Wanawake stress nyingine tunazitafuta

Wanawake stress nyingine tunazitafuta

mac
Kucheat ni bahati mbaya? Kuchat na wanawake tofauti na mkeo kimahaba ni bahati mbaya? Hivi vitu vina process ndo maana tunawashangaa mnavyosemaga ni bahati mbaya

Bahati mbaya maana yake kitu kimetokea ghafla bin vuu siyo utongoze wanawake huko uhonge hadi ukubaliwe mkubaliane kukutana sehemu mfanye yenu halafu useme ni bahati mbaya? Jamani Mungu anawaona mjue
macho hayana pazia
 
Unaongea kama kuna aliyekupigia simu na kutukana au amekukosea heshima lakini kuchunguza simu hakusaidii, mwenye tabia yake anayo tu.
Dada kuna michepuko haina adabu inatafuta hadi namba za mke na kumletea ubabe kuna mfano mmoja niliambiwa siku hiyo mke wa mtu amekaa ametulia zake ghafla namba ngeni inapiga kupokea kidada kinajitambulisha kama mchepuko wa mume wake halafu kwa kejeli kinasema eti "nina mimba ya mume wako" yule mke alitumia busara sana kumjibu akamuuliza kwa upole tu "kwani yeye mwenyewe umeshamwambia?" eti kakajibu "ndiyo anajua" mke akamwambia "sasa kama yeye tayari umeshamwambia anajua mimi unaniambia ili nifanyeje?" kenyewe kakaona aibu kakakata simu hii michepuko saa nyingine ndo ina kiherehere cha kutafuta namba za wake haya unakuta mume alikuwa anaficha ila mchepuko ukafichua hapo mke afanyeje jamani?
 
Back
Top Bottom