Wapi chuo cha teolojia cha walokole

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2017
Posts
3,868
Reaction score
5,160
Kwa uchunguzi wangu nimegundua kuna vyuo vinavyofundisha teolojia kwa madhehebu ya kiluteri mfano kiko Makumira Arusha.

Wakatoliki Kipalapala n.k.

Sijawahi sikia chuo cha teolojia cha walokole.

Hawa jamaa wanapiga kelele sana ilimradi mtu abarikiwe kujua kuongea.

Mbona YESU wakati analeta injili alikuwa hapigi kelele?
 
Kwa walokole kuwa na sauti ya zege + kujua vimistari vichache vya bibilia + kujua kukata mitama + kunywa pombe kwa kificho ni vigezo tosha kabisa.

Ukiwa na upara kwa basi waumini wanazidi kukuamini.

Ukiwa na hivyo vigezo basi utaitwa bonge la mchungaji.
 
Sio Yesu tu hata mimi huwa sipigi kelele. Huwa nafundisha na kuhubiri kwa utulivu ili wasikiao waelewe.

My declaration: Nimeokoka hivyo
Roho wa Mungu ndio chuo changu. Kazi ya Mungu inahitaji kuongozwa na Mungu mwenyewe na si vinginevyo!
 
Wanaropoka tu hawana elimu ya theolojia. Ni kukariri tu mistari kwa kwenda mbele.
 
unaposema chuo cha theolojia cha walokole kwani kuna dhehebu linaitwa walokole? lutheran/catholics ni dhehebu na ndiyo maana wana chuo chao sasa hilo dhehebu linaitwa la walokole lipo wapi Tanzania hii?
 
Dodoma karibu na chuo cha mipango
 
Vipo kuna pale kudiembe Chalinze,Dodoma na Temeke

TAG wanacho cha kwao
EAGT wanacho cha kwao
AIC wanacho cha kwao
FGBFS pia na n.k

USSR
 
Vipo kuna pale kudiembe Chalinze,Dodoma na Temeke

TAG wanacho cha kwao
EAGT wanacho cha kwao
AIC wanacho cha kwao
FGBFS pia na n.k

USSR
Ni taasisi zao zisizo rasmi tena Chalinze na Pwani wana vichuo njoo vingi sana.

Kingine AIC watoe kwenye kundi lao maana wao hujifunza thiolojia vyuo vya kawaida kama St John's dodoma n.k

Karibu tule makali
 
unaposema chuo cha theolojia cha walokole kwani kuna dhehebu linaitwa walokole? lutheran/catholics ni dhehebu na ndiyo maana wana chuo chao sasa hilo dhehebu linaitwa la walokole lipo wapi Tanzania hii?
Kuna hujui neno Pentecost hutanielewa
 
Yesu aliwapiga wafanyabishara waliokua wanauza bidhaa mbele ya nyumba ya Bwana,Yesu huyo huyo ndiyo aliekua akikemea mapepo yanamtii,Yesu huyo huyo ndiyo aliefanya miujiza mingi unasema Yesu hakupiga kelele wakati alikuja kuleta ukombozi
 
Sio Yesu tu hata mimi huwa sipigi kelele. Huwa nafundisha na kuhubiri kwa utulivu ili wasikiao waelewe.

My declaration: Nimeokoka hivyo
Roho wa Mungu ndio chuo changu. Kazi ya Mungu inahitaji kuongozwa na Mungu mwenyewe na si vinginevyo!
we bure kabisa. ushajiuliza kwnini Mungu alimchagua msomi Paulo kupeleka injili kwa mataifa akawaacha Petro ndani au kwanini Paulo alikuwa anasisitiza kwa akina Timotheo kuwa wawafundishe wengine. hata hiyo theolojia umejuaje kuwa hao walioanzisha hawakuongozwa na Roho Mtakatifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…