Ndetirima
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 1,008
- 789
Wadau naomba kupata uzoefu kutoka kwa wanaume tuu. Mwenzenu mara nyingi kazi zangu zinanilazimu kusafiri nje ya mkoa wakati mwingine hata miezi mitatu nakuwa mbali na familia yangu, ninaposafiri kikazi nje ya Mkoa ninapata taabu sana kukwepa kutoka nje ya ndoa. Mara nyingi huwa nastahimiri kipindi cha mwezi mmoja mpaka mmoja na nusu, lakini kuanzia hapo hata nitumie mbinu gani nimejikuta nashindwa kabisa uzalendo...... Naombeni kupata uzoefu kwa mdau mwenye nature ya kazi kama yangu anawezaje kushinda hii hali?
Kwa uzowefu wangu wa miaka mingi nimeona ndoa nyingi kwa baba au mama kuwa anasafiri mara kwa mara kikazi na kukaa kwa muda huwa hao wanandoa hawana maisha marefu kama ambao wanakua pamoja kwa 90% ya maisha yao. Safari zinachangia matatizo ya ndoa kwa kiasi kikubwa kama wanandoa hawamjui Mungu. Mimi ninayaona kutokana na kufanya kazi kwenye baadhi ya Hoteli. ILA NACHOKUSHAURI FANYA SANA MAZOEZI BAADA YA KAZI HUTAKUWA NA MATAMANIO KABISA LABDA KAMA UNATABIA ZA KUPENDA KUFANYA UMALAYA.