Wapi ulienda ukakuta ardhi bei ya kutupwa?

Wapi ulienda ukakuta ardhi bei ya kutupwa?

Mwaka 2022! Nilisafiri kwenda Lindi kikazi. Katika ile project tulikuwa tunazunguka wilayani na kwenye vijiji ndani ndani huko.

Nilikuja kufika sehemu Ruangwa kuna vijiji tulienda huko ardhi ni bei ya kutupwa.

Ekari inauzwa elf 10 hapa kama unanunua serikali ya kijiji (ukitaka nyingi)
Kama unataka chache moja au mbili wananchi wanauza elf20

Kweli Tanzania bado ardhi nyingi!
Mwika Kilimanjaro kuna ardhi inapatikana kwa bei ya kutupwa.
 
Bungu Kibiti Acre 1 = 400,000

Na hii ni bei ya makampuni ya wauza viwanja..

Pata picha bei ya wazawa atakuuzia bei gani
Bungu ipi kaka? Msoro? Nyamisati? Nyanjati? Mjawa? Au mahege?
Sema uzuri wa Kibiti maji kila sehemu yapo ni pazuri sana kwa kilimo
 
Kwanini Kisarawe haiendelei? Wilaya zote za Pwani zinakuwa kwa kasi kasoro Kisarawe! Kulikoni?
Kisarawe ni miongoni mwa Wilaya kongwe hapa nchini, tangia enzi za Utawala wa Muingereza.

Tatizo sijui liko wapi kwakweli. Ukifika Kisarawe centre pale utakutana na mji uliojichokea.

Kunahitajika juhudi za makusudi kutangaza fursa zake

K
 
kwa 300,000 unaweza kupata pori lililopimwa
Mkuu fika Manerumango ofisin ulizia sehemu inaitwa Konde kwa ofisini Kama una kiasi Cha milioni Tano wanakupa heka 50 ufanye kazi.

Hiyo laki tatu kwa heka ni kama unajua kwa mtu binafsi na kwa offer hiyo utapata mashamba mpaka ukimbie mwenyewe
 
kwa 300,000 unaweza kupata pori lililopimwa

Wacha kukaza fuvu njoo ofisin ya kijiji Manerumango muone mtendaji .
Utapewa pori lako la hekari 50 kwa milioni Tano tu. Joanah ardhi Ina rutuba dongo jeusiii mazao yote ya horticulture na cerial yanafanya vizuri sana

Kuna changamoto kidogo za ngedere
Ngedere sio changamoto ndogo Mkuu.
 
Mwaka 2022! Nilisafiri kwenda Lindi kikazi. Katika ile project tulikuwa tunazunguka wilayani na kwenye vijiji ndani ndani huko.

Nilikuja kufika sehemu Ruangwa kuna vijiji tulienda huko ardhi ni bei ya kutupwa.

Ekari inauzwa elf 10 hapa kama unanunua serikali ya kijiji (ukitaka nyingi)
Kama unataka chache moja au mbili wananchi wanauza elf20

Kweli Tanzania bado ardhi nyingi!
Mwanza
 
Back
Top Bottom