Wapendekeza umri urais uongezwe badala ya kupunguzwa - Maoni Katiba Mpya

siungi mkono hoja ya umri kwani wengi ambao ni wazee busara zao ni za kuhujumu uchumi wetu tu. Nadhani tunahitaji uadilifu zaidi kuliko umri katika uongozi.
 
Ni mapendekezo mazuri sana hasa ukizingatia nafasi yetu tulipo kama taifa yaani kisiasa, kiuchumi na kifikra. Taifa letu hatupaswi kabisa kufanya majaribio. Hekima ya hali ya juu sana inahitajika katika ofisi ya juu kama ikulu. Nikiangalia jinsi taifa la China lilivyo imara na serious katika masuala yote nyeti, jibu ni kwa sababu wameiheshimu sana ofisi kuu(ikulu) nchini mwao. Rais wa China huanzia umri wa miaka 70 na kuendelea. Kwetu kulingana na umri kushuka na watu kutaka kuwahi kujionyesha hata kabla ya kukomaa kiakili na kifikra napendekeza umri wa mtu atakaeruhusiwa kikatiba kuingia ikulu, angalau uanzie miaka 50 na ukomo wa mtu kuwepo ikulu uwe miaka 85 kwa maana kwamba atakaepata uraisi akiwa na miaka 80 ataongoza awamu moja tu.
.
 
Hata ubunge iwe miaka 30 maana huku mtaani vijana wanapigana vikumbo kutaka kuwa wabunge wanachukulia ubunge kama sehemu ya kutokea kimaisha na si kuwatumikia wananchi wakiingia kule ni vurugu tu wanabishana hadi wanapanda juu ya meza hamna ustaarabu kabis
 
ikulu_300_185.jpg



Mwakilishi wa viti Maalumu CCM Asha Bakari Makame amependekeza kwa kamati ya kuratibu maoni ya katiba kwamba umri wa rais inafaa uongezwe ili kiongozi atumie busara katika kuongoza nchi.

Amesema mgombea urais kuwa chini ya miaka 40 inamaanisha atapatikana rais wa watoto. Aliyasema hayo juzi tume hiyo ilipokutana na Baraza la Wawakilishi.

Yote hayo ZITTO asigombee 2015? haiwezekani kamwe, ZITTO lazima agombee, hizo njama za kupenyeza watu wa kummaliza zitashindwa tu.
 
Ni mapendekezo mazuri sana hasa ukizingatia nafasi yetu tulipo kama taifa yaani kisiasa, kiuchumi na kifikra. Taifa letu hatupaswi kabisa kufanya majaribio. Hekima ya hali ya juu sana inahitajika katika ofisi ya juu kama ikulu. Nikiangalia jinsi taifa la China lilivyo imara na serious katika masuala yote nyeti, jibu ni kwa sababu wameiheshimu sana ofisi kuu(ikulu) nchini mwao. Rais wa China huanzia umri wa miaka 70 na kuendelea. Kwetu kulingana na umri kushuka na watu kutaka kuwahi kujionyesha hata kabla ya kukomaa kiakili na kifikra napendekeza umri wa mtu atakaeruhusiwa kikatiba kuingia ikulu, angalau uanzie miaka 50 na ukomo wa mtu kuwepo ikulu uwe miaka 85 kwa maana kwamba atakaepata uraisi akiwa na miaka 80 ataongoza awamu moja tu.
.

Semeni yote lakini mwisho wa siku ZITTO ndani ya nyumba tena kwa katiba hiyo hiyo mpya.
 
Haya ni mapendekezo ya kumkomoa mtu. Mapendekezo kama haya hayafai kabisa hasa katika suala nyeti kama katiba. Niwaulize swali je umri mkubwa ndio kigezo cha mtu kuwa na busara na uwezo wa kuongoza?
Hatuandiki katika mpya kumfurahisha mtu mwenye tamaa zake, bali tunaandika katiba mpya kwa ajili ya miaka 50 ijayo, labda ungeuliza wakati Marekani inaweka kikomo cha Urais kuwa miaka 8 walikuwa wanamkomoa nani?

Hakuna Muislamu yeyote mwenye akili zake timamu asiye juwa kwamba sifa kuu ya kwanza ya Next President ni lazima uwe Mkristo, hili wala halina mjadala na haijarishi atokane na chama gani. kama mnadanganya Zitto endeleeni kudanganyana. Time will tell hata Ubunge hawezi kupata.
 
Hili ni pendekezo zuri kwa kila kipimo. Lakini binafsi naamini ingeongezwa kwenye nafasi zote; udiwani na Ubunge isiwe chini ya miaka 30; Urais isiwe chini ya miaka 45 na nafasi zote ukomo uwe miaka 70! Na mtu akigombea akiwa na miaka sabini basi anaruhusiwa kipindi kimoja tu katika nafasi zote.

Mkuu unamtaka ugomvi Zitto, mwenzio hiyo 40 tuu anaiona mingi na ipunguzwe
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom