Wanaume tuwe wastaarabu, hebu mcheki huyu

Wanaume tuwe wastaarabu, hebu mcheki huyu

Kiukweli foleni zinachangia hali hii hapa mjini mpaka mtu mzima anafikia kufanya hivyo basi ujue kabanwa kweli...
 
Hujafanya vizuri mkuu.huyo no MTU mzima na ukiona kafanya hivi ujue alibanwa sana
 
Mkuu unaweza kukuta jamaa amebanwa Sana.halafu kumpiga mtu picha unarushia kwenye mtandao dunia nzima imeona si ustaarabu kama ni mimi lazima nikutafute.

Kimekuuma coz ndiyo tabia zako..
 
Yaani ndugu yangu umenipiga picha na kuja kunidhalilisha JF?
 
Nani amekupa mamlaka ya kuiweka picha yangu mbele ya hadhara.....ngoja nikaripoti TCRA....
 
na wale mnaokunywa maji na kutupa chupa hovyo kesho mnasema mitaro imeziba
 
Haijawahi kuwakuta nyie,,, na hizi foleni za kipumbavu za dar!!! Kwa mfano umebanwa pale jangwani na ngoma haitembei utafanyaje?? Au tazara unakuja buguruni na ngoma haitembei...
huu ni unafiki, baadala ya kupiga picha ungeshuka na kumwambia!!!
 
Foleni dar haina makadilio, inawezekana kuvuka hizo taa za tabata ilimchukua zaidi ya saa moja na kutibua timing zake za kwenda kukojoa mwisho wa safari yake!
 
Kwa foleni ya Dar hizo censor zimewekwa na kwenye foleni?
Mkuu, acha bwana.. FYI, kwenda haja ndogo au kubwa ni natural kuanzia utotoni na zipo taratibu kimaadili, huwezi kujikamua hadharani... hiyo fole imeanza juzi na imesababishwa na ujenzi tu!! Mwili wako unakutambulisha kuwa unahaja ya kujisaidia "at least dakka 45 hadi saa moja" !!! Sasa jipange !!
 
Taa zingekua zimeruhusu asingekojoa hapo. Halafu alikotoka huko hakuna sehemu ya kujihifadhi.
 
wanaume wa Dar hao, eti hakuna vyoo vua umma kama zamani
 
Jamaa tuko ya mataa ya tabata mida hii kashuka kwenye Gari yake hiyo karudi nyuma kaanza kukojoa.Dah ustaarabu uko wapi wadau??

1. Foleni ya Dsm unaijua inawezekana mpo masaa 4 hapo, lkn hilo huhakiona!

2. Wapo wanaokojoa kwnye chupa akiwa kwny gari (private) nadhani ulitaka iwe hv, si jema pia!

Isishutu moja kwa moja kuna mazingira ambayo huezi epuka hilo, hujawahi safir na bus mkachimba dawa njiani? Tofauti na hii nn au hiyo lami?
 
Kwa suala la kukojoa ovyo hadharani wanaume tunaongoza kwa uchafuzi wa mazingira.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom