Hammaz
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 7,035
- 15,332
Malcom X aliulizwa kuhusu suala la ubaguzi wa rangi unaosababisha kuchukiana(pamoja na kutoleana lugha chafu) na hata kuuana baina ya jamii ya watu weupe na weusi.Kweli jukwaa la intelijensia kwa kiasi kikubwa kuna unafuu. Ila kwani siasa ni lazima matusi? Hatuwezi kufanya siasa safi zisizo na matusi na udhalilishaji wa utu wa watu ambao ni kaka,dada,mama,baba zetu pengine hata babu na bibi zetu?
Alichojibu ni kwamba kwanza jamii inabidi wapatiwe elimu kwani ndiyo msingi wa kila kitu ili watambuane wote ni binadamu na wote wana haki sawa. Kisha itungwe sheria itakayolinda huo undugu.
Kwa swali ulilouliza ninachokiona ni kwamba serikali ililipokea hili suala kwa ghafla pasipo jamii kutanabaishwa siasa itakayokwenda nayo ni siasa ya namna gani.
Kwamba ni siasa ya kukosoana, siasa ya kushindana kwa hoja, ni siasa yenye kukubaliana kwa kukubaliana na ni siasa ya kukubaliana kwa kutokukubaliana ikijumuishwa pamoja na kutokuathiri tamaduni zetu za kuheshimiana. Ambazo hizi tamaduni ndizo zingelikuwa ni kama nguzo ambazo zinalinda utu na heshima ya mtu/watu kwa sababu jamii yetu ndivyo ilivyojengeka.
Kiini cha yote naona elimu! Bado jamii haina elimu ya siasa inayoishi nayo. Licha ya umri wa siasa ya vyama vingi bado ni mdogo (kwa hapa Tz) ila naamini jamii ikijengwa kwa msingi wa elimu(kwa huu muktadha tunaouzungumzia) inakuwa staarabu na shupavu. Na haya yote ya utovu wa nidhamu ya siasa lawama itarudi kwa serikali, kwa sababu serikali ndiyo inayounda jamii iwe ya namna gani.
Ndicho ninachokiona kwa jicho langu.
