Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

duuh yaani nina hizi sifa zote, mimi wangenichukua na mbegu za uzazi kabisa
Hakuna ukweli wowote ni uzushi tu,pia ikazushwa eti kuna wachuna ngozi!

Ikaja ukiwa na kipara unakatwa kichwa! Mara ukiwa na mwanya unakatwa kichwa!

Ikaja ukiwa na alama ya M kiganjani unakatwa mkono!

Hizi ni hadithi za kufikirika tu za utotoni.
 
Hakuna ukweli wowote ni uzushi tu,pia ikazushwa eti kuna wachuna ngozi!

Ikaja ukiwa na kipara unakatwa kichwa! Mara ukiwa na mwanya unakatwa kichwa!

Ikaja ukiwa na alama ya M kiganjani unakatwa mkono!

Hizi ni hadithi za kufikirika tu za utotoni.
Wachuna ngozi usilete ubishi kama hukuwahi kuishi mbeya. Mbozi 2003 - kurudi nyuma
 
Ni kweli kulikuwa na wanyonya damu. Kubali kataa. Walipewa nafunzo na vibali, vyombo vya kuhifadhia damu na mihuri. Ni kama walikuwa wanalipia ukiwa kule. Walitumia njia za kunyonya na kuua kwa kuwa ilikuwa ni kwa nguvu. Baadaye wakaona haikuwa effective way hivyo wakaanza kampeni za kuhamasisha watu kujitolea pia issue ya HIV ikawa ni tatizo pia. Hivyo ndiyo maana leo kampeni za kuchangia damu zipo. Watu wale walipewa pia Makoti Meusi marefu. Kwetu walikuwepo na marehemu kaka yangu alinusurika mara mbili na watu tofauti Mmoja akiwa ndugu upande wa mama na mwingine jirani wa mbali kiasi. Marehemu mama alikwenda kuwauliza live na kuchimba mkwala kuwa atawatangaza kijijini. Walituogopa kinamna. Yule Mzee alichukiwa na alikufa kifo cha mateso na Watoto wake hovyo kabisa.
 
Hii ni kwelI kuna jamaa alikuwa anaitwa sekeni kwa wenyej wa iringa maeneo ya ndiwil ,kilolo,igula,nyabula alitikisa sana na ni kweli alikkuwa ananyonya damu ilaa naskia hawa watu walikuwa na kibal maalumu cha serikal na ndo walikuwa matajir na wana vigari fulan kama vikobe vyenye msalaba
 
Hayo mambo dhaifu ya wagogo wenzangu. Baada ya kulewa mizoga ndio wanaleta hizo hadithi za kufikirika. Kimeta kikitokea Dodoma half the population will go
 
Damu hutumika kama sadaka kwa watu wenye imani zao... Hii nadharia ya kunyonya dmu either walikuwa wanachangisha damu ili kutibu wagonjwa based on msalaba mwekundu au kutoa sadaka... But hata leo hii still kuna wanyonya damu (hahahaha!) Kutoka hospitalini wanazungukua au kuweka kituo cha kuchangia damu salama.. Ingawa tunaon wameva uniforms but still hatujui damu hupelekwa kwenye lengo husika..
 
Hizo zilikuwa mbinu za CCM kutengeneza taifa la wajinga
 
Ni kweli kulikuwa na wanyonya damu. Kubali kataa. Walipewa nafunzo na vibali, vyombo vya kuhifadhia damu na mihuri. Ni kama walikuwa wanalipia ukiwa kule. Walitumia njia za kunyonya na kuua kwa kuwa ilikuwa ni kwa nguvu. Baadaye wakaona haikuwa effective way hivyo wakaanza kampeni za kuhamasisha watu kujitolea pia issue ya HIV ikawa ni tatizo pia. Hivyo ndiyo maana leo kampeni za kuchangia damu zipo. Watu wale walipewa pia Makoti Meusi marefu. Kwetu walikuwepo na marehemu kaka yangu alinusurika mara mbili na watu tofauti Mmoja akiwa ndugu upande wa mama na mwingine jirani wa mbali kiasi. Marehemu mama alikwenda kuwauliza live na kuchimba mkwala kuwa atawatangaza kijijini. Walituogopa kinamna. Yule Mzee alichukiwa na alikufa kifo cha mateso na Watoto wake hovyo kabisa.
Upo sahihi Kuna mzee amethibitisha yeye ni miongoni mwa waliokuwa wakifanya kazi hiyo anasema walikuwa mawakala wa kukusanya damu na waliweza kukopeshwa fedha za kuwa na miradi kama usafirishaji ama maduka na mashamba makubwa ambayo yalitumika kukusanya watu kutoka maeneo ya mbali (vibarua) ambao hao katika kuwaua hawakushtukiwa kwa haraka kwani ilikuwa vigumu kupata profile zao kutoka kwenye jamii, lakini mchezo huo ulikuwa mkubwa nchi nzima Iringa kuna mtu alikuwa maarufu Chalamila kuelekea Sadani alikuwa anafanza hayo,Mbozi kuna akina Bantu orodha ndefu tu walifanya kazi hiyo. Walipewa vifaa vya kuhifadhia damu na mahala pa kukabidhi walipewa, pia damu nyingi ilivuka mipaka kwenda nje, kwa mujibu wa mzee huyo, anasema kulikuwa na mzungu waliyekuwa wakiwasiliana naye kwa utaratibu wa chain kama wanavyofanya watoa taarifa ambapo watu say wapo 05 lakini A hamfahamu C, ingawa A anampa B na B anakabidhi kwa C hadi E kwa utaratibu huo.
 
Back
Top Bottom