Wanaume, heshimuni urafiki hii sio Sawa

Ungeliwa vibaya sana binti, mtu anakwambia eti uende ukapaone kwake usiku na ww unaenda

Nilimuamini kwasababu niliona ana aminika halafu alisema tu upite upaone na Mimi sikutaka kukaa sana hata nusu saa haikuisha nikasema sio vizuri kukaa zaidii nisimtie majaribuni kaka wa watu niondoke ila yeye akaona kapata chaka
 
7913e7e1d04edd67247765bb13cd14fa.jpg
 
Na angefanikiwa mukaja kuwa wapenzi siku ya ndoa unreported tulianza kama marafiki date your friend.
 
Nilimuamini kwasababu niliona ana aminika halafu alisema tu upite upaone na Mimi sikutaka kukaa sana hata nusu saa haikuisha nikasema sio vizuri kukaa zaidii nisimtie majaribuni kaka wa watu niondoke ila yeye akaona kapata chaka
Kumbe ulijua kuna majaribu?
 
Nimesikitika sana rafiki yangu wa Miaka mingi alivyotaka kunigeuka

Niko mkoa x nimekuja nina Kama siku 3 nikamtonya best yangu kwamba nipo alipo bila hiyana akasema kadogo2 usiondoke bila kuonana na Mimi nikakubali wito kwasababu amekuwa rafiki yangu sana na hatujaonana Miaka miwili

Basi nikaitikia wito tukaonana alikuwa na mshikaji wake wakaagizia mbuzi katoliki tukala tukaenjoy na story mbili tatu, kufika saa3:20 nikamwambia best muda umeenda pia nasikia huku usalama mdogo wacha nirudi nilipotoka tutaonaa siku nyinginee ndio jamaa kuniomba nikaone alipoamia ili siku nyinginee nije

Nikauliza tu Kama usalama wa mimi kurudi nilipotoka utakuwepo akasema niondoe shaka anajuana na wengi,, basi mie huyo nikakubali tukaenda kwake, jamaa ana kageto chake cha kishikaji tukapiga story kidogo saa 4:15 nikamwambia muda umeenda niondoke sasa anitafutie Usafiri looohhapo ndio aliponiletea ungese pumbavu

Akaanza kung’ang’aniza nilale kwake akidai kuwa usiku umeenda sijui Hakuna usalama jamani sijawah kuchukia Kama nilivyochukuia hiyo siku… yaani nilitamani hata kumpiga maana mimi kule ni mgeni sipaelewi na ni usiku

Jamaa yule alifunga mlango mkubwa wa kutokea nikabaki koridoni masaa2 hataki niende ananilazimisha nilale, tuliendelea kubishana sana,, nilimtolea maneno magumu sana mwisho wa siku akaniruhusu nikaondoka

Nilichojifunza wanawake hawa wanaume tusiwaamini Hakunaga urafiki kati ya mwanaume na mwanamke period ni suala la muda tu

Kikawaida hakuna urafiki wa mwanaume na mwanamke hasa wakiwa wanavutiana
 
Na angefanikiwa mukaja kuwa wapenzi siku ya ndoa unreported tulianza kama marafiki date your friend.

Haiwezekani mimi na yeye kuwa wapenzi ( nilishawai kuwa na uhusiano na ndugu yake japo sio ndugu yake in such
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom