Heaven Sent
Platinum Member
- Sep 27, 2013
- 32,719
- 98,386
Kuna hawa wamama wawili walinichekesha hadi basi. Huyo mama A mumewe ni kama kaioa kabisa nyumba ndogo na kahamia huko, hawajafunga ndoa na bi mkubwa. Vitu vingine vinatolewa kwa mkubwa vinapelekwa kwa mdogo, hali ambayo ikawa inamuumiza sana A. Sasa A ana rafiki yake B, huyu B akawa anamsema sana A. Kwa nini unajistress hivyo, hela ya kula hupewi, huna nyumba ya kuishi, sijui watoto hawasomi? EtcSasa fikiria wale wale wanaowasema wenzao nje, kwanza katoka nje na pili anakusema huko nje alikotoka. Usiweuke mchezo? Halafu eti ndo utoke ukampigie simu huyo aliyeambiwa ABC zako. That is dealing with the wrong enemy!
Siku hiyo B akanotice mumewe ana nyumba ndogo, kaiba namba kaipigia. Nyumba ndogo kapokea kwa bashasha na namba ya mama B alishapewa na Mzee. Kapokea eeh mama fulani (B), sijui pole na hongera (alijifungua last born kwa c section), ndo kujitambulisha me ni mke mdogo and najua Mna watoto kadhaa, ila mtoto wa 3 sio mtoto wa mume wetu (B kuna kipindi mume alimtelekezaga, akapata sponsor ndo na baba wa huyo mtoto wa3, ila mume akaja akajirudi wakasameheana). B kukata simu na kilio na presha juu, sio kwa kutolewa hadi siri ya mwanae watatu. Ndo nikakuta A anamcheka sasa "wewe nini kujitia stress, hauli? Huna pa kuishi? Watoto hawasomi? . Huwa naimagine mtu anayesema "mimi as long as mume ananijali na wanangu akichepuka hata sijali", like seriously wewe umefuata kula tu kwa mumeo so roho haiumi? Anyway we differ