Kutinginya86
Member
- Nov 7, 2014
- 85
- 52
Nilikuwa nazungumza na rafiki yangu mmoja ni mkristo wa Roman akaniambia kuwa.....[emoji116] [emoji116]Mimi ni muumini wa Kanisa la Roman Catholic.
Utaratibu wa Kanisa umetenga upande wa wanaume na upande wa wanawake.Kinachonikera ni pale unakuta wanawake wanaingia kanisani na wanakuta upande wa akina mama nafasi zipo lakini baadhi yao hawapendi kukaa upande waliopangiwa wanaamua kujichomeka kati kati ya wanaume kitu ambacho mwanaume huwezi kwenda kukaa upande wao.
Najiuliza hivi huu ujasiri wanautoa wapi?Tena si wamama watu wazima ila ni mabinti.Huku si kuharibiana usikivu wa ibada?
Unaanza kuwaza mengine wakati uko kwenye ibada!Au hua mnatumwa na shetani?
Kama viongozi wa Kanisa mpo hebu jaribuni kulikemea hili,hasa Kanisa kuu Kigoma mabinti wanapenda sana kujipachika kati kati ya wanaume hata kama upande wao kuna nafasi.
......baada ya YESU kufa msalabani aliondoka na tamaa zote na kwamba shetani hana nafasi tena kwenye mioyoni ya wanao mwamini YESU....sasa malalamiko haya yanaashiria nn
In short hayo ndiyo madhara ya kushindana na ukweli wa maumbile....
Biblia ilikataza wake kwa waume wasiotokana na familia moja kuchanganyika wakati wa ibada (zakaria 12:12-14)
Tena ikaagiza wanawake wajipambe kwa kujisitiri na wasioneshe mapambo yao kwa watu ambao sio ndugu zao(kama kaka, baba, mjomba n.k) kasome (1Timotheo 2:9-12)
Tena inasema wanawake wafunike vichwa vyao wawapo katika Ibada (1 wakorinto 11:5)
[emoji115] [emoji115] [emoji115] [emoji115]
Lakini leo hii hayo hakuna linalofanyika.
....wanawake wanavaa mavazi ambayo sio ya kujisitiri kabisa........na ninyi wenyewe ni mashahidi mana lait yangekuwa ya kujisitiri huyu ndugu yetu hapa tusingemsikia analalamika...........
.....kuchanganyika ndio kama hivyo......
......vichwa wazi ibadani, tena asiyena nywele ndefu anaenda kutafuta wigi maalum la kuvalia kanisani.....
[emoji116] [emoji116]
Sasa hapo utulivu kwenye ibada utatoka wapi!?????[emoji15] [emoji15] [emoji15]