia ya kuwapokonya vyeo vyao na ajenda imechukuliwa tofauti kabisa. Suala hapa liko wazi kabisa sasa naona watu wameiweka katika masuala ya kidini of which I think is inferiority complex ya baadhi ya watu ambao wanatoa expressions zao katika kuegemea udini. Mimi sitaki nielekee huko isipokuwa Kanisa ni Institution na Kanisa Katoliki lina waumini wengi ambao kama raia wa Tanzania wanayo haki ya kujua umuhimu wa uchaguzi mkuu na kiongozi gani anayefaa. Kama wewe umeshindwa kuongoza unataka nini? Unakuja na hoja ooh kanisa linaingilia masuala ya siasa mbona huyo aliyeropoka na kusema mwakani hatuichagui CCM hamshambulii. Yeye ana hoja gani ya msingi au ni Mahakama ya Kadhi ? Na masuala mengine ya kihistoria ambayo hata mtu akitafakari kwa makini ni kama njama ya kulipizana visasi baina ya dini moja yenye dola dhidi ya nyingine. Hizi propaganda za Misikitini tusizilete hapa JF. Wengine wanaenda misikitini kufundishana karate, Judo na Kungfu ili iweje? Muje kuwapiga Wakristo? Hasira za Mwembe Chai? Au ni kuhusu Nyerere kuwanyima elimu Kama inavyokuzwa wakati hakuna ukweli wowote. Tanzania ni nchi ya amani lakini sasa naona inafikia wakati watu tutakuja kukatana mapanga kwa misingi ya kidini na hii sumu inaanza kuota mizizi. Ni mbaya sana itatuletea matatizo na ndio maana Nyerere aligundua mapema. Leo hii wanamwandama Chikawe eti kisa kasema serikali haina dini. Wana nia gani? Mimi siamini kama kuna ajenda ya amani . Huwezi kuongoza nchi kwa kufuata mapendekezo ya Waislamu, Wakristo , Wabudha, Wa Zionist kwa sababu nchi haijengwi kwa misingi hiyo . Nchi inajengwa kwa kujituma na kuchapa kazi. Ndio maana Karl Marx alisema kuwa "Religion is an Opium of the People". Sote tumwabudu MUNGU kwa namna na jinsi zetu tusikwazane tujenge hoja za msingi tusianza kujenga hoja za kulipizana visasi kwa kigezo cha kihistoria ambacho mimi sidhani kama kina ajenda yoyote ya amani katika nchi yetu ya Tanzania. Samahani kama nitakuwa nimemkwaza Muislamu humu ndani ama Mkristo kwa matamshi yangu lakini mimi ninachoona Kama kanisa Katoliki limeamua kutoa mafunzo kwa waumini wake basi na wengine wafanye hivyo kwa kulingana na mafundisho yao na sio kuupotosha umma kwa kigezo cha kidini.
 
Kanisa Katoliki nchini latishwa

Mwandishi wa Raia Mwema​
Julai 8, 2009


.Wao waendelea na uhamasishaji 2009-2011

KUNA habari kwamba Kanisa Katoliki Tanzania limepata vitisho kutoka sehemu mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kutoka kwa watu wazito ndani ya dola kutokana na mkakati wake wa kuwaandaa waumini wake kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, Raia Mwema limefahamishwa.
Habari za uhakika zilizothibitishwa na vyanzo mbalimbali vya kanisa hilo na serikalini zimeeleza kwamba, vitisho hivyo ambavyo vimewasilishwa katika utaratibu usio rasmi, vimelenga ‘kulikumbusha’ kanisa hilo lenye nguvu kubwa nchini kwamba kuna vyombo vyenye nguvu kuliko kanisa hilo nchini.
Ofisa Mwandamizi wa Serikali amelithibitishia Raia Mwema kwamba kitisho hicho kimelenga kujaribu kuzuia athari za nyaraka zilizoandaliwa na Kanisa Katoliki na kusambazwa nchi nzima, zikiwa kwa kiasi kikubwa zinakosoa mfumo wa sasa wa serikali na chama tawala cha CCM.
“Unajua mumeanza kuandika haya mambo wakati tayari yalikwisha kuwa yamesambaa nchi nzima kwa waumini wote na programu ilikuwa imeanza kutekelezwa katika ngazi ya chini kabisa ya kanisa, hata serikali ilikwisha kujua na kuwatisha kuwaambia kwamba dola ina mkono mrefu,” anasema mtoa habari wetu aliye karibu na pande zote husika, serikali na Kanisa Katoliki.
Habari zaidi zinaeleza kwamba, hata suala la ‘kutikisa kiberiti’ kuhusiana na kuondoa misamaha ya kodi kwa taasisi za dini, ilikuwa ni mkakati mahususi wa kuwavuta viongozi wa dini waiangukie serikali na ‘kujitia kitanzi’ lakini baadhi ya Maaskofu walielezwa kushitukia mpango huo wa serikali na kukataa kuibembeleza.
“Unajua hata suala la kutufutia misamaha ilikuwa ni mbinu ya kutaka twende tukaiangukie serikali ili sasa tuwe tume-compromise na hivyo kulegeza kamba na kuanza kuimba nyimbo wanazotaka wao. Wakubwa zetu wakashituka na kukataa pamoja na kuwa baadhi walianza kulainika na kutaka tukawabembeleze,” anasema kiongozi mmoja wa dini ambaye anahusika katika mchakato wa maandalizi ya waumini kuelekea 2010.
Raia Mwema lilishindwa kuwapata viongozi wa juu wa Kanisa Katoliki jana Jumanne baada ya kuelezwa kwamba viongozi hao walikuwa katika misa maalumu ya upadirisho iliyochukua karibu siku nzima ya jana jijini Dar es Salaam.
Wakati hayo yakiendelea, Kanisa hilo tayari limeanza utekelezaji wa programu yake tokea Januari mwaka huu inayoishia mwaka 2011, ikiwa na lengo la kuwaandaa waumini wake kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na baadaye tathmini yake baada ya uchaguzi huo.
Likielezea umuhimu wa programu hiyo, Kanisa Katoliki limesema;
“Watu wengi wanadhani kwamba mambo ya umma sio sehemu ya majukumu yetu ya kidini na kiimani, na hivyo Kanisa halipaswi kujishughulisha na mambo hayo. Kinyume chake Kristo anatualika kuleta mafundisho ya Mungu, maadili ya asili yetu ya kibinadamu kama tulivyoumbwa na Mungu. Tunaalikwa kuyafanya hayo yawe ndio msingi na mwanga unaoongoza maamuzi na sera zetu.”
“Katika miaka ya hivi karibuni sote tumeshuhudia haya yakitokea na tumepata madhara yake katika amani na utulivu katika taifa letu. Kumekuwa na mgawanyiko miongoni mwetu, kumejengeka matabaka ya wenye mali nyingi na watu wengi ambao wana mali kidogo sana, maskini na fukara hasa . Mwelekeo huu unatishia na kuhatarisha amani na moyo wa ujamaa tuliokuwa nao na kushamiri kwa utengano na chuki kati yetu..”
Imeelezwa katika programu hiyo ya kichungaji kwamba kumeandaliwa hatua madhubuti za ufuatiliaji ambao utaanzia kwa kufanyika mikutano ya makleri na viongozi wa halmashuri walei kujadiliwa katika ngazi ya Jimbo na kupewa umuhimu unaostahili.
“Katika kazi ya kuongoza mkutano wajumbe wa CPT (Wanataaluma Wakristo) na wawakilishi wa Serikali waalikwe kutoa maelezo juu ya hali halisi pale watu wanamoishi. Inapendekezwa paundwe timu ya Jimbo kwa ajili ya ufuatiliaji wa programu hii. Katika ngazi ya Parokia programu ilenge kufundisha wanavijiji/watu mitaani na katika jumuiya ndogo ndogo ili waweze kujadili masuala yaliyomo katika programu,” inaeleza sehemu ya waraka huo wa kichungaji.
Sehemu ya mkakati inaeleza kwamba ripoti za majadiliano katika vikao hivyo zitumwe Parokiani (Paroko na Halmashauri) kila baada ya miezi mitatu zikionyesha mambo yaliyojadiliwa na maamuzi yaliyofikiwa.
Maelekezo ya yaliyotolewa kwa kuzingatia mada zilizojadiliwa katika mkutano wa Wakurugenzi wa Kichungaji na Wajumbe wa Tume ya Haki na Amani (TEC) yanalenga kugusia vipaumbele kwa mujibu wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii.
Mambo mengine ni umuhimu wa uongozi wenye maadili katika kuleta mabadiliko ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kidini katika Tanzania; mfumo wa sheria Tanzania ( Nguvu na Changamoto); haki za binadamu katika sera za biashara na fedha; mtazamo wa kimaadili katika mfumo wa kisiasa na kiuchumi na hifadhi ya jamii.
Pamoja na uongozi wa juu wa Kanisa kueleza kwamba hii si mara ya kwanza kwa Kanisa Katoliki kuandaa waraka wa kuongoza waumini wake na wananchi kuhusiana na mambo muhimu, hatua ya mwaka huu imeelezwa si ya kawaida na inaashiria kuwapo kwa ombwe (vacuum ) kubwa katika mfumo wa kiuongozi na kijamii.

Source:Kanisa Katoliki nchini latishwa

hs3.gif
 
Mpango huu wa maaskofu ni pedagogi ya ukombozi kwa wote

lC.gif
Deusdedit Jovin​
Julai 8, 2009
rC.jpg

NIMEFURAHISHWA na "Mpango wa Kichungaji Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010" kama ulivyoandaliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kwa kusaidiana na Chama cha Wanataaluma Katoliki Tanzania (CPT); kiasi kwamba nimeshawishika kuandika makala kuwahamasisha Watanzania wa dini zote kuunga mkono mpango huo kwani ndiyo ukombozi wa nchi yetu.
Wakiwa wanatimiza wajibu wao wa ‘kufundisha', ‘kuongoza' na ‘kutakatifuza' jamii kwa mawazo, kwa maneno na kwa vitendo, kama wanavyoagizwa na Katiba ya Kanisa Katoliki kuhusu majukumu ya ulei, upadre na uaskofu (Lumen Gentium 1965), wajumbe wa Mkutano wa Wakurugenzi wa Kichungaji na Wajumbe wa Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), waliamua kuchapisha na kusambaza, sio "Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2010" kama vyombo vya habari vilivyoripoti kimakosa, bali "Ilani (ya) Mapendekezo ya Vipaumbele vya Kitaifa" kwa ajili ya kufanikisha "Mpango wa kichungaji kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010".
Mpango huo unatekelezwa kwa kuzingatia mafundisho rasmi ya Kanisa Katoliki kuhusu haki za binadamu wote.
Hata hivyo, pamoja na ukweli huu ulio wazi, uamuzi wa maaskofu Katoliki umekumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa baadhi ya Watanzania. Upinzani huo, kwa sehemu kubwa, unatokana na baadhi ya wachambuzi ama kujikwaa kwenye kisiki kiitwacho argumenum adhomin au kuamua kukipiga teke kisiki hiki kwa makusudi.
Yote mawili yana matokeo yaleyale; yaani kumhakiki mtoa hoja badala ya kuihakiki hoja iliyowekwa ulingoni. Hivyo, kwa maoni yangu, ni muhimu kuweka bayana hoja ya Kanisa Katoliki na mazingira yanayoizunguka ili tuweze kuitendea haki.
"Ilani (ya) Mapendekezo ya Vipaumbele vya Kitaifa" ni waraka unaofafanua kwa lugha nyepesi jozi za maneno kama vile uhai na kifo, uhuru na utumwa, wema na ubaya, ukweli na uwongo, unafiki na uwazi, elimu na ujinga, afya na ugonjwa, uadilifu na uhalifu, haki na dhuluma, utajiri na umaskini.
Maneno kama vile ubinadamu na uhayawani, kichocheo na matokeo, umakini na usanii, utajiri na umaskini, maendeleo na utapia-maendeleo, kiumbe na muumba, kiwa na ombwe, na jozi za maneno mengine yanayopigana kisogo mithili ya usiku na mchana (conceptual dichotomies).
Umuhimu wa hizi jozi za mawazo yanayopigana kisogo ni kwamba huwawezesha wanadamu kutazama na kuona yanayowazunguka, kusaili waliyoyaona ili kubainisha tatizo lililopo, kusanifu haipotesia zinazoonyesha mapendekezo ya chimbuko la tatizo na dawa yake, kufanya utafiti ili kuthibitisha au kubatilisha haipotesia hizo, kutoa hukumu kwa msingi wa matokeo ya utafiti, kuchukua hatua za kivitendo kwa ajili ya kutatua tatizo husika, na hatimaye kupima matokeo ya matendo yao mara kwa mara kwa ajili ya uboreshaji.
Kwa mfano, ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha baadhi ya viongozi wa taifa la Uingereza kuona kwamba utawala wa kifalme ulikuwa unakiuka utu wa binadamu, na hivyo kuhitimisha kwamba lilikuwa ni tatizo linalopaswa kutatuliwa ambapo walionyesha njia ya kulitatua kupitia matamko mbalimbali ya haki za binadamu ikiwa ni pamoja na "Magna Carta" (1215), "Habeas Corpus" (1679), na "Bill of Rights" (1689).
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha waasisi wa taifa la Marekani kuona kwamba ukoloni wa Kiingereza ulikuwa unakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalopaswa kutatuliwa na hatimaye wakaonyesha njia ya kulitatua kupitia Tangazo la Uhuru wa Marekani (The Declaration of Independence (1776), tamko ambalo lilisisitiza "uhai, uhuru na furaha" kama haki za msingi kwa kila binadamu.
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha waasisi wa Jamhuri ya Kikatiba ya Ufaransa kuona kwamba utawala wa kifalme ulikuwa unakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalopaswa kutatuliwa na hatimaye wakaonyesha njia ya kulitatua kupitia Matamko ya Haki za Raia wa Ufaransa na Binadamu Wote (Declaration of the Rights of Man and of the Citizen (1789/1793), matamko ambayo yanasisitiza "udugu, uhuru na mali" kama haki za msingi kwa kila binadamu.
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha Karl Marx wa Ujerumani na mwenzake Friedrich Angels wa Urusi kuona kuwa mahusiano kati ya mwajiri na mwajiriwa wakati wa enzi za Mapinduzi ya Viwanda yalikuwa yanakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalohitaji kutatuliwa hatimaye walionyesha njia ya kulitatua tatizo hili kupitia kijitabu chao kiitwacho "Ilani ya Ukombozi kwa Mtazamo wa Kikomunisti" (The Communist Manifesto (1848)).
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha viongozi mbalimbali wa mataifa ya ulimwengu kuona kwamba vita kuu ya kwanza na vita kuu ya pili ya dunia ilikuwa ni mifano tosha kuonyesha kuwa utemi wa kijeshi unakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalopaswa kutatuliwa na hatimaye kuonyesha njia ya kulitatua kupitia kitabu chake kiitwacho "Sisi ni Watumwa Ndani ya Nchi Yetu" (The Universal Declaration of Human Rights (1948)).
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizomwezesha Frantz Fanon wa Algeria kuona kwamba ukoloni nchini mwake ulikuwa unakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalopaswa kutatuliwa na hatimaye kuonyesha njia ya kulitatua kupitia kitabu chake kiitwacho "Sisi ni Watumwa Ndani ya Nchi Yetu" (The Wretched of the Earth (1961)) ambapo anasisitiza haki ya taifa kujitawala katika nyanja zote za maisha.
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha wajumbe wa Mtaguso wa Pili wa Vatikano kuona kwamba baadhi ya mapokeo ya Kikatoliki yalikuwa yanakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalopaswa kutatuliwa na hatimaye kuonyesha njia ya kulitatua kupitia "Katiba ya Kanisa Katoliki Kuhusu Jukumu la Kukuza na Kuhami Haki za Binadamu" (Gaudium et Spes 1965)).
Haki zote za Binadamu kama zinavyopatikana katika Tangazo la Dunia Kuhusu Haki za Binadamu zimeingizwa katika katiba hii.
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizomwezesha Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere kuona kwamba kasumba za kikoloni nchini mwetu zilikuwa zinakiuka utu wa binadamu, na hivyo tatizo linalopaswa kutatuliwa na hatimaye kuonyesha njia ya kulitatua kupitia "Azimio la Arusha" (The Arusha Declaration 1967), azimio linalotaja vipaumbele vya kitaifa kuwa ni mapambano dhidi ya umaskini, ugonjwa, ujinga na maradhi.
Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizomwezesha Paul Freire wa Brazil kuona kwamba mfumo wa elimu unaomfanya mwanafunzi aenende kama roboti (banking system of education) ni kiini cha udumavu wa kimawazo ulio na madhara makubwa sana kwa uhai wa taifa la kesho, na hatimaye akaonyesha njia ya kulitatua kupitia kitabu chake kiitwacho "Pedagogi ya Ukombozi" (Pedagogy of the Oppressed 1969)), uamuzi ambao ulimfanya aitwe, sio mkandamizaji, bali mkombozi.
Aidha, ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizowawezesha Watanzania walioshiriki katika kuandaa Katiba yetu ya mwaka 1977 kuona kwamba kuna haja ya kuzitambua rasmi, kuliko ilivyokuwa hukonyuma, haki za binadamu, na hatimaye kuonyesha njia ya kulitatua kupitia marekebisho yaliyoziingiza haki za binadamu ndani ya katiba hiyo.
Katika katiba yetu kwenye Ibara ya 12 hadi ibara ya 24 zinaorodheshwa haki muhimu za kila Mtanzania kwa mujibu wa Tangazo la Dunia Kuhusu Haki za Binadamu. Tangazo hilo lilikubaliwa na kutiwa saini na Serikali ya Tanzania mara tu baada ya uhuru mwaka 1961.

Ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizomwezesha Enrique Dussel wa Argentina kuona kwamba baadhi ya mawazo yanayopenyezwa katika ulimwengu wa tatu kutoka katika ulimwengu wa kwanza ni kutu ya kimawazo (ideological contamination) inayopaswa kutatuliwa na hatimaye akaonyesha njia ya kulitatua tatizo hilo kupitia kitabu chake kiitwacho "Falsafa ya Ukombozi" (A Philosophy of Liberation 1985).
Na hatimaye ni jozi za mawazo yanayopigana kisogo zilizoliwezesha vilevile Kanisa Katoliki Tanzania kuona kwamba kuna ukosefu wa "vipaumbele vya kitaifa" nchini, na hatimaye wakaonyesha njia ya kulitatua kupitia vijitabu vitatu vinavyojulikana kama: "Mpango wa Kichungaji Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010", "Ilani (ya) Mapendekezo ya Vipaumbele vya Kitaifa", na "Mada za Kuongoza Maandalizi ya Uchaguzi Mkuu 2010".
Kwa ufupi basi, niseme kwamba historia hii pana inaonyesha mambo mawili makubwa. Mosi, inaonyesha ukweli kwamba kukiuka utu wa binadamu (human dignity) ni jambo lisilokubalika sehemu yoyote duniani. Na pili inaonyesha ukweli kwamba njia bora zaidi ya kukuza na kuhami utu wa binadamu tajwa ni kukuza na kuhami haki za binadamu wote bila kujali upekee wao kwa misingi ya vigezo vya kinasibu kama vile dini, jinsia, umri, uzito, urefu, rangi, kabila, au itikadi za kisiasa.
Katika muktadha huu, nimevisoma vijitabu vyote vilivyotolewa na Kanisa Katoliki ili nijiridhishe kwamba wamezingatia mambo haya mawili. Na sasa naweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba haki zote za binadamu zimezingatiwa. Hakuna mahali popote ambapo Kanisa Katoliki limependekeza ama kudumaza au kutelekeza haki yoyote ya binadamu.
Kimsingi, bila kuathiri haki yoyote ya binadamu, Mpango wa Maaskofu Katoliki Tanzania unapendekeza orodha ya haki za binadamu ambazo, kwa maoni yao, zinapaswa kuchukuliwa kama "vipaumbele vya kitaifa".
Kwa hiyo, ninalazimika kuhitimisha makala yangu kwa kusema kwamba Maaskofu Katoliki Tanzania wamechagua fungu lililo bora kwa binadamu wote wa Tanzania.
Anayekataa ukweli huu ama atakuwa anashindwa kutofautisha kati ya hoja na mtoa hoja au atakuwa anakanusha upita-mipaka wa utu wa binadamu (universality of human dignity).
Katika hilo la kwanza, tutalazimika kumpuuza mtu huyo; maana atakuwa amechagua kufanya utovu wa nidhamu ya kitaaluma. Na katika lile la pili, mtu wa aina hiyo atakuwa anatukuza utabaka kwa msingi wa vigezo vya kinasibu (specificity of human persons). Watu wa aina hii watakuwa wanaipinga katiba ya Tanzania na hivyo watu wa kuogopwa kama ukoma!
hs3.gif

Mpango huu wa maaskofu ni pedagogi ya ukombozi kwa wote

Simu:
0734 800808​
 
Kwani ni SIRI,

Kuna watu wametumwa humu kuja kushambilia DINI za watu.
Na wengine wametumwa kuja KUTETEA UFISADI.
Na kuna wengine wachache ni Wakorofi tu wanaojifanya wao ni SAMAKI kwa siku zote kwenda AGAINST the streams. Mkimpinga yeye anafurahii na kuja kurusha makombora zaidi ya kutetea huo ukorofi wake.
Huyu dawa yake na wewe mjibu kikorofi, utagundua. Akijibu matusi ujuwe KATUMWA huyo (kama Tumain na MaxShimba). Akianza kutetea maelezo yake na kuyachambua zaidi kwa kuunganisha points ili kuonyesha alikuwa na lengo zuri, basi fahamu ni MKOROFI (mfano hai ni Dilunga, Masatu na Game Theory, Shy). Hapo huwepo watu kama Yo Yo, Nyani Ngabu, MkamaP na wengine kushabikia, Mpe huyoo mpe huyoo.....

Washambuliwaji wakubwa humu ni Mwanakijiji na FMes. Wazee wa busara ni akina Mtanzania, Kichuguu, Mkandara, Mkumbo nk nk.

Kwa ufupi JF kweli imekuwa JAMII.
 
CCM na viongozi wao na hata Serikali JK na uzoefu wake wote wa kuwa madarakai anasahau kwamba wakatoliki ndiyo wamekuwa walinzi wa Nchi hii kwa miaka mingi.Nikiwa na maana kwamba kuanzia Usalama wa Taifa na kwingineko , akina Membe Mseminary , Pinda Mseminary , Mkapa Mseminary na wako wengi kwenye system na hivyo kufanya uhalifu dhidi ya kanisa katoliki si rahisi na hawa watu wote wako very royal kwa uongozi wa Kanisa katoliki.Kumbe ile misaada ilikuwa tisha toto sasa mbona kuna kuumbuka mtu hapa ?

Mkono means what ? Umkamate Kilaini ama Pengo au uvunje makanisa ?
 
Kwani ni SIRI,

Kuna watu wametumwa humu kuja kushambilia DINI za watu.
Na wengine wametumwa kuja KUTETEA UFISADI.
Na kuna wengine wachache ni Wakorofi tu wanaojifanya wao ni SAMAKI kwa siku zote kwenda AGAINST the streams. Mkimpinga yeye anafurahii na kuja kurusha makombora zaidi ya kutetea huo ukorofi wake.
Huyu dawa yake na wewe mjibu kikorofi, utagundua. Akijibu matusi ujuwe KATUMWA huyo (kama Tumain na MaxShimba). Akianza kutetea maelezo yake na kuyachambua zaidi kwa kuunganisha points ili kuonyesha alikuwa na lengo zuri, basi fahamu ni MKOROFI (mfano hai ni Dilunga, Masatu na Game Theory, Shy). Hapo huwepo watu kama Yo Yo, Nyani Ngabu, MkamaP na wengine kushabikia, Mpe huyoo mpe huyoo.....

Washambuliwaji wakubwa humu ni Mwanakijiji na FMes. Wazee wa busara ni akina Mtanzania, Kichuguu, Mkandara, Mkumbo nk nk.

Kwa ufupi JF kweli imekuwa JAMII.

Mkandara ana busara gani..?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom