Wanaume: Unamuachaje Mzazi Mwenzio?

Wanaume: Unamuachaje Mzazi Mwenzio?

Huwezi amua kuishi maisha ya stress na shida kibao kisa ulihangaika akiwa mjamzito.

Waliotuletea hizi taratibu za kupeana vyeti hawavumilianagi stress hata kidogo huko ndani.
Ndio maana wanatengana hata vikongwe kabisa.
Imagine Putin katalikiana na mkewe miaka michache iliyopita.

Na sisi wafuasi wa asili ya mwafrika tunaongeza mke tu na huyo mwenye matatizo yake tunamuachia nyumba na watoto aendelee kulea.
 
Na huu siyo msimu wa maembe, nimekuta wauza matunda wawili wote wamenipa majibu sawa.

Najiona nikimpelekea juisi ya embe

Kumbe hujamuoa unazalisha nje? Maana angekuwa mkeo usingeona kero.
 
Kumbe hujamuoa unazalisha nje? Maana angekuwa mkeo usingeona kero.
Hapana sijaona kero.

Nimemaanisha ikiwa mtu unavumilia hizi zote za kipindi hichi ni kwa vipi uachane na mzazi mwenzio.
 
Jibu ni moja tu wewe ni ndezi watu wangapi wanawake zao wana mimba na hawafanyiwi undezi huo
 
Sisi wanawake mkituendekeza tukiwa wajawazito basi hakuna rangi hamtaiona. Kuna baadhi ya sababu unaona zina mashiko, zisizona mashiko kuweni na misimamo. Wanawake huwa tunapenda kuwapima wanaume sasa kama mnakubali tu kupelekwa pelekwa kisa ujauzito basi natanguliza pole zangu za dhati kwa baadhi yenu wanaume
Kweli Dada,huwa wakipima akakuta maji ambayo hawez kuyaoga wanakuwa wapole
 
Cha kwanza na kianze.

-Nimeambiwa nikanunue embe usiku huu.

Mama Kijacho tangu iwe confirmed mambo ni moto.

Kwa upande wangu lakini.

-Kuna siku alinipigia simu mchana kua anataka kachori mbili hajisikii kula usiku huo. Mimi ilibidi nishuke vituo viwili kabla ya kituo changu ili nikute meza ya muuza pweza, sijui bei ya kachori kwahiyo nilitoa elfu moja nikataka nigewe zote, nikagewa kumi, namfikishia akakasirika kwanini nimenunua kumi, nina matumizi mabaya ya hela akasusa kula.

-Wiki moja nyuma saa tano usiku nilipigiwa simu kua mama kijacho anaumwa tukafika hospitali baada ya vipimo Dokta akasema binti anadeka hakuna lolote.

-Jana usiku saa sita anasema ana kiu ya maji ya baridi lakini hataki maji yatoke kwenye friji letu, linanuka, akaanza kugonga kwa wapangaji wenzetu Wakamjibu hawana maji akaniambia nitoke nikatafute maji dukani.

-Mtandika kitanda, mfagiaji, mpishi, muandaaji mtoto mkubwa na kumuogesha ni mimi na leo nimeenda kliniki.

-Aliniambia kila siku nirudi na mtindi. Leo nimefika kasema hautaki anataka mkate wa supa loaf, nimeenda kuununua kaonja silesi moja kasema mkate una harufu ya mafuta ya taa kauacha.

-Memori kadi yangu kachukua kurudisha hataki na haifanyii kitu.

-Kwa miezi miwili mfululizo sijapata usingizi wa uhakika.

Nawaza kama kweli anataka embe au anataka nikabwe maana si kwa muda huu.

Hapa ninajiuliza.

Mwanaume unamuachaje mzazi mwenzio? Hizi nenda rudi, fanya acha, simama kaa anazonifanyia ni kama kuna bond inajijenga kati ya mimi na yeye ambayo inanifanya nijiulize...

Mwanaume unamuachaje mzazi mwenzio?
Hamna kitu napenda kama kudekewa na mwanamke (mjamzito zaidi) nnayempenda
 
Jomba mda mwingine kuwa kauzu, Mimi alijaribu mwanzo mwanzo tu mimba iliposhika, Mara ooh kanipikie ugali wakati chakula kingine kipo kakipika mwenyw ila amekikataa, mbona alilala njaa, Mara nibebe mgongoni, Mara mkilala anataka aweke pua kwapani kwangu ukimkataza anaanza kulia.
Aisee alinyooka, sikuwa na mpa ushirikiano kabisa. Nikaongea na mamayake akakubali aende home kwao, nikambembeleza akakubali kusafiri, hadi miezi mitatu baada ya kujifungua ndiyo nilienda kufuata.
Ila nilikuwa namsafiria kila mara, walau kila mwezi naenda.
Namshukuru mamamkwe wangu nimwelewa sana, niliogopa kumpeleka kwa mamangu, wanaweza wakafarakana ikawa shida nyingine.
 
Jomba mda mwingine kuwa kauzu, Mimi alijaribu mwanzo mwanzo tu mimba iliposhika, Mara ooh kanipikie ugali wakati chakula kingine kipo kakipika mwenyw ila amekikataa, mbona alilala njaa, Mara nibebe mgongoni, Mara mkilala anataka aweke pua kwapani kwangu ukimkataza anaanza kulia.
Aisee alinyooka, sikuwa na mpa ushirikiano kabisa. Nikaongea na mamayake akakubali aende home kwao, nikambembeleza akakubali kusafiri, hadi miezi mitatu baada ya kujifungua ndiyo nilienda kufuata.
Ila nilikuwa namsafiria kila mara, walau kila mwezi naenda.
Namshukuru mamamkwe wangu nimwelewa sana, niliogopa kumpeleka kwa mamangu, wanaweza wakafarakana ikawa shida nyingine.
Inafurahisha kusimulia ila kiukweli ni mtihani.

Kuna vijitabia vimezuka na logic yote imewekwa pembeni.
Nachoka sometimes.
 
nilimaliza mitaa nasaka ice cream ya baridi mbaya zaidi wanaume tuna tayari mana ile hali tunaiogopa so whatever anataka lazima ukasake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom