Mimi sijaona ulichojibu ndio maana nimeuliza, ingekuwa vyema kama ungenijibu swali langu moja kwa moja, nisaidie kunielewesha mjinga mimi namna huu mfumo una madhara kwa wanawake
1. Huu mfumo unatengeneza structure mbovu ya kijamii inayokinzana na matarajio au malengo ya ustawi wa jamii maendeleo ya wanawake na watoto. Mwanamke anawajibika kubeba majukumu ya kiume mwenyewe isivyo lazima na kuacha shughuli zake za kimsingi kama kuwa mlezi wa familia yake na mume wake na kukuza ustawi wa jamii.
2. Huu mfumo unatengeneza wanawake wasio na kaliba ya kike sababu unawalazimu kuishi kama vichaa ili kuendana na mazingira ya ulimwengu wa kisasa unaowashawishi kushindana na kila kitu. Matokeo yake wanawake wa sasa wanatumia muda mwingi sana kufanya mambo ambayo ni nje ya context ya uanamke na yanawapotezea muda na kufuta mantiki ya uwepo wa mwanamke katika jamii. Hii ni mbaya sana kwenye ustawi wa jamii especially katika makuzi ya watoto wa kike ambao wengi watakuwa victims katika mfumo ambao hawakuuchagua.
Imagine jamii ambayo Wanawake hawajafiti katika nafasi yao ya asili sababu ya kuchallenge wanaume matokeo yake hawawezi kuishi kama wanaume na hawajui namna ya kuwa wanawake sababu hawana role models wazuri katika jamii. Mfano tu ni wewe
Jadda nani ataweza kuishi na wewe kama mke kwa hizi tabia zako za maviburi na ujuaji plus majibu ya kishujaa ukijiona unayaweza na mjua yote.
3. Narrative ya mwanamke wa shoka inawatoa wanawake kwenye reli ya goals halisi za kike. Tazamia hawa mabinti wa sasa kwa kuwatazama watukuja kuwa mama wa familia ipi siku za baadae. Kwa namna walivyo unaona wanafanania na mama yako au bibi yako japo hata kwa asilimia 30 tu?
4. Mfumo huu unawaendesha wanawake at the expense of their mental health. Wengi wa wanawake wa kisasa taratibu wanaanza kuwa wendawazimu ( psychopaths) kimatendo. Wanatoa mimba sababu ya kushindwa kuwa wake na mama wa familia, wanakopa hata wasivyomudu kulipa, wanamatarajio makubwa yasioendana na uwezo wala hali zao etc. Hii inaongeza pressure ya msongo wa mawazo kwa wanawake wengi wa sasa.
5. Ukifuatilia takwimu za kiafya,magonjwa mengi ya sasa victims ni wanawake na sehemu kubwa ya haya magonjwa yamechangiwa na lifestyle ya sasa. Magonjwa kama Fungus,UTI,PID,kansa ya shingo ya kizazi, again stress na depression, vyote vikitokana na aina ya mahusiano wanayojenga na wanaume katika mfumo huu ambao wao hitazama maslahi tu.
6. Childless women pandemic. Kuna wanawake wengi kwa sasa kutokana na utoaji mimba uliopitiliza,matumizi ya contraceptives,kulala na wanaume wengi in search for money na aina zingine za kupuyanga zimewanyima nafasi ya kutulia sehemu moja na mwanaume wa kueleweka na kutengeneza watoto na familia. Mama zetu by the age 35 tayari ameshakuwa mama wa familia ya watoto wa 5,7 au 12. Miaka hii mwanamke wa miaka 35 amepanga chumba cha master bedroom,anaishi mwenyewe,ana madeni ya marejesho kama 20, amevurugwa,mlevi,mpenda zinaa,hana mtoto na ameshachelewa kuwa mama bora,akipata mtoto hapo atakuwa tu kazaa kama bata malezi ni zero.
7. Gharama za maisha kwa wanawake zinapanda sana. Zingatia tena hali ya miaka ya nyuma na sasa. Ghatama za mwanamke katika kujikeep well kwenye jamii zipo juu na akiwa pekee yake ndio balaa linazidi.
8. Pandemic of old homeless women. Hapa ninavyoandika kuna wanawake wanamiaka 45 wamepanga uswahilini huko wanaishi wenyewe bila mume wala watoto,hawana ramani wanafedheheka,wanatamani kuolewa hata na mzee wa miaka 70 ila anatokea wapi at that age. Imagine wamepanga sababu ya mfumo huu wa maisha. Tutarajie idadi hii kutripple by 2030 kuendelea huko mbeleni.
9. Usalama wa mwanamke katika huu mfumo maeneo ya afya, domestic violence, harassments, bullying, emotional damages, na hata kifo ni mdogo sana. Mwanamke yupo prone zaidi kupata haya matatizo akiwa katika maisha ya usimbe kuliko akiwa katika ndoa yake na familia.
10. Kiroho haya si maisha kabisa na hakuna sehemu kuna imani au dini imetambua mwanamke kuishi maisha ya kujitafutia na kujitegemea mwenyewe kwasababu huleta madhara ya kiroho mengi sana kama kumjaza na nafsi yake na chuki dhidi ya wanaume,kulea watoto kwa mlengo wa kushoto,kujaza watoto na upotofu,kulea kizazi cha wanaume ambao sio wajenzi wa jamii,na kadhalika.
Ningeendelea ila nadhani kwa tabia yako ya kudharau maoni ya wanaume utanikera kwa kusema nimeandika upuuzi na hiyo huwa inanikwaza sababu najua umesoma umeelewa ila shida yako kubwa ni accountability na kuwajibika huwa hauwezi unapenda ligi zaidi kuliko maridhiano.