Wapenda ugali mpo?

Wapenda ugali mpo?

Ugali niliokulaga enzi hizo boarding kwa miaka minne na maharaghe yenye wadudu umetosha kabisa. Yani sina hamu ya ugali kabisa.
Bora umesema kwel,,maana hakuna jins ya kukataa kule,utakula kwa lazima,sasa hvi oiga wali tu tena kwa nazi
 
Habari za J3 wapendwa

Mimi ninapenda sana kula ugali, ninaweza kula chakula hiki siku saba za juma mradi tu nibadilishe kitoweo. Kuna wanaume nikiwaeleza mapenzi yangu kwa ugali wananiona mlugaluga.

Imebidi nipunguze ulaji wa ugali kutokana na issue za uzito wa mwili. Siku hizi ninakula ugali Jumamosi tu. Kuna wanawake wanaopenda kula ugali kama mimi?

Wanaume pia mnakaribishwa
Ugali m'baya bhana,kitu wali bhana!!!
 
Ugali na maharage pembeni nguru/papa ya kuchoma na nyanya chungu za kuoka
 
mie na ugali hapana!..ila nkienda kwa mtu nkakuta ugali ntakula.

Napenda viazi vitamu kwa karanga za kukaanga ama maziwa mgando.

hata mwaka mzima ntakula hivyo ila UGALI...hapana aseee
 
mie na ugali hapana!..ila nkienda kwa mtu nkakuta ugali ntakula.

Napenda viazi vitamu kwa karanga za kukaanga ama maziwa mgando.

hata mwaka mzima ntakula hivyo ila UGALI...hapana aseee
Wewe utakuw Msukuma
 
Wenzio wanatukimbia tukiwalisha ugali mfululizo eti tunawakomaza!
 
Habari za J3 wapendwa

Mimi ninapenda sana kula ugali, ninaweza kula chakula hiki siku saba za juma mradi tu nibadilishe kitoweo. Kuna wanaume nikiwaeleza mapenzi yangu kwa ugali wananiona mlugaluga.

Imebidi nipunguze ulaji wa ugali kutokana na issue za uzito wa mwili. Siku hizi ninakula ugali Jumamosi tu. Kuna wanawake wanaopenda kula ugali kama mimi?

Wanaume pia mnakaribishwa

Mie sio mwanamke, lakini nikuulize, unapenda ugali kweli au ugali mwingine? Maana bado kichwa kinanizunguka kwamba pamoja na mambo mengi na changamoto zinazoikabili nchi yetu leo wanawake waanze kuchangia kupenda au kutopenda kula ugali.

Then hii topic itawapeleka wapi wanawake, kuzalisha mahindi zaidi?
 
tupo wengi kumbe, mi ninakula ugali siku 7 za juma na huula mchana tu.usiku ni mbogamboga au mtori.asubuhi ni matunda kwenda mbele
 
Dawa ni kufanya mazoezi mkuu. Ugali una carbohydrates kubwa na hii isipotumika mwilini inabadilishwa kuwa mafuta ambayo yanahifadhiwa kwenye ini kwa matumizi yabaadae kama vile inacyoweka nafaka ghalani. Ukizidi kuyaongeza yanahifadhiwa katika sehemu nyingine za mwili kama tumboni ndiyo yanasababisha kitambi. Yakizidi sana yanashindana nafumo wa mwili wa kurekebisha kiwango cha sukari.
Asante kwa ufafanuzi mkuu
 
Ukipata Ugali, Dagaa nazi imekoleaaa ila lisiwe supu, Matembele kandimu kasisahaulike na Roast la bamia na nyanyachungu

Unashushia na maji ya bariiidiii au mtindi doh
 
Back
Top Bottom