Wanawake na magari

Umenikumbusha sister angu mmoja alisha wahi kunokisha engine ya gari hata haina week... kisa kajifanya siku hiyo kufungua boneti kaweka maji kasahau kufungu mfuniko... kakanyaga mafuta na safar zake mpaka gari likazimika

Eeeeehhh huyo alitoa mpyaaa, tena umenikumbusha wengine wanaendesha gari kila siku ila ikija kulifanyia service anataka mwanaume ndo alipeleke gereji, au mwengine maji yameisha kwenye rejeta wala hashituki, mshale wa kuonyesha engine inapata moto uko juu kwenye red yeye wala hashituki anakanyaga mafuta tuu matokeo yake engine inachemsha yaani.
 
wengi wanajua kudrive tu tena hizo zenye automatic gear system akikanyaga mafuta hadi anafika. Hawana ujanja ikizngua wanajua wanaume watahusika hapo


ni kweli kabisa, ila niseme ukweli hata manua mie mwenyewe kuiendesha ilikuwa wakati wa driving school na pale unajua mwalimu anaibia kukusaidia kukanyaga clutch na break hivo leo ukinipa gari ya manual looh nahisi ntaiendesha kwa notsi za kwenye kidiary changu ambapo ni kwamba tuu siwezi iendesha looh.
 
ukisema hivo huwa nawaza, ikitokea mdada yuko mwenyewe kwenye gari anaenda mahali in between safari anapata break down na anakuwa kwenye mazingira ambayo hamna watu au ni nia ambayo haipiti watu na labda ni kapori ambapo inasadikika kuna nyoka au hata fisi ambao unajua wanadhuru na jua linazama akipiga simu fundi aje atengeneze ni siku ingine. Hapo ndo huwa nawaza bora mdada anayeendesha gari walau ajue kubadili tyre ili aweze kuendelea na safari au hata ajue kucheki kama maji kwenye rejeta yapo, maji ya wiper, ajue kucheki oil, awe anacheki maji kwenye betri kama ni betri ya maji au kuiangalia kama betri terminals zimekaza au ziko loose walau ile first aid ya gari ili zaidi ya hapo sasa ndo una rely kwa fundi.

 
Hahahahahahaa nimejikuta nacheka tuu looh,
Natamani itokee siku moja nikutane na mkaka awe mwenyewe kwenye gari halafu awe hawezi kubadili tairi halafu mie nimpe hiyo service ya kubadili tyre, natamani hiyo hali initokee


 
vpi umerudi lini kutoka kwa Obama au unaongele ukiwa uko
 

Hahah mi nimekupa pongezi tu bana ila nilijua hili ni gari la pili umenunua si lile la makrashi...

okeee ila wanatakiwa wajifunze walau kubadiri tairi au hata kuchokonoa betri ikiwa iko loose sio gari inazima unapigia fundi anakuja kusogeza betri tuu gari inawaka .....................

Mkifanya nyie kila kitu mafundi watakula wapi?


We mara kibao nimekwambia twende wote jogging lakini wanikimbia...

If u serious utanitafuta mwenyewe...
 
Nitapata wapi mie hela yakukodisha gari?Labda kama unipe lote lote......lol

bure inaua dada bora ubaki bila kuwa nalo, maana akikupa bure tuu ujue utarudi kwake kutaka hela ya mafuta, service, tairi zimekuwa kipara bora usilitamani la uligharamikie kwa heloa zako
 
Habari zenu wapendwa.
Issue inakuja gari ikiharibika inakabidhiwa mwanaume. Ni kudeka au ndo kawaida maana mie gari pancha nabadili mwenyewe, na vitu vidogovidogo.

Au kwakuwa mie sina husband nimejiseti tatizo likitokea ni langu.
 
 
Habari zenu wapendwa.
Nikiwa njiani leo kuelekea kazini kuna mama mmoja tyroad hand ikaachia tairi ya mbele kulia ikakaa migulu baja.Nikiwa kwenye foleni mama akawasha hazard na kuchukua kilongalonga probably alikuwa anampigia husband au fundi.
 
mie nimeshauzoea usafirngu niliopewa na Mungu hapa napita njia tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…