Mkuu umeua kabisaaaaa! mtu anapigwa anajiuliza kwa lipi? Alafu kazi ya kumtunza mke ilikua ya mwanaume sasa wasikuhizi wabahiri sjui wabinafsi.Mwanaume usipomuhudumia mkeo usitarajie utii.Mungu aliwapa uongozi sasa nyie mwataka heshima bila majukumu.
Wanaume walikuwa enzi hizo walijua majukumu yao ...decision making..kuwafikisha wake zao
Wanaume wa siku hizi chipsi yai...kulia lia tu hawana hela za kuhonga..
Wanawake zaman unamkuta anamiaka 28 lakin bado bikra anaitunza heshima ya mumewe mtarajiwa lakin sasa hivi unakutana na cave, mwanamke zaman ilikuwa mwiko kujibizana na mume wake mbele ya watoto hata akipigwa akiona watoto wamekuja anajifuta lakn sasa hvi duu!
Wanaume wa zaman halikuwepo suala la kumfumania mkewe alikuwa ni aibu kwa mwanaume ndio maana baba kama anarudi nyumban usk alikuwa anaanzia mbali kuimba ili kama kuna mwiz akimbia
zamani walikuwa na hela za kuhonga?
Sikuwahi kuona babu yangu akiongea jambo la kumkwaza mkewe mbele ya watoto,ila wanaume wa sasa unatoka huko hujali chochote unaanza kuporomosha maneno kwa mkeo,.unafikiri kutakua na ustahamilivu hapo?
wanawake zaman unamtongoza mwez mzima na bado anakuzungusha lakin sasa hvi mnafahamiana hapohapo na anakuvulia nguo hapo hapo tena bila hata ya kutongoza
Mkuu kweli wanawake walikuwa zamani, siku hizi unapata mchumba siku ya pili tu anaanza mizinga ya ajabu ajabu mara vocha, hela ya saloon, sijui mchango wa birthday bila kuregard mtu una uwezo gani kiuchumi.. Yani wanaboa sana.
utandawazi ndo chanzo cha mabadiliko kwa wanawake wa leo.
Enzi zile mwanamke amepigwa na mumewe analia, akisikia tu hodii hodiii haraka sana anajifuta machozi na kuanza kucheka, wa siku hizi mbona ataenda kulilia kwa jirani ili dunia nzima ijue kapigwa au huyooo mahakamani. Hebu sasa tutumie uzi huu kutaja matendo ya wamama wa zamani ya kishujaa kama hili nililolitaja ili hawa watoto wa siku hizi kina miss neddy, DEMBA, mama la mama, miss chagga na wengine wajifunze.
Unampiga mkeo halafu unajiita mwanaume?????
Kama una nguvu sana si ukapigane na wanaume wenzio? Au kachukue jembe ukalime?