hivi siku zote hujui kuwa Khantwe ndio mama mwenye nyumba?
Sina muda wa kujibu upuuzi kwa Annonymouse.
Kwann kama Mdada usitumie njia salama za kuzuia mimba ambazo ni natural na hazina side effects?????? Najua mwazijua.
aiseee hongera
Zile zilikuwa hujuma za wazi..
ana nyumba kibao huyo hajulikani mmliki halali
hahahaaa!... Karibu kwenye ulimwengu wa kulala bila.....pi
ana nyumba kibao huyo hajulikani mmliki halali
Wakati mwingine hutokea bahati mbaya, hapo ndio moto unawaka, la muhimu kuwa tayari kwa lolote kila jambo lina faida na madhara.
Sidhani kama kuna watu huwa wanapenda kubeba mimba kabla ya ndoa (siwazungumzii wale wanaohitaji watoto tu ila kuolewa hawataki). Inapokuwa imetokea si vizuri kutwishana mizigo na kusukumiana makosa....wanaume huwa mnakimbilia kusema kwa nini mdada kakubali kubeba mimba,hayuko makini. Well mimi naweza kuwa makini na siku zangu lakini jamani semeni ukweli huwa mnaelewa??? When it comes to sex wanaume ninyi akili huwa zinahama ila akili zikisharudi mnajifanya kuwapondea watoto wa watu.
hahaha ndo mana sikubabaikii kwa sababu najua we ni sharo
Mimi ni kibabu tena kimwaga lol shaulizako wakosa mengi
Kwanini usiende kuchukua changudoa huko ukamaliza genye zako?????
Muwe na huruma aiseeeh
Na mimi baada ya kusoma ngoja nije na wadada.Leo nije kwakina kaka. Kwakweli sikufahamu kuwa hadi miaka ya dot.com bado watu wanakataa ujauzito na watoto, really????
Wakati unafanya hilo tendo na huyo dada hukujua kuwa matokeo yanaweza kuwa nini??? Wako wapi vijana wanaojua thamani ya msichana na kumsubiri hadi siku ya harusi???? Wako wapi vijana wanaosimamia na kuamini wanayoyasema???
Vijana wa siku hizi wamejaa mashairi mazuri mno ya mapenzi, yaani maneno yao yanawamaliza kabisa wadada hata wakilokole wanajikuta wametoa yote. Inapotokea mimba basi huruka mita mia, kama sio yeye kabisa, mashairi ya kubembeleza yanageuka mikuki ya kuchoma moyo.
Umeshamkosea Mungu, Dada amepata mimba nijukumu lako kuutambua ujauzito huo na kuulea pamoja na mtoto. Wengine wanawashauri wasichana watoe mimba, na wasichana kwakutokujua lakufanya wanakubali. Nijambo la aibu Sana kukataa mimba na mtoto wako, na akishafika miaka 5 unajitutumua Mahakamani kumdai mtoto, mbaya Sana.
Wewe kijana unayesoma hapa, Mungu anajua ni watoto wangapi umewakataa. Tubu sasa mbele za Mungu na haraka uende ukaombe radhi kwa mama watoto wako na ukubali majukumu yako.
source: www.rosemarymazizi.blogspot.com