Wanaume Haya Tuliyataka Wenyewe

Wanaume Haya Tuliyataka Wenyewe

wanawake walivyo sasa ni matokeo yetu sisi wanaume

Ila Kuna baadhi ya issue kama

👉 Elimu

👉 Kukua kwa teknolojia

👉 Mabadiliko kwenye ishu ya ustawi wa jamii

Imewafanya wanawake kubadilika ukilinganisha na zama za mababu na mabibi zetu,

Though kwenye kazi mbona zamani mabibi zetu hawakuwa watu wa kukaa nyumbn walikuwa wanaenda shambani kama kawaida, kukatia malisho ya mifugo, na kuangalia watoto ingawa bado mwanaume alisimama kwenye nafasi yake kama kawaida,

Wazee waliamini watoto wanavyo wafundisha kazi, plus utayari wa jando ule uliwafanya wasiogope sana wakifa watoto wataishi vipi,

Ukilinganisha na sasa unakuta mtoto au kijana mpka wa miaka 30 baadhi hawajui kazi hata kusukuma mkokoteni hawezi, au kulima, ama ujuzi wowote ana pengine cheti Cha chuo au wengine waliishia njian lkn maisha ya kwao hayakumfanya afunguke akili ndo unakuta mzazi anawaza hayo,

Kingine sasa hivi kina mama nao hawana misimamo ile haiba na aibu ya uanawake hawana, kipindi Cha nyuma wanawake maybe akifiwa na mumewe walio wengi kama ana watoto watatu wanne, kuolewa ni ngumu, atabaki bomani kulinda na kupambania familia yake,

Ila wamama wa sasa hivi mtu anaolewa na mwanae wote wanaolewa, ndo maana inafanya wanaume tunawaza watoto wetu ikiwa umekufa kwenye umri ambao bado mtoto ni tegemezi kwa mzazi,
 
Zamani swala na digidigi walikuwa wakimulikwa na tochi wanaanza kuufuata ule mwanga na kujikuta wapo mikononi mwa wawindaji kiurahisi mno.

Sasa hivi wamesha elimika ukiwamlika na tochi utaambulia vumbi tu.Ndivyo ilivyo kwa wanawake wa sasa baada ya wanaume kuwapa mwanga huo wa elimu sasa hivi hao wanaume wanaambulia majuto makubwa kuliko mwanamke mwenyewe.

ukisoma mara2 hivi unaweza kuelewa
Mfano mzuri sana huu
 
Kama madhara yapo kwa wanaume zaidi

Je ambao hulalamika hizi mambo ni wanaume au wanawake?

Tuwe wakweli tu!
Wanaume wa sasa ukilinganisha na wazamani nadhani wa sasa wana advantage zaidi.

Wanawake wengi wanalea watoto pekee yao this means wanaume hawana gharama au bajeti ya malezi ya watoto sababu wanawake wametaka kubeba majukumu wenyewe.

Wanaume wa sasa anaweza asiwaze kujenga kwa gharama pesa zake akatia kwenye biashara.

Kiafya mwanaume kuishi sehemu moja na mwanamke m'moja huwa ina madhara makubwa sana ya kiakili na kimwili. Magonjwa mengi kama sonona,moyo,stroke,kisukari,tezi dume, na kadhalika ukichimbua yana changiwa sana na kuishi na mwanamke mpelekeshaji au mjuaji. Na ndio maana wanaume wengi walikufa mapema sana chanzo ni hayo magonjwa. Kwasasa hiyo hali kama inapungua sana sababu wanaume wengi wanaishi wenyewe.

Mwanaume ana matumizi madogo sana ukilinganisha na mwanamke. Kichwa cha mwanaume kwa mfano,kwa mwezi kinaweza kutumia 10,000 kunyoa. Ila mwanamke inaweza fika hata 300,000. Sijagusia maeneo mengine ambayo huu mzigo alibeba mwanaume pekee yake kwasasa wanaume wengi hawafanyi huo upuuzi na hii ni advantage kwao.

Kwa kifupi mwanaume ana vingi vya kugain kwenye huu mfumo mpya wa wanawake wenye viburi tofauti na zamani vile.
 
Zamani swala na digidigi walikuwa wakimulikwa na tochi wanaanza kuufuata ule mwanga na kujikuta wapo mikononi mwa wawindaji kiurahisi mno.

Sasa hivi wamesha elimika ukiwamlika na tochi utaambulia vumbi tu.Ndivyo ilivyo kwa wanawake wa sasa baada ya wanaume kuwapa mwanga huo wa elimu sasa hivi hao wanaume wanaambulia majuto makubwa kuliko mwanamke mwenyewe.

ukisoma mara2 hivi unaweza kuelewa
Nimekuelewa vema sana.
 
Nakataa hii kitu, mimi nina ushahidi wa famikia yetu, mama alianza kupata kazi kabla ya mama na wote wakawa wafanyakazi, na mama alikuwa anamuheshimu baba kwa hali zote
Mwanamke mwema hutoka kwa Mungu na changamoto inayotokea ni kwamba tunachagua mwanamke kwa utashi wetu siyo kumshirikisha Mungu
Awe msomi, assume kama hiyo ni tabia yake itajionesha tu, na hatujipi muda wa kufuatilia familia za tunaowaoa, na hii imekuwa mwiba mchungu kwa familia nyingi
Kwahiyo ni jukumu letu kuhakikisha watoto wetu tunawalea katika maadili ili wasije kuingia mkumbo kama unaotukuta sisi
Dunia imevaa bukta, kila mtu hajali
,
Hapo unazungumzia mama yako ambae ni mwanamke wa miaka ilee. Kuna hichi kizazi cha sasa mkuu akimudu kula na kubadilisha kijora na wigi anaona kamaliza kila kitu na hakuna mwanaume anaemsumbua. Kwasasa mambo yamebadilika sanaa ni 1in 100 ndo unaweza kukuta amesoma au ana kipato na akaheshimu ndoa.
 
Nyanja zote za maisha zimekuwa zikibadilika kwa kasi kuanzia karne ya 20, hasa kufuatia uvumbuzi wa computer.

There will be more chaos until an external force arrives to change the dynamics of everything, to return order.

A great RESET.
 
Wanaume wa sasa ukilinganisha na wazamani nadhani wa sasa wana advantage zaidi.

Wanawake wengi wanalea watoto pekee yao this means wanaume hawana gharama au bajeti ya malezi ya watoto sababu wanawake wametaka kubeba majukumu wenyewe.

Wanaume wa sasa anaweza asiwaze kujenga kwa gharama pesa zake akatia kwenye biashara.

Kiafya mwanaume kuishi sehemu moja na mwanamke m'moja huwa ina madhara makubwa sana ya kiakili na kimwili. Magonjwa mengi kama sonona,moyo,stroke,kisukari,tezi dume, na kadhalika ukichimbua yana changiwa sana na kuishi na mwanamke mpelekeshaji au mjuaji. Na ndio maana wanaume wengi walikufa mapema sana chanzo ni hayo magonjwa. Kwasasa hiyo hali kama inapungua sana sababu wanaume wengi wanaishi wenyewe.

Mwanaume ana matumizi madogo sana ukilinganisha na mwanamke. Kichwa cha mwanaume kwa mfano,kwa mwezi kinaweza kutumia 10,000 kunyoa. Ila mwanamke inaweza fika hata 300,000. Sijagusia maeneo mengine ambayo huu mzigo alibeba mwanaume pekee yake kwasasa wanaume wengi hawafanyi huo upuuzi na hii ni advantage kwao.

Kwa kifupi mwanaume ana vingi vya kugain kwenye huu mfumo mpya wa wanawake wenye viburi tofauti na zamani vile.
Nakubaliana na maoni yako endapo mwanamke ataishi mwenyewe

Ila kama mwanamke akiwa ndani ya ndoa ni mtihani sana kama huo uliosema,ujuaji mwingi,na kutaka kushindana na mwanaume

Nawapa kongole wanawake ambao mna elimu yenu na vipato vyenu na bado mkajua nafasi yenu katika ndoa na mkatambua nafasi ya mume pia
 
Wanapamba kama Malkia wa Nguvu 🤣ufanyaji wa kazi wa wanawake ni wa kitapeli..Mtu akizaa anaenda maternity leave ,akirudi anaondoka masaa mawili kabla hapo mwaka umeisha hivyo ,mtoto akiumwa bado ana excuses ...Yaani hao watu baadhi ya sehemu hawawezi kuajiri kabisa ni tabu mwanzo mwisho.

Wanapenda kuwa mbele mble ila utendaji ni zero labda ukute mtu mkubwa , kuanzia miaka 40 ila hivi vitoto zinasumbua sana ..Yaani mkeo anahanishwa kigoma wewe uko Dar ,hapo kama ni ndoa ishakuwa ni gharama ni utapeli mtu kwa karne hii kuoa mfanyakazi.
 
Wanapamba kama Malkia wa Nguvu 🤣ufanyaji wa kazi wa wanawake ni wa kitapeli..Mtu akizaa anaenda maternity leave ,akirudi anaondoka masaa mawili kabla hapo mwaka umeisha hivyo ,mtoto akiumwa bado ana excuses ...Yaani hao watu baadhi ya sehemu hawawezi kuajiri kabisa ni tabu mwanzo mwisho.

Wanapenda kuwa mbele mble ila utendaji ni zero labda ukute mtu mkubwa , kuanzia miaka 40 ila hivi vitoto zinasumbua sana ..Yaani mkeo anahanishwa kigoma wewe uko Dar ,hapo kama ni ndoa ishakuwa ni gharama ni utapeli mtu kwa karne hii kuoa mfanyakazi.
Hayo mazingira uliyosema yanadhibitisha nature ya mwanamke ni kutafutiwa na sio kutafuta,kwasababu hata akikomaa kutafuta bado kuna sababu lukuki za kutofanya kwa silimia mia moja
 
View attachment 3318660


Huko nyuma wazazi wetu na wazee wetu waliishi na bibi zetu na mama zetu,hali ya kuwa wanaume ndio watafutaji na ilikuwa hivyo siku zote,wala hawakuhofia sijui sisi tukifa watoto wetu wataishi vipi?

Kwasababu anayetoa riziki ni Mungu,kwahiyo hata kama hao walipo kufa Mwenyezi Mungu aliendelea kuipa riziki familia kwa namna anayojua yeye,na watu waliendelea kuishi na watu wakakua vizuri tu

Kimekuja kizazi ambacho kina woga wa maisha,wakaanza kubadilisha nidhamu ya ulimwengu huu,maana hapo awali nidhamu ilikuwa baba au mwanaume ndio mtafutaji na mama au mke analea familia

Sasa kizazi hiki kikaona nidhamu hii imepitwa na wakati,wakahofia maisha na kuhisi kwamba wao wanaume wakifa basi familia zao zitapata shida,wakasahau kabisa kwamba riziki inatoka kwa Allah

Sasa wakaanza kuona mwanamke nae ajishughulishe achangie upatikane mkate wa familia,na kweli baada ya wanawake kuona wanashinikizwa wachangie kulisha nao wakaanza kufanya hivyo

Kama haitoshi kizazi hiki cha wanaume ambao ni waoga wa maisha,wakaona hapana kuoa mwanamke ambaye ni wa darasa la saba au ambaye hajasoma sio sawa,inabidi waoe wake wasomi,basi dada zetu wakaona isiwe tabu nao wakafungua vitabu na alhamdulillah wana stashahada zao,shahada na shahada za uzamivu

Sasa ambacho hawakujua hiki kizazi cha wanaume waoga wa maisha kuwa,mwanamke wa zamani alikuwa mtiifu kwa mumewe kwasababu alikuwa anamtegemea mumewe kwa kila kitu,ndio maana walikuwa wenye nidhamu na adabu

Hawakujua kwamba baada ya mwanamke kusoma na kuingiza kipato,itafika kipindi ataweza kujitegemea na hivyo hato muhimtaji mwanaume tena kama zamani,kwani nae anauwezo wa kupata mkate wake wa kila siku

Matokeo yake leo hii,walio oa wanawake walio soma wanalia na walioa wanawake wenye kipato pia wanalia,wamesahau kwamba haya mazingira wametengeneza wao wenyewe


Na riziki ndio imekuwa mtihani kweli kweli,kwa maana vipato havina baraka kwasababu hamu mtegemei Mwenyezi Mungu sasa ila mnategemea kazi zenu ndio zitaendesha maisha yenu,matokeo yake tunaenda resi sana lakini mwisho wa siku mishahara haikutani,yaani lazima utakuwa na madeni tu

Na mlibugi zaidi kwakutojua kwamba mwanamke ni malikia ameumbwa ili ahudumiwe na sio yeye ahudumie,ndio maana kutwa kuchwa mnalalamika mwanamke anakipato kikubwa lakini hakuna anachochangia ndani,hamjui kwamba mwanamke sio asili yake kuprovide bali tuna wafosi tu

Kwahiyo haya tuliyataka wenyewe,tumeoa wasomi wanatuendesha,na tumeoa wajasilia mali wanatuendesha,kwahiyo buddies tukae kwa kutulia na tunapambane na hali zetu

Haya hayakutokea kwa bahati mbaya ila tuliyatafuta wenyewe na sasa tuishi nayo

Na wanawake wakazidi kujiongeza kwa kutaka haki sawa zaidi kwahiyo yajayo yanafurahisha

Ni hayo tu!
Sijajua kama mawazo yako yamejikita katika mrengo wa kidini au unafuata uhalisia kwa kuakisi maisha halisi ya jamii za kiafrika.
Kwa jamii nyingi za Tanzania ninazozifahamu mimi hasa jamii za wakulima mzalishaji mkuu katika ngazi ya familia alikuwa mwanamke.
Ingawa kinadharia wengi waliamini mzalishaji mkuu ni mwanaume ila kiuhalisia mzalishaji mkuu wa familia alikuwa mwanamke akishirikiana na watoto wake.
Mwanamke na watoto wake ndiyo wataandaa mashamba, watalima na kupalilia kisha mwanaume huwa anakuja kushiriki kikamilifu wakati wa mavuno na mauzo ya mazao yaliyopatikana.
Najua utajiuliza ilikuwa mwanaume alionekana kuwa yeye ndiye provider mkuu wa familia ilihali yeye sio mzalishaji mkuu katika familia?
Mambo yalikuwa hivi; Mwanaume alishiriki katika mavuno na mauzo ya mazao na pesa iliyopatikana ilikuwa inatumika kwa maelekezo ya mwanaume. Yaani kwa kifupi mwanaume ndiye alikuwa muhasibu, store keeper na afisa masoko.
Mama akitaka kununua mafuta ya taa, chumvi pesa anaenda kuomba kwa Baba na ikihitajika watoto kulipiwa ada basi baba atapakiza mahindi debe kadhaa kwenye baiskeli anakwenda kuuza na fedha ndiyo inapelekwa kwenda kulipa ada.
Kwa kifupi kazi ngumu kuchota maji umbali mrefu, kutwanga nafaka hadi kupata unga, kutafuta kuni n.k. alifanya mwanamke kwakuwa hata kibaiolojia mwili wa mwanamke japo hauna misuli kama mwanaume lakini miili yao inavumilia shida kuliko mwanaume na mwanaume alifanya kazi zinazohitaji akili zaidi
Hii ilisaidia wanaume wa kipindi hicho kuishi miaka mingi zaidi kwakuwa hawakuwa na msongo wa mawazo na wala miili yao haikushughulishwa sana na kuchakaa kama sasa hivi ambapo tulidanganywa kuwa mwanaume anatakiwa afanye kila kitu jambo ambalo lipo nje ya uwezo wake.
Ukitaka kuamini hiki ninachokisema fuatilia jamii za wakulima utaona ni kwa namna gani wanawake zao ni watu wenye nguvu na fuatilia nani anashiriki kuizalishia familia.
Matokeo ya mfumo huu wa kisasa yamepelekea jamii kuwa na wajane wengi kuliko wagane tofauti na ilivyokuwa hapo awali kwa wanaume kuwa too exposed kwenye risk za kupoteza uhai wakipambania familia zao.
Hata ukienda kwa simba, jike ndiyo mwindaji.
Kilichofanyika na waliobadili mifumo ni kuchukua BMW na kuzipeleka kiwangwa kubeba mananasi na kuziacha toyota hilux zikitembea kwenye lami posta
 
Sasa unasema ana akili finyu wakati unamkuta mtu ana elimu ya kutosha?

Ukienda kinyume na asili lazima utakutana na yasiyo kufurahisha

Kwanini huwa tunamheshimu boss?

Kwakuwa amebeba hatima yetu ndio maana tunajua tukizingua kinanuka

Sasa na ndoa nayo iko hivyo hivyo,mke akikutegemea atakaa kwa kutulia
Kitabu kina elimu ila hakina akili
 
Sijajua kama mawazo yako yamejikita katika mrengo wa kidini au unafuata uhalisia kwa kuakisi maisha halisi ya jamii za kiafrika.
Kwa jamii nyingi za Tanzania ninazozifahamu mimi hasa jamii za wakulima mzalishaji mkuu katika ngazi ya familia alikuwa mwanamke.
Ingawa kinadharia wengi waliamini mzalishaji mkuu ni mwanaume ila kiuhalisia mzalishaji mkuu wa familia alikuwa mwanamke akishirikiana na watoto wake.
Mwanamke na watoto wake ndiyo wataandaa mashamba, watalima na kupalilia kisha mwanaume huwa anakuja kushiriki kikamilifu wakati wa mavuno na mauzo ya mazao yaliyopatikana.
Najua utajiuliza ilikuwa mwanaume alionekana kuwa yeye ndiye provider mkuu wa familia ilihali yeye sio mzalishaji mkuu katika familia?
Mambo yalikuwa hivi; Mwanaume alishiriki katika mavuno na mauzo ya mazao na pesa iliyopatikana ilikuwa inatumika kwa maelekezo ya mwanaume. Yaani kwa kifupi mwanaume ndiye alikuwa muhasibu, store keeper na afisa masoko.
Mama akitaka kununua mafuta ya taa, chumvi pesa anaenda kuomba kwa Baba na ikihitajika watoto kulipiwa ada basi baba atapakiza mahindi debe kadhaa kwenye baiskeli anakwenda kuuza na fedha ndiyo inapelekwa kwenda kulipa ada.
Kwa kifupi kazi ngumu kuchota maji umbali mrefu, kutwanga nafaka hadi kupata unga, kutafuta kuni n.k. alifanya mwanamke kwakuwa hata kibaiolojia mwili wa mwanamke japo hauna misuli kama mwanaume lakini miili yao inavumilia shida kuliko mwanaume na mwanaume alifanya kazi zinazohitaji akili zaidi
Hii ilisaidia wanaume wa kipindi hicho kuishi miaka mingi zaidi kwakuwa hawakuwa na msongo wa mawazo na wala miili yao haikushughulishwa sana na kuchakaa kama sasa hivi ambapo tulidanganywa kuwa mwanaume anatakiwa afanye kila kitu jambo ambalo lipo nje ya uwezo wake.
Ukitaka kuamini hiki ninachokisema fuatilia jamii za wakulima utaona ni kwa namna gani wanawake zao ni watu wenye nguvu na fuatilia nani anashiriki kuizalishia familia.
Matokeo ya mfumo huu wa kisasa yamepelekea jamii kuwa na wajane wengi kuliko wagane tofauti na ilivyokuwa hapo awali kwa wanaume kuwa too exposed kwenye risk za kupoteza uhai wakipambania familia zao.
Hata ukienda kwa simba, jike ndiyo mwindaji.
Kilichofanyika na waliobadili mifumo ni kuchukua BMW na kuzipeleka kiwangwa kubeba mananasi na kuziacha toyota hilux zikitembea kwenye lami posta
Maono yangu ni kijamii zaidi, niseme.kwamba nakubaliana na wewe kweli kuna baadhi ya jamii ambazo wanawake na watoto wanachakalika na wanaume wanakuwa wasimamizi,hilo sina shida nalo

Pamoja na jamii hiyo uliyoizungumzia lkn bado uliona baba ndie msimamizi mkuu wa mambo yote,kwahiyo hapo uongozi na mamlaka yaliheshimiwa na mambo yalienda sawa

Ukiacha jamii hiyo lkn kuna jamii ambayo wababa walikuwa watafutaji zaidi

Sasa jamii yetu ya leo hakuna mipaka ya kuheshimiana,mke nae anataka kuwa mume, je tunajenga jamii ya namna gani?

Kwahiyo kwa kumalizia nakubaliana na maoni yako kama ulivyoeleza
 
Kwasababu anayetoa riziki ni Mungu,kwahiyo hata kama hao walipo kufa Mwenyezi Mungu aliendelea kuipa riziki familia kwa namna anayojua yeye,na watu waliendelea kuishi na watu wakakua vizuri tu
Ndugu yangu..... Naomba nikukosoe kwa kukujenga
Kwanza , Mungu hashushi miujiza ya pesa kama vile zinaota kwenye miti bali kipindi hicho mazingira ya uchumi yalikuwa yanaruhusu extended family (Kaka wa marehemu, Wajomba na kadhalika na kadhalika) kubeba majukumu ya kulea watoto wa ndugu yao aliyetangulia mbele ya haki ; tulikuwa na utaratibu wa kukusanyika kama watoto kwa wajomba au Mashangazi kipindi cha likizo miaka ya 90 na 2000 mwanzoni na ndugu hawa walikuwa na disposable income ya kutosha kulisha Lundo kubwa la watoto ambao hata sio wao bila kinyongo ,sahizi huo utaratibu uko wapi? Wajomba wamekuwa waoga wa maisha?

Point Hapa sio UOGA bali ni UCHUMI
 
Kitabu kina elimu ila hakina akili
Nakubaliana na wewe kuna kusoma na kuelimika

Wengi wetu tumesoma lkn hatujaelimika

Na mfano mzuri ndio huu wa wasomi ambao wanategemea kufanya maamuzi mazuri kwa niaba ya jamii,lakini wao wanaingiza nchi katika mikataba ya ajabu kabisa
 
Zamani haikuwa bora kuliko sasa, na sasa sio bora kuliko zamani.

Tunapochukulia zamani kuwa bora zaidi ya sasa, tunafanya declinism bias. Ugumu wa maisha ya sasa unafanya tudhani ya zamani yalikuwa bora, ilihali hatukumbuki mengi.

Siamini kwamba zamani wanawake hawakuwa watafutaji. Bibi yangu alikuwa muuza pombe licha ya babu kuwa na kazi zake tayari.

Tatizo ni kwamba jamii haitaki kuwatambua wanawake kama watafutaji, visa vya wanawake watafutaji vimepotea kwenye historia ambayo wanaume tu ndo wanaandika.

Pia dini nazo huchochea mifumo kandamizi.

Mtazamo wangu ni kwamba wanaume wanaochukia wanawake wasomi ndo waoga wa maisha, hawataki kuishi kwa akili, wanafuata mapokeo tu, hawana fikra huru.

Changamoto hii ipo kwa wanawake pia.
 
Ndugu yangu..... Naomba nikukosoe kwa kukujenga
Kwanza , Mungu hashushi miujiza ya pesa kama vile zinaota kwenye miti bali kipindi hicho mazingira ya uchumi yalikuwa yanaruhusu extended family (Kaka wa marehemu, Wajomba na kadhalika na kadhalika) kubeba majukumu ya kulea watoto wa ndugu yao aliyetangulia mbele ya haki ; tulikuwa na utaratibu wa kukusanyika kama watoto kwa wajomba au Mashangazi kipindi cha likizo miaka ya 90 na 2000 mwanzoni na ndugu hawa walikuwa na disposable income ya kutosha kulisha Lundo kubwa la watoto ambao hata sio wao bila kinyongo ,sahizi huo utaratibu uko wapi? Wajomba wamekuwa waoga wa maisha?

Point Hapa sio UOGA bali ni UCHUMI
Hata leo mazingira ya uchumi yanaruhusu pia iwapo tutaacha ubinafsi

Leo hii hatuchangiani tunapoumwa lkn tunachangiana tunapokufa,tena utasikia ndugu mmoja anasema gharama za usafiri wa marehemu niachieni mimi,je wakati anaumwa alikuwa wapi?

Leo tunachangia sherehe kwakuwa tunajua tutakula monde na chakula

Kwahiyo hapa ni kutojali na ubinafsi kupitia jina la maisha yamebadilika
 
Wanapamba kama Malkia wa Nguvu 🤣ufanyaji wa kazi wa wanawake ni wa kitapeli..Mtu akizaa anaenda maternity leave ,akirudi anaondoka masaa mawili kabla hapo mwaka umeisha hivyo ,mtoto akiumwa bado ana excuses ...Yaani hao watu baadhi ya sehemu hawawezi kuajiri kabisa ni tabu mwanzo mwisho.

Wanapenda kuwa mbele mble ila utendaji ni zero labda ukute mtu mkubwa , kuanzia miaka 40 ila hivi vitoto zinasumbua sana ..Yaani mkeo anahanishwa kigoma wewe uko Dar ,hapo kama ni ndoa ishakuwa ni gharama ni utapeli mtu kwa karne hii kuoa mfanyakazi.
Huko mataifa ya magharibi wamekwisha lishtukia hili swala na wameanza kuchukua hatua. Unaweza kuta wahasibu wawili mwanaume na mwanamke wote wana level sawa ya elimu.

Ila mshahara ni tofauti sababu kule wenzetu mtu analipwa kwa uwezo wake wa kufanya kazi na saa za kazi anazokimbiza kazi zake.

Sasa mwanamke ukipima productivity yake eneo la kazi ndani ya mwezi utagundua siku ambazo yupo active ni chache sana compared na mwanaume.

Zifuatazo ni sababu kwann huwezi compare au linganisha uzalishaji wa mwanaume na mwanamke eneo la kazi.

1. Mwanamke ana ziku za mwezi ama period ambazo huleta hitilafu za kisaikolojia na kumfanya akose focus ya kawaida eneo la kazi.

2. Mwanamke ana response ya haraka ya pressure tofauti na mwanaume. Unabisha,muweke mwanamke mrembo na mwanaume kwenye gari,pandisha vioo,halafu usiwashe AC,utaona nani atakuwa wa kwanza kulalamika joto na hewa nzito.

3. Mwanamke anaitazama pesa kama kitu cha kupewa na stahiki yake hata pale ambapo hajaifanyia kazi tunayaona haya eneo la mahusiano ambapo mwanamke unakutana nae leo, dakika chache anaomba umpe anachotaka as if mna mnajuana sana. Eneo la kazi ni same story, wanawake hutazamia kulipwa zaidi na bila kujua mashirika na taasisi hulipa zaidi wanawake kuliko wanaume.

Kwa maneno mengine ni gharama zaidi na less productive kumuweka mwanamke kwenye kazi za kiume ambazo kuna wanaume wengi ambao wapo willing kuzifanya kwa bei nzuri bila marupurupu na wanafanya huku wanaenjoy.
 
View attachment 3318660


Huko nyuma wazazi wetu na wazee wetu waliishi na bibi zetu na mama zetu,hali ya kuwa wanaume ndio watafutaji na ilikuwa hivyo siku zote,wala hawakuhofia sijui sisi tukifa watoto wetu wataishi vipi?

Kwasababu anayetoa riziki ni Mungu,kwahiyo hata kama hao walipo kufa Mwenyezi Mungu aliendelea kuipa riziki familia kwa namna anayojua yeye,na watu waliendelea kuishi na watu wakakua vizuri tu

Kimekuja kizazi ambacho kina woga wa maisha,wakaanza kubadilisha nidhamu ya ulimwengu huu,maana hapo awali nidhamu ilikuwa baba au mwanaume ndio mtafutaji na mama au mke analea familia

Sasa kizazi hiki kikaona nidhamu hii imepitwa na wakati,wakahofia maisha na kuhisi kwamba wao wanaume wakifa basi familia zao zitapata shida,wakasahau kabisa kwamba riziki inatoka kwa Allah

Sasa wakaanza kuona mwanamke nae ajishughulishe achangie upatikane mkate wa familia,na kweli baada ya wanawake kuona wanashinikizwa wachangie kulisha nao wakaanza kufanya hivyo

Kama haitoshi kizazi hiki cha wanaume ambao ni waoga wa maisha,wakaona hapana kuoa mwanamke ambaye ni wa darasa la saba au ambaye hajasoma sio sawa,inabidi waoe wake wasomi,basi dada zetu wakaona isiwe tabu nao wakafungua vitabu na alhamdulillah wana stashahada zao,shahada na shahada za uzamivu

Sasa ambacho hawakujua hiki kizazi cha wanaume waoga wa maisha kuwa,mwanamke wa zamani alikuwa mtiifu kwa mumewe kwasababu alikuwa anamtegemea mumewe kwa kila kitu,ndio maana walikuwa wenye nidhamu na adabu

Hawakujua kwamba baada ya mwanamke kusoma na kuingiza kipato,itafika kipindi ataweza kujitegemea na hivyo hato muhimtaji mwanaume tena kama zamani,kwani nae anauwezo wa kupata mkate wake wa kila siku

Matokeo yake leo hii,walio oa wanawake walio soma wanalia na walioa wanawake wenye kipato pia wanalia,wamesahau kwamba haya mazingira wametengeneza wao wenyewe


Na riziki ndio imekuwa mtihani kweli kweli,kwa maana vipato havina baraka kwasababu hamu mtegemei Mwenyezi Mungu sasa ila mnategemea kazi zenu ndio zitaendesha maisha yenu,matokeo yake tunaenda resi sana lakini mwisho wa siku mishahara haikutani,yaani lazima utakuwa na madeni tu

Na mlibugi zaidi kwakutojua kwamba mwanamke ni malikia ameumbwa ili ahudumiwe na sio yeye ahudumie,ndio maana kutwa kuchwa mnalalamika mwanamke anakipato kikubwa lakini hakuna anachochangia ndani,hamjui kwamba mwanamke sio asili yake kuprovide bali tuna wafosi tu

Kwahiyo haya tuliyataka wenyewe,tumeoa wasomi wanatuendesha,na tumeoa wajasilia mali wanatuendesha,kwahiyo buddies tukae kwa kutulia na tunapambane na hali zetu

Haya hayakutokea kwa bahati mbaya ila tuliyatafuta wenyewe na sasa tuishi nayo

Na wanawake wakazidi kujiongeza kwa kutaka haki sawa zaidi kwahiyo yajayo yanafurahisha

Ni hayo tu!
Wafuasi wa muudi na ukandamizaji wa jamii ya wanawake na ubokoharamu ndio zao,maelezo yote ya nini si ungesema tu ile kauli yenu haramu mwanamke kusoma na kufanya kazi kama watalibalin wenzako walivyofanya.

Upuuzi mtupu.
 
Kimekuja kizazi ambacho kina woga wa maisha,wakaanza kubadilisha nidhamu ya ulimwengu huu,maana hapo awali nidhamu ilikuwa baba au mwanaume ndio mtafutaji na mama au mke analea familia
Lawama unazozitupia kizazi uzielekeze kwa serikali yako ambayo ndio responsible kwa kupanga uchumi ; majukumu ya Baba kwenye nyumba yalibaki pale pale wakati pesa anayozalisha iliendelea kupukutika thamani; mwanamke kutoka ndani ya nyumba sio kwasababu mwanaume ametaka bali kwasababu serikali yako imefuata sera za kilibelari za magharibi ; serikali imewatoa wanawake zetu ndani na sio sisi maana itafika muda familia kuwa na kipato kimachozalishwa na mzazi mmoja ni impossible
 
Back
Top Bottom