Wapinzani wakivurugana wanafukuzana, CCM wakivurugana wanapatana na kuombana msamaha. Hii imekaaje?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,503
2,046
Wanabodi naomba mnisaidie kuelewa shida iko wapi, maana tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini, tumeshuhudia vyama tofautitofauti vya upinzani vikiibuka na kujipatia wafuasi wengi na hivyo na hivyo kuwa tishio kwa chama tawala.

Kwa kumbukumbu zangu ni kwamba ilianza nccr mageuzi ilipata umaarufu mkubwa sana siku za mrema na kutoa ushindani mkali sana kwa ccm hasa kwenye uchaguzi wa 1995.

Baada ya hapo ulizuka mgogoro mkubwa sana ndani ya chama hicho ambapo viongozi wakuu waliishia kuvurugana na kufukuzana na kukiumiza sana chama na kukiondoa kwenye ramani ya siasa za ushindani.

Ndipo ikafuata zamu ya cuf chini ya prof Lipumba na Maalim Seif, kama ilivyokua kwa nccr ingawa kwa huku bara cuf haikufikia ile nguvu ya nccr ya Mrema lakini taratibu ilianza mizozo ya ndani ambayo nayo haikuiacha CUF salama.

Kilele cha CUF kuvurugana tulikishuhudia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo mambo yaliyotokea yameifanya cuf isiaminike tena. Maana viongozi wakuu walivurugana na kufukuzana.

Kwa upande wa chadema ingawa walikuwa na nguvu za waziwazi tangia 2010, lakini pia wao hawakuwa na kinga dhidi ya hii changamoto ya kuvurugana maana tulishuhudia baada ya kumpokea lowasa chamani katibu mkuu alisusa na baada ya hapo tumeshuhudia matukio mengi ya fukuzafukuza ndani ya chama.

Ila kinachonishangaza ni kwamba ccm ina wanachama wengi sana, na mara kadhaa wamekua wakitifautiana kauli na mitazamo hata hivyo wao huitana kuombana msamaha na makaripio na maisha kuendelea.

Ni kwa nini wapinzani ni ngumu kumaliza tofauti zao kwa kusameheana na kuruhusu maisha yaendelee!?
 
Wanabodi naomba mnisaidie kuelewa shida iko wapi, maana tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini, tumeshuhudia vyama tofautitofauti vya upinzani vikiibuka na kujipatia wafuasi wengi na hivyo na hivyo kuwa tishio kwa chama tawala.

Kwa kumbukumbu zangu ni kwamba ilianza nccr mageuzi ilipata umaarufu mkubwa sana siku za mrema na kutoa ushindani mkali sana kwa ccm hasa kwenye uchaguzi wa 1995.

Baada ya hapo ulizuka mgogoro mkubwa sana ndani ya chama hicho ambapo viongozi wakuu waliishia kuvurugana na kufukuzana na kukiumiza sana chama na kukiondoa kwenye ramani ya siasa za ushindani.

Ndipo ikafuata zamu ya cuf chini ya prof Lipumba na Maalim Seif, kama ilivyokua kwa nccr ingawa kwa huku bara cuf haikufikia ile nguvu ya nccr ya Mrema lakini taratibu ilianza mizozo ya ndani ambayo nayo haikuiacha cuf salama.
Kilele cha cuf kuvurugana tulikishuhudia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo mambo yaliyotokea yameifanya cuf isiaminike tena. Maana viongozi wakuu walivurugana na kufukuzana.

Kwa upande wa chadema ingawa walikuwa na nguvu za waziwazi tangia 2010, lakini pia wao hawakuwa na kinga dhidi ya hii changamoto ya kuvurugana maana tulishuhudia baada ya kumpokea lowasa chamani katibu mkuu alisusa na baada ya hapo tumeshuhudia matukio mengi ya fukuzafukuza ndani ya chama.

Ila kinachonishangaza ni kwamba ccm ina wanachama wengi sana, na mara kadhaa wamekua wakitifautiana kauli na mitazamo hata hivyo wao huitana kuombana msamaha na makaripio na maisha kuendelea.

Ni kwa nini wapinzani ni ngumu kumaliza tofauti zao kwa kusameheana na kuruhusu maisha yaendelee!?
Ukweli ni kwamba hata CCM wanafukuzana mfano Sophia Simba. Kuombana msamaha na kusameheana ni kwa sababu CCM kuna keki ya taifa inayoliwa ambayo ni vigumu kuiacha. Kama si hiyo keki akina January Makamba, Nape, mzee Makamba, mzee Kinana, Ngeleja na wengine wasingepiga magoti na kusamehewa. KEKI TAMU.
 
Wanabodi naomba mnisaidie kuelewa shida iko wapi, maana tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini, tumeshuhudia vyama tofautitofauti vya upinzani vikiibuka na kujipatia wafuasi wengi na hivyo na hivyo kuwa tishio kwa chama tawala.

Kwa kumbukumbu zangu ni kwamba ilianza nccr mageuzi ilipata umaarufu mkubwa sana siku za mrema na kutoa ushindani mkali sana kwa ccm hasa kwenye uchaguzi wa 1995.

Baada ya hapo ulizuka mgogoro mkubwa sana ndani ya chama hicho ambapo viongozi wakuu waliishia kuvurugana na kufukuzana na kukiumiza sana chama na kukiondoa kwenye ramani ya siasa za ushindani.

Ndipo ikafuata zamu ya cuf chini ya prof Lipumba na Maalim Seif, kama ilivyokua kwa nccr ingawa kwa huku bara cuf haikufikia ile nguvu ya nccr ya Mrema lakini taratibu ilianza mizozo ya ndani ambayo nayo haikuiacha cuf salama.
Kilele cha cuf kuvurugana tulikishuhudia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo mambo yaliyotokea yameifanya cuf isiaminike tena. Maana viongozi wakuu walivurugana na kufukuzana.

Kwa upande wa chadema ingawa walikuwa na nguvu za waziwazi tangia 2010, lakini pia wao hawakuwa na kinga dhidi ya hii changamoto ya kuvurugana maana tulishuhudia baada ya kumpokea lowasa chamani katibu mkuu alisusa na baada ya hapo tumeshuhudia matukio mengi ya fukuzafukuza ndani ya chama.

Ila kinachonishangaza ni kwamba ccm ina wanachama wengi sana, na mara kadhaa wamekua wakitifautiana kauli na mitazamo hata hivyo wao huitana kuombana msamaha na makaripio na maisha kuendelea.

Ni kwa nini wapinzani ni ngumu kumaliza tofauti zao kwa kusameheana na kuruhusu maisha yaendelee!?
kwa sababu kuna wanafiki nawakweli hivyo sirahisi wakakaa pamoja,naukiona watu wanagombana kwa hoja kisha wanasema tumeyamaliza ujue mipango yao nimimoja wanachopishana ninjia tu! Utajuaje ? Angalia kati yawana ccm katafute kauli zake za kipindi cha maraisi kikwete,magufuli na sasa samia,hakuna mwenye kauli moja sasa watu kama hawa kwanini washindwe kumaliza tofauti zao?
 
... hao wanaofukuzwa upinzani ni wapizani? Mapandikizi yakishtukiwa hamna alternative ndugu ima yatimuliwe au yajiondokee yenyewe like Covid-19.
 
CCM ukivuruga au kuvurugwa wanakushughulikia .Watu waliovuruga /vurugwa wanakuwa hawana namna zaidi ya kurudi na kupiga magoti.Vinginevyo unapotezwa kimaslahi au Hata kimaisha Kwa ujumla wake!
 
Madaraka ndio yanawafanya waonekane wamoja.nje ya madaraka CCm hakuna Maisha.
Siku ccm ikitolewa madarakani ndio utajua kama ccm Wana umoja wa kuombana samahani.
Rejea kANU ya kenya.
Chadema ni chama halisia.hawana madaraka,hawana hela lakini chama kinazidi kusonga Mbele.
Haswaaaa!!Ulaji na maslahi lakini pia upinzani ni kujitoa muhanga wakati ndani ya CCM kula kuku kwa mrija.
 
ukiindoa keki ya taifa ccm hawana umoja wala nini, tizama wanachomfanyia jiwe kwa sasa kisha ulinganishe na walivyoimba mapambio alipokua hai ndo utajua vile maccm walivo mashetani.
 
Wote wezi hakuna wakumnyooshea kidole kwa ukali mwenzake. Ukijifanya mkali watu wanaweka faili lako mezani, halafu unaulizwa eeenhhh....what next? Ndio maana wanaridhiana kinafki na kukubalian kulindana(hichi kwao ndio kiapo kikubwa sana). Kula kwenye eneo lako tusiingiliane. Angalia nani na nani anapewa wizara nyeti au ukatibu mkuu kwenye wizara.
 
Madaraka ndio yanawafanya waonekane wamoja.nje ya madaraka CCm hakuna Maisha.
Siku ccm ikitolewa madarakani ndio utajua kama ccm Wana umoja wa kuombana samahani.
Rejea kANU ya kenya.
Chadema ni chama halisia.hawana madaraka,hawana hela lakini chama kinazidi kusonga Mbele.
Umeongea point. Mtu ameshika dola na Hana nidhamu utegemee ukishindana naye na ukashupaza shingo lazima akuvunje. Rejea ardhi ya Sumaye alivyohamia Chadema.
 
Wanabodi naomba mnisaidie kuelewa shida iko wapi, maana tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini, tumeshuhudia vyama tofautitofauti vya upinzani vikiibuka na kujipatia wafuasi wengi na hivyo na hivyo kuwa tishio kwa chama tawala.

Kwa kumbukumbu zangu ni kwamba ilianza nccr mageuzi ilipata umaarufu mkubwa sana siku za mrema na kutoa ushindani mkali sana kwa ccm hasa kwenye uchaguzi wa 1995.

Baada ya hapo ulizuka mgogoro mkubwa sana ndani ya chama hicho ambapo viongozi wakuu waliishia kuvurugana na kufukuzana na kukiumiza sana chama na kukiondoa kwenye ramani ya siasa za ushindani.

Ndipo ikafuata zamu ya cuf chini ya prof Lipumba na Maalim Seif, kama ilivyokua kwa nccr ingawa kwa huku bara cuf haikufikia ile nguvu ya nccr ya Mrema lakini taratibu ilianza mizozo ya ndani ambayo nayo haikuiacha CUF salama.

Kilele cha CUF kuvurugana tulikishuhudia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo mambo yaliyotokea yameifanya cuf isiaminike tena. Maana viongozi wakuu walivurugana na kufukuzana.

Kwa upande wa chadema ingawa walikuwa na nguvu za waziwazi tangia 2010, lakini pia wao hawakuwa na kinga dhidi ya hii changamoto ya kuvurugana maana tulishuhudia baada ya kumpokea lowasa chamani katibu mkuu alisusa na baada ya hapo tumeshuhudia matukio mengi ya fukuzafukuza ndani ya chama.

Ila kinachonishangaza ni kwamba ccm ina wanachama wengi sana, na mara kadhaa wamekua wakitifautiana kauli na mitazamo hata hivyo wao huitana kuombana msamaha na makaripio na maisha kuendelea.

Ni kwa nini wapinzani ni ngumu kumaliza tofauti zao kwa kusameheana na kuruhusu maisha yaendelee!?

Umoja wa CCM uko katika mlo, hata huko kusameheana sio kusameheana kwa sababu ya msamaha, bali ni kusameheana katika kulinda mlo. Siku CCM itatoka madarakani ndio utajua kiwango cha uhovyo wa CCM.
 
Back
Top Bottom