Wapenda ugali mpo?

Wapenda ugali mpo?

Dhaa!! Pilau na ugali +
Wali maharagwe kama nmelogwa na vyo yan
 
napenda sana ugali..naweza kuula hata bila mboga..naula mtupu hivihivi na maji na naenjoy..i dont know why!
sasa ikitokea kuna mboga nnayoipenda sana kama vile samaki waloungwa kwa nazi au mlenda na dagaa mchele walokaangwa...aisee hilo pande la ugali ntalobeba wananishangaa

but dona siliwezi kabisaa nkila nawashwa kwenye koo panapopita chakula.
 
Waache viepe, thubutu… watakuja wachache kukuunga mkono
 
Ugali ndicho chakula nikipendacho...Nakutana na Changamoto nikimwambia wife apike hata usiku Mara nyingine hulazimika kunipikia Mimi huku wao wakila kingine wakipendacho. Wali kwangu nikila mfululizo unanikifu mnoo.

Nipate Ugali Na Mboga Kavuu, pembeni Kachumbari then liwepo Tembele, utalika ugali mkubwa sana.
 
Habari za J3 wapendwa

Mimi ninapenda sana kula ugali, ninaweza kula chakula hiki siku saba za juma mradi tu nibadilishe kitoweo. Kuna wanaume nikiwaeleza mapenzi yangu kwa ugali wananiona mlugaluga.

Imebidi nipunguze ulaji wa ugali kutokana na issue za uzito wa mwili. Siku hizi ninakula ugali Jumamosi tu. Kuna wanawake wanaopenda kula ugali kama mimi?

Wanaume pia mnakaribishwa
Wife material
 
Mi ugali hata niende sehemu za kula nakanyaga ugali mbuzi,kitimoto,kuku,kachumbari ,majani,pilipili,mtindi basis raha tu..naupenda ugali
 
Napenda sana wali na ndizi..... Ugali mmm naweza maliza mwezi sijautia mdomoniii.....
.na hata Nikola uwe dona siyo sembe
 
Back
Top Bottom