Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa? Tunaomba ushauri wako

Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa? Tunaomba ushauri wako

youngkato

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
3,638
Reaction score
3,641
Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa?

Tunaombaushauri wako utatusaidia na sisi tunaojitafuta.

Najitajidi kufata kanuni zote za biashara na kanuni za biashara lakini hakuna hatua.

Kitu gani kinatufanya tusifanikiwe?
 
Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa?

Tunaombaushauri wako utatusaidia na sisi tunaojitafuta.

Najitajidi kufata kanuni zote za biashara na kanuni za biashara lakini hakuna hatua.

Kitu gani kinatufanya tusifanikiwe?
Wanasemaga wenyewe code ya mafanikio huwa haitolewi eti, kwahiyo we endelea kubonyeza bonyeza tu hadi utaipata right button.

Thecoder tunaomba code
 
Pamoja na kuwa sijajua unayazungumzia mafanikio katika angle ipi lakini maisha ya chini ya jua
ili kubalansi msawazo na mzunguko wa maisha hapa duniani watu wote hatuwezi kuwa sawa.....

Maisha ya duniani ni kama filamu na kila mtu ana character yake!!!

Kuna watu wanalilia kupata fremu kati kati ya Kariakoo...na kuwa watu wanafunga fremu Kariakoo...,..

L I F E
 
Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa?

Tunaombaushauri wako utatusaidia na sisi tunaojitafuta.

Najitajidi kufata kanuni zote za biashara na kanuni za biashara lakini hakuna hatua.

Kitu gani kinatufanya tusifanikiwe?
Mtumainie Bwana wetu Yesu Kwa kila jambo.
 
Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa?

Tunaombaushauri wako utatusaidia na sisi tunaojitafuta.

Najitajidi kufata kanuni zote za biashara na kanuni za biashara lakini hakuna hatua.

Kitu gani kinatufanya tusifanikiwe?
Hakuna njia moja kila aliyefanikiwa basi kafanikiwa kwa namna yake, so huwezi pata jibu la moja kwa moja hapa, kama wakijitokeza kukuambia lakin. Ujue tu kwamba Kuna aliyefanikiwa kwa halali na mengine kwa haramu. Hii inaweza kuwa kwa biashara (mbalimbali) au kwa ajila (pia tofauti tofauti) so hypothetical wakijoteka kukuambia utapagawa bcoz hutojua ufate ipi auache ipi.

Chakukushauri we pambana kama ni mpambanaji na pia endelea kujifuza, nakuweka strategy na mission na pia kua na nidhamu ya njia ambayo utaichagua kufikia hapo unapopataka, haijarishi uchague njia haramu ama halal ili kufikia mafanikio yako but mipango sahihi lazima uwe nayo. Halafu Kisha sasa acha BAHATI ichukue nafasi yake.

Because kufanikiwa pia bahati ina nafasi yake japo sio kubwa au ndogo au ndo guarantee, yani hiyo "bahati pia huja kwa bahati" vilevile 😂 ndo ujue bahati sio poa kuipata na mafanikio sio kwa ajili ya wote.

Yours truly

Adios! ✌🏽 Amigo​
 
Mafanikio ni nini?

Kujipata unapo paongelea ni kipesa au kiafya? Naamini ni kipesa.

Kama ni Kipesa Mkuu ili Uone mafanikio naamini hela unapata ila tu huoni zinakoelekea..

Kama kwenye Biashara

Usianzishe kitu kipya/Biashara Mpya

Biashara unayofanya baki nayo kama zipo mbili chagua 1 inayoingiza zaidi komaa nayo ile ingine FUNGA kama zote zinaingiza vizuri (Stick to Them) ila usiongeze pesa wala biashara nyingine.

Naamini hela unapata ila unazitumia kuongeza biashara ukiamini utatoboa unasahau biashara inachukua Muda kuleta matokeo unakuta umetupia 1m,2m,3m,nk

Mpk uone faida ya ule uwekezaji muda umeenda, lakini mwenzako aliepata 3m yake akaongezea na kamkopo akanunua gari Unamuona Amepiga STEP lakn wewe uko pale pale sababu uli opt kuzalisha zaidi pesa ukiwa na target za mbali ukasahau MUda ndio mtaji ktika biashara.

So FUNGA biashara zote unazoona haziingizi pesa komaa na kitu ki 1 unachoona kinakupa pesa na ukipata HELA usijitoe ufahamu.

Hela yako Fanyia kitu nnje ya biashara, kama ni kiwanja,nyumba,usafiri,nk Nunuaa Usiulize Mtu na wala usifanye lile wazo la kuongeza biashara au kuongeza Bidhaa kwenye duka lako.

Punguza misaada na majukumu

Kama unamajukumu umejipa yapunguze kama unasomesha watoto za watu rudshia wenye watoto wao majukumu yao jitue mizigo ulojitwisha kwa roho yako nzuri baki wewe kama wewe na wanao/mwanao/mke,nk chako.

Kuanzia hapi ukiyatmiza Mwakani muda kama huu utakua na Kitu umefanya ila Achana kabisa na Kutia Pesa katika Biashara zaidi na misaada.

Anza kuzuia pesa zako zifanye MAENDELEO mengine BIASHARA yatosha mkuuu.

Utajiona umejipata muda si mrefu ukiyatimiza haya.
 
Wanaume waliojipata kimaisha. Kitu gani kinafanya sisi wengine tuchelewe kufanikiwa?

Tunaombaushauri wako utatusaidia na sisi tunaojitafuta.

Najitajidi kufata kanuni zote za biashara na kanuni za biashara lakini hakuna hatua.

Kitu gani kinatufanya tusifanikiwe?
Wazazi wapumbavu ni sababu hata ya watoto kukosa ujasiri na motisha
 
Mkuu Umejibu kiufupi Sana
Muulize namba ya kiatu chake alitumia mbinu gani kuijua?

Size ya kiuno chake alitumia njia gani kuijua?

Muulize anaamini kuna baadhi ya nguo akivaa anapendeza ila kuna zingine akivaa hazimkai poa, ni njia gani alitumia kulijua hili?

Majibu yake yote atakayooujibu lazima yataangukia kwenye kujaribu kwanza, kwamba utaenda kwenye duka la viatu utataka kununua kiatu watakuuliza namba yako utasema huna uhakika then wao watatoa viatu kwa size tofauti tofauti kisha watakupa ukaribu hadi utapata namba inayoendana na mguu wako, the same kwenye nguo...

Kwahiyo unaweza usijue size ya kiatu chako ila ukajua aina ya kiatu unachotaka kununua kwasababu unaamini ukivaa aina hiyo ya kiatu utapendeza kulingana na namna ulivyo, na hii ni bila kujali kama umeshawahi kuvaa aina hiyo ya kiatu au hujawahi ila kuna kitu tu kinakuambia hivyo ya kwamba nikivaa aina hii ya kiatu lazima nitapendeza.

So hamishia huo mfano kwenye lile jibu la aendelee kujitafuta atajipata😅😅, aione Evelyn Salt
 
Muulize namba ya kiatu chake alitumia mbinu gani kuijua?

Size ya kiuno chake alitumia njia gani kuijua?

Muulize anaamini kuna baadhi ya nguo akivaa anapendeza ila kuna zingine akivaa hazimkai poa, ni njia gani alitumia kulijua hili?

Majibu yake yote atakayooujibu lazima yataangukia kwenye kujaribu kwanza, kwamba utaenda kwenye duka la viatu utataka kununua kiatu watakuuliza namba yako utasema huna uhakika then wao watatoa viatu kwa size tofauti tofauti kisha watakupa ukaribu hadi utapata namba inayoendana na mguu wako, the same kwenye nguo...

Kwahiyo unaweza usijue size ya kiatu chako ila ukajua aina ya kiatu unachotaka kununua kwasababu unaamini ukivaa aina hiyo ya kiatu utapendeza kulingana na namna ulivyo, na hii ni bila kujali kama umeshawahi kuvaa aina hiyo ya kiatu au hujawahi ila kuna kitu tu kinakuambia hivyo ya kwamba nikivaa aina hii ya kiatu lazima nitapendeza.

So hamishia huo mfano kwenye lile jibu la aendelee kujitafuta atajipata😅😅, aione Evelyn Salt
Saw apo Nimekupata ni Kazi iendelee
 
Back
Top Bottom