Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Ni kweli walikuwepo, kuna ugonjwa unaitwa filariasis vidudu vyake mchana hupotea kwenye damu alafu usiku vina rudi, husababisha matende. Sasa wakati huo kulikua na kama mlipuko kwahiyo walibidi wachukue sample usiku kupeleka maabara. Ilo jina ndo likaanzia hapo
 
Maeneo ninakotoka ilishika kasi kuanzia Oparesheni Vijiji Mwaka 1972 ili kuwafanya waliokuwa wabishi kuondoka mashambani ili wakajiunge na wenzao kuanzisha vijiji vya ujamaa. Miaka ilivyoenda ikawa ni tatizo lililoisumbua sana serekali hasa maeneo ya vijijini. Ilifikia hatua hata watumishi wa serikali walikosa ushirikiano hata kwenye masuala mbalimbali kama vile kampeni za chanjo, elimu, kilimo nk.
Ukosefu wa ubunifu na utashi miongoni mwa viongozi wengi wa wakati huo (na hata sasa) imegharimu nchi hii pakubwa.
Na Bado!
 
Naamini kulikuwa na ukweli fulani, kwa kuzingatia mahitaji ya damu na ugumu wa kuipata kwa hiari.
Ila kuna 'exaggeration' ya taarifa kutokana na ukosefu wa elimu miaka hiyo.
 
Nakumbka enzi hizo niko darasa la kwanza,tulitimua mbio shule nzima baada ya kuona gar likidaiwa la wanyonya damu kitambo sana sijui kama ilikua ukwel.
Haha zamani raha sana
 
Vp mkuu hii issue ilikuwa ni kweli?
Hakuna kitu kama ''chinja chinja'' au wanyonya damu. Huo ni uvumi wala hauna maana yoyote. Ila zamani watu wengi waliamini na wazazi walikuwa wanatumia hii njia kutishia watoto wasitembee usiku hasa wakiogopa watu wabaya watawabaka.
 
Hakuna ukweli wowote ni uzushi tu,pia ikazushwa eti kuna wachuna ngozi!

Ikaja ukiwa na kipara unakatwa kichwa! Mara ukiwa na mwanya unakatwa kichwa!

Ikaja ukiwa na alama ya M kiganjani unakatwa mkono!

Hizi ni hadithi za kufikirika tu za utotoni.


WACHUNA NGOZI WALIKUWEPO, SIO UZUSHI KWANI KUNA MIILI ILIOKOTWA IKIWA IMECHUNWA NGOZI NA NINA KUMBUKA WATUHUMIWA WALIKAMATWA ISIPOKUWA SINA KUMBUKUMBU YA KESI ZAO ZILIISHAJE
 
Ilikua Kweli serekali ilitumia mbinu hiyo kupata Damu kwaajili ya hospital
Leo hii watu wanajitolea Ndio maana Huwezi ona Yale matukio
Hospital wana nunua Dam Lita moja elfu hamsini 50000

Sasa hawawezi kukabana na mtu polini tena
 
Bwana @uhurukenyata kwa maelezo yako ni kwamba haya matukio yalikuwa ni kweli. Hawa jamaa hiyo damu walikuwa wanaifadhi wapi? Je walikuwa wakinyonya wanaimaliza kwenye mwili wa mnyonywaji maana kama nilivyosema hapo kwenye post yangu #1 unatoaje uhai wa mtu ili kuokoa uhai wa mtu?
 
Bank ya Damu, zamani watu walikua ni wagumu sana ukimwambia swala la kutoa Damu! Ana husisha na mambo ya kishilikina hii ni kwa sababu ya ukosefu wa Elimu
 
WACHUNA NGOZI WALIKUWEPO, SIO UZUSHI KWANI KUNA MIILI ILIOKOTWA IKIWA IMECHUNWA NGOZI NA NINA KUMBUKA WATUHUMIWA WALIKAMATWA ISIPOKUWA SINA KUMBUKUMBU YA KESI ZAO ZILIISHAJE
Nakumbuka wachuna ngozi wawili walikamatwa mbozi mbeya wakiwa na ngozi waliyoichuna,yaani yule binadamu aliyechunwa huwezi kukuangalia mara mbili,
Kuna watu wakatili sana kwenye dunia hii
 
Bwana @uhurukenyata kwa maelezo yako ni kwamba haya matukio yalikuwa ni kweli. Hawa jamaa hiyo damu walikuwa wanaifadhi wapi? Je walikuwa wakinyonya wanaimaliza kwenye mwili wa mnyonywaji maana kama nilivyosema hapo kwenye post yangu #1 unatoaje uhai wa mtu ili kuokoa uhai wa mtu?
Tena mtu anayekwenda kuokolewa ni yu mgonjwa hoi na huyo anayenyang'anywa uhai ni mzima kabisa! Vitu vingine wala huhitaji shule kujua huu ulikuwa ni uongo. Biashara ya viungo vya binadamu iliyopo ni hii ya vitu kama figo. Japokuwa hapa Bongo haipo lkn sehemu kama India mtu akikaa vibaya anatolewa figi zinakwenda kuuzwa kwa tajiri mwenye fedha anayehitaji. Kuna kisa niliambiwa cha jamaa ''aliibiwa' figo moja hospitalini wakati wa operation!
 
Back
Top Bottom