Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 9,283
- 19,922
Labda sababu wanaweza kuongea kilughaMimi nimefika huko sio Mwanza tu, hadi Simiyu vijijini Wigelekelo hadi Bushashi ukoo! And believe me wasukuma ni kati ya watu ninaowakubali kwa sababu nimeishi nao sana. Nimewasikiliza sana kina Bhudagala Mwanamalonja, Bhulemela Thomas, Juma Kairo, Kado Chiza, Nyakabaya, Nyanda Lunduma, n.k kwaio ni watu ambao ninawaheshimu siwaoni kama washamba au inferior!
Lakini lazima nikiri kwamba linapokuja suala la utafutaji wageni tuna struggle sana kuaminiwa na wenyeji yaani wasukuma. Wasukuma ni ngumu sana kumuamini mgeni na kumpa kazi (tender), hivyo hivyo kwenye biashara sijui wanaona kama unataka uwaibie hivi sijawai kuwaelewa hapo.
Makazini nako hivo hivo mfano hospitali unakuta nurse ambae ni msukuma anaaminika zaidi kwenye issue za magonjwa na matibabu kuliko daktari ambae si msukuma. Au unakuta tabibu ngazi ya chini mfano CA, C O au AMO ambae ni msukuma anaaminika kuliko superiors wake kama MD, Specialist, na Super specialist.
Huko Usukumani ukiongea Kiswahili ni kama mtu aongee Kiingereza miji mingine