Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Wanyonya damu walikuwa wanaipeleka wapi damu?

Nakumbuka Arusha ile njia ya kwenda Kisongo kule mikahawanii. Duuh Yaani palivuma sana kuwa kuna wanyonya damu.

Ila siamini kama ilikuwa kweli.
Aahaha pale burka lakin boda boda walikua wanatolewa vichwa pLe
 
Miaka ya 1980 na 1990 kwenda 2000 kulikuwa na watu wanadaiwa kuwa ni wanyonya damu. Magari ya msalaba mwekundu tulikuwa kukikutana nayo lazima tutoke mbio kwa hofu ya kunyonywa damu.

Binafsi mimi kuna watu pale kijijijni kwetu mkoani kilimanjaro walikuwa wakihusishwa na unyonyaji damu. Mmoja nadiriki kumtaja alikuwa akiitwa Michael Ibrahim wa kijiji cha Longuo. Huyu bwana alikuwa akiogopwa na kila mtu.

Watoto wadogo wakimwona walikuwa lazima wakimbie. Pia baadhi ya wakina mama nao pia walikuwa wakimwogopa. Kuna taarifa za wakati huo kukutwa kwa miili ya watu wakiwa wamekufa na huku miili yao ikiwa imegongwa mihuri kuonyesha kuwa yule marehemu kanyonywa damu. Na wengi wa watu ambao walikuwa akisemwa kuwa ni wanyonya damu walikuwa ni watu wenye kipato. Hivyo kipato chao kuhusishwa na unyonyaji wa damu.

Kilichonifanya nilete huu uzi hapa ni kutaka kujua hii kadhia ni kweli ilikuwepo? Na kama ni kweli hiyo damu walikuwa wanapeleka wapi?

Sababu mimi nachojua ni kwamba damu ni kwa ajili ya tiba yaani kwa ajili ya kumwongezea mtu aliyepungukiwa na damu.

Sasa inakuwaje utoe uhai wa mtu kwa ajili ya kuokoa uhai wa mtu?
Zilikuwa Imani za kijinga Tu sisi Mbeya hapo Uyole kuna Dokta mmoja Mkinga anamiliki Hospitali anaitwa Sijabaje watoto miaka ya tisini walikuwa wakimuona wanatoka nduki eti ananyonya damu ili atengenezee vidonge...... ulikuwa ni ushamba Tu na kukosa elimu,si unajua tatizo letu kubwa ni elimu hata sasa! Mawazo ya wengi wetu yamejaa ushirikina shirikina..... That's why mtu akifanikiwa tunamwita mchawi, mostly hatuamini ktk uwezo na matumizi sahihi ya akili na utashi kuleta mabadiliko
 
Damu ilihitajika kwa wingi kipindi kile na ilikuwa ni Biashara kubwa isiyo rasmi kutokana na vita mbalimbali.
Ilikuwa ni vigumu kushawishi watu kujitolea damu kwa hiyari lakini damu ilihitajika sana.hata ktk vita ya kagera kulikuwa na mahitaji makubwa ya damu ili kuokoa maisha ya askari mbalimbali ambao ni majeruhi.
Wanaosema hayo ni mambo ya kufikirika hawajui wanachosema.
 
Acha kumuita michael ibrahim babu yangu kipenzi myonya damu akili kisoda wewe ulishawahi kushuhudia akinyonya damu jitu zima linashindwa kufikiri mtu anyonye damu aipeleke wap.ninyi si majirani pale mlikua mna wivu tu na maendeleo yake ushirika wa neema nzima yeye ndio alikua mtafutaji kwa bidii ninyi kwenu mlikua mnashinda kwenye baa za mbege badala ya kwenda kulima mashamba ya kosata
Forgive me ndugu yangu. Sijasema alikuwa ananyonya damu but alikuwa akitajwa sana kwenye hayo mambo. Pia nimesema sijawahi kuona ushahidi wa mtu akiyenyonywa damu.
 
Miaka ya 1980 na 1990 kwenda 2000 kulikuwa na watu wanadaiwa kuwa ni wanyonya damu. Magari ya msalaba mwekundu tulikuwa kukikutana nayo lazima tutoke mbio kwa hofu ya kunyonywa damu.

Binafsi mimi kuna watu pale kijijijni kwetu mkoani kilimanjaro walikuwa wakihusishwa na unyonyaji damu. Mmoja nadiriki kumtaja alikuwa akiitwa Michael Ibrahim wa kijiji cha Longuo. Huyu bwana alikuwa akiogopwa na kila mtu.

Watoto wadogo wakimwona walikuwa lazima wakimbie. Pia baadhi ya wakina mama nao pia walikuwa wakimwogopa. Kuna taarifa za wakati huo kukutwa kwa miili ya watu wakiwa wamekufa na huku miili yao ikiwa imegongwa mihuri kuonyesha kuwa yule marehemu kanyonywa damu. Na wengi wa watu ambao walikuwa akisemwa kuwa ni wanyonya damu walikuwa ni watu wenye kipato. Hivyo kipato chao kuhusishwa na unyonyaji wa damu.

Kilichonifanya nilete huu uzi hapa ni kutaka kujua hii kadhia ni kweli ilikuwepo? Na kama ni kweli hiyo damu walikuwa wanapeleka wapi?

Sababu mimi nachojua ni kwamba damu ni kwa ajili ya tiba yaani kwa ajili ya kumwongezea mtu aliyepungukiwa na damu.

Sasa inakuwaje utoe uhai wa mtu kwa ajili ya kuokoa uhai wa mtu?
Ilikuwa Ujinga tu, ni kama sasa hivi Magufuli anavyoogopa mitandao ya kijamii - Whatsapp, Twitter na Instagram; au anavyoogopa kupanda ndege!
 
jamii yetu inaishi kwa uzushi kwa sababu ya ujinga
.babu wa loliondo
. free manson
.pesa za majini
.mvuto wa mapenzi
.biko na tatu mzuka
(collective incimbilization= ujinga wa halaiki)
 
afadhali Chadema haikuwepo miaka hiyo maana tuhuma zingekuwa nyingi sana
 
humu kuna watu wa zamani ila uelewa wao bado una walakini, ila sishangai mtu unakula ugali tangu kuzaliwa hadi kufa. huwez elewa chochote.
 
KUNA DEREVA TAX MMOJA NASIKIA KACHUNWA NGOZI YA USO,MAINI NA MOYO NAVYO NASIKIA VIMEONDOLEWA WIKI ILIYOPITA KWENYE MKOA MMOJA WA KASKAZINI.
 
Nakumbuka Arusha ile njia ya kwenda Kisongo kule mikahawanii. Duuh Yaani palivuma sana kuwa kuna wanyonya damu.

Ila siamini kama ilikuwa kweli.
Hahahaha.....ofcourse,kwetu ni pale majengo ya chini,mikahawani kwa wazungu kule tulkua tunapaogopa had si vizur
 
Back
Top Bottom