Wanawake: Mazungumzo haya yanatukera wanaume

Wanawake: Mazungumzo haya yanatukera wanaume

tajirijasiri

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
2,863
Reaction score
3,854
Utakuta kila kwenye mazungumzo ya simu na mpenzi wako anakuuliza maswali yale yale mazungumzo yale yale mpangilio ule ule mpaka unakereka na kupata ukurivu na uchoshi (boredom and tiresome) maneno na maswali yenyewe ni haya:-

1. Baby uko wapi? Ili hali anajua muda huo uko job.
2. Baby Umekula? Ili hali anajua kila siku lazima ule?
3. Baby umevaa nini? Ili hali anajua lazima uvae nguo.
4. Baby Umeoga? Ili hali anajua lazima uoge.
5. Baby unafanya nini? kana kwamba yeye ni mlinzi wako.

Najua mnakuwa na lengo la kuonesha mnajali, but mkiwa mnayauliza kila mara, kila siku, kila mazungumzo ya simu, kila wakati, kwa namna ile ile, mpangilio ule ule, yanaboa na kuonesha hamna uwezo wa kuwaza zaidi. Sijui mnanielewa vile!

Ladies; Badilisheni badirisheni mpangilio wa phone conversation ili mlete mvuto na hamu ya kuzungumza!

Unaweza ukayauliza hayo kitofauti tofauti sio kwa mpangilio ule ule kwa kila mazungumzo mpaka inakosa mvuto.

Wakati mwingine kwenye mazungumzo ya simu, mwambie mwanaume wako about wazo la biashara, kiwanja kizuri, n.k. atakuona unafaa kuwa good partner!

Maoni yangu lakini, ladies msinichukie.

Haya nikosoeni
 
Mmh jamani tukicare ooh tumezidisha. Tusipocare ooh hatuwajali. It's true mnahitaji wanawake wa kuwapa mawazo chanya kuhusu maisha. But Usisahau pia kwenye mapenzi " some lil things matter most". And sometimes, those little things can occupy the biggest part of your spouse's heart.

Labda cha muhimu ni kukumbushana tu when to do those little things ili visije vikainterrupt na mambo mengine muhimu zaidi.. Sio muda wote tutahitaji kuongelea biashara na kazi. Muda mwingine tuenjoy tu uwepo wa kila mmoja wetu as a couple. "Sometimes happiness can be hiding where u least expect it"
 
Mpenzi hayana formula..cha msingi ni kujua mwenza wako anapenda nn..utaweza ukawa unapetipeti sana kumbe mwingine anaziona hizo ni kero...nadhani we ni miongoni mwa watu wasiopenda kupetiwapetiwa
 
Umesema kitu hapo... Wapo baadhi sio wabunifu hata ukichati nae.. Utakuwa short answers like "k" "sawa" " ndio.. Binafsi I get bored. Basi ukiacha room aendeleze conversation, anadakia " niambie".. Jirekebisheni kwakweli, at the same time unakutana na mwingine very interesting to chat with., then you automatically shift interests zako
 
Unaitwa 'baby' kwani wewe unavaa diaper?

Aaaaaahhhaaaaaaaa aisee mbavu zangu haaaahhhaaaa... Jamani acheni tujidae kwa babe zetu....aaahhhhaaaaa.. Mko tofauti bwana mbona wengine wanapenda kuulizwa hivyo to show care.... Asante kwa kunichekesha dear.... aaaaahhhhhaaa.. Thanks..
 
Namba 1 ndio zangu izo 🙈🙈🙈🙈
 
Back
Top Bottom